News Details

Kulaani Vikali Ubaguzi Na Unyanyasaji Uliofanywa Na Jeshi La Polisi Dhidi Ya Wanaharakati.

 

Mtandao wa #WenyeNchiWananchi unaohusisha wananchi mbalimbali wakiwemo wanaharakati inalaani vikali vitendo vya ubaguzi na unyanyasaji vilivyofanywa na jeshi la polisi dhidi ya wanaharakati na wasomi waliofika Mwanza kwa ajili ya Kongamano kuhusu Katiba Mpya na kupinga mkataba mbovu wa DP World wa kuchukua bandari zetu (Kampeni #OkoaBandariZetu)
Kwa mujibu wa wajumbe kati ya tarehe 02 hadi 04 Oktoba 2023, wao binafsi na wahusika mbalimbali wakiwemo watoa huduma walinyanyaswa na kuhujumiwa kupitia vitisho vilivyofanywa na Jeshi la Polisi. Baadhi ya matukio makuu muhimu yalikuwa yafuatayo:

0 Comment

Leave a Comment