Updates

SHERIA YA BIMA YA AFYA KWA WOTE YA MWAKA 2023

Sheria kwa ajili ya kuweka masharti ya kuwezesha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi kupitia bima ya afya, kuanzisha mfumo wa bima ya afya kwa wote, kuweka masharti ya kupanua wigo wa huduma mbalimbali za afya; na kuweka masharti mengineyo yanayohusiana na hayo. Read More

Read More Download Document

YUKO WAPI DR MPANGO?  Where is Dr Mpango ?

Hili swali sasa limefika hatua mbaya kidogo, serikali imekuwa na utamaduni wa kudanganya kuhusu wapi walipo viongozi au safari wanazofanya viongozi, Kwa mwezi sasa Dr Mpango haonekani, lakini pia amewakilishwa kwenye shughuli alizotakiwa kufanya kama Makamu wa Rais, Dr Mpango haonekani popote na wasiwasi umeanza kuwa mkubwa, kuna mengi yanasemwa mfano Yuko kwenye Matitabu Korea Kusini na wengine wanasema yuko Israel kwa matibabu, Lakini hayo yote sio muhimu, kwa nini Dr Mpango asijitokeze kutuliza hali hii ambayo imejenga wasiwasi wenye haki miongoni mwa wananchi ?Juzi ameibuka  Waziri Mkuu na kusema Dr Mpango yuko nje ya nchi kwa majukumu bila kusema ni majukumu gani na wapi imeleta shida kubwa kuliko ya awali. Waziri Mkuu anadanganya umma, Kwa sababu kama Mpango yuko nje ya nchi, yuko wapi na anafanya nini? Toka lini Taarifa kama hii ikawa ni siri kwa umma? Toka lini makamu wa Rais akaenda nje ya nchi kwa mwezi mzima na kusiwe na Taarifa yoyote maalum kwa umma? Kwa uchunguzi uliofanyika (kupitia wadau mbalimbali ) ,kuanzia uwanja wa ndege na kwa  wananchi na wafanyakazi wanaofanya shughuli zao uwanja wa ndege, hakuna anayesema kaona makamu akisafiri, kama Dr Mpango yuko nje ya nchi hakutoka kwa njia za kawaida. Hii inaashiria labda anaweza kuwa mgonjwa kwa kuwa hakuna uwanja wa ndege wenye kumbukumbu ya kumuona Mpango kwa mwezi sasa. Je alisafiri vipi kwenda nchi za nje na kusiwe na TAARIFA kwenye uwanja wa ndege wowote? Kwa nini Majaliwa hakusema Dr Mpango yuko nchi gani kwa shughuli gani ? Alichofanya Majaliwa ni kusema tu hayuko nchini ili kuondoa swali la kwanini ajaenda Katesh na Hanang kwenye maafa sababu yenye ni kiongozi namba mbili pale Rais anapokuwa nje ya nchi. Lakini hata ili la maafa ajaonekana wala kuzungumza chochote ? Yuko wapi Mpango? Kama wananchi tunahoji Dr Mpango anafanya shughuli gani nje ya nchi mwezi mzima hakuna picha wala video moja, hakuna hata Taarifa tu kwenye media yoyote kuonyesha shughuli za Makamu wa Rais kwa mwezi mzima,  Hii inawezekana vipi? Lakini pia hakuna shughuli yoyote ya kiserikali kwenye maeneo yaliyozoeleka, barabara anazotumia Dodoma na Dar hakuna msafara wake umeonekana, Kanisani hayupo , Dr  Mpango ni wa kuacha kusali mwezi mzima?  Kwa nini serikali inaficha jambo hili? Kauli ya Waziri Mkuu Dr Mpango kuwa nje ya nchi imeibuwa wasiwasi na Maswali mengi zaidi Babati , Hanang na Kateshi huko Manyara kumetokea mtikisiko ambao umesababisha maafa na uharibifu wa miundo mbinu mbalimbali Hanang na Katesh, Inasadiliwa kwamba ni volkano inalipuka lakini serikali hapa pia inaonekana kuficha taarifa ili tope jepesi linalotembea ni nini? Ni kama Serikali imedanganya na kusema ni mafuriko ili kupoza na kuondoa wasiwasi kwa wananchi bila kujali kama tukili linaweza jirudia. Toka lini mvua ni matope laini vile? Je mvua ina uwezo wa kuporomosha mawe makubwa kutoka milimani na mlima kumwagika hayo ni mafuriko au kuna taarifa zilizojificha? Hoja hii ya  Hanang na Katesh inaturudisha kwenye Hoja ya Mpango, kama Yuko nchini kwa nini asijitokeze kutembelea wahanga si mlisema yuko LIKIZO? anaendelea na LIKIZO? ili kuondoa hoja ya yuko LIKIZO ndipo Majaliwa ametumika kusema Mpango yuko nje ya nchi, Tunakuwa na waziri Mkuu asiye muwazi kwa nini?  Hii inatukumbusha pia kipindi wananchi wanaulizia alipo Hayati Magufuli ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa yupo vizuri ana anaendelea na majukumu yake ya kawaida kuwa hatuwezi kukutana na Rais Kariakoo,  lakini matokeo yake kila mtu aliyashuhudia kuwa Rais alipatwa na umauti.  Majaliwa anasema mitandao inasema uongo? inasema uongo gani? kwa Mpango ameonekana lini mara ya mwisho? Watu wanauliza alipo Mpango kwa sababu ni kiongozi ana dhamana ya ofisi wananchi wanatakiwa kujua viongozi wao wako wapi na wanafanya nini. Inakuwa  hivi ili kuwakinga viongozi. Kusema Mpango yuko Nje ya nchi haitoshi, lazima Mpango mwenyewe ajitokeze na kusema yuko wapi anafanya nini? Majaliwa ana sababu gani kufafanua alipo mtu HAI akiendelea na shughuli zake kama kawaida? kuna ugumu gani kwa serikali kuridhisha umma kwenye swali la msingi kabisa ya kwamba, Makamu wa Rais yuko wapi? ni swali linatakiwa kujibiwa na Mpango mwenyewe sio wasaidizi wake wala waziri Makuu. Ni Makamu wa Rais pekee ndiye anayetakiwa kuondoa wasiwasi huu ambao unaweza kuwa na nia njema au ovu haijalishi lakini cha msingi ni lazima wananchi wapate kujua alipo huyu kiongozi tena kwa kuona na kusikia kauli yake. #ChangeTanzania Download Now

Read More Download Document

MADHARA YA KUFUTA UMILIKI NA KUUZA KWA MTU MWINGINE  NAMBA ZA SIMU ZINAPOKAA MIEZI 3 BILA KUTUMIKA.

Kuna utaratibu mbaya sana umewekwa namna ya usimamizi wa namba SIMU zinapokaa miezi mitatu bila kutumika, Utaratibu huu umelalamikiwa sana na pande zote. Yaani wale wanaopewa hizo laini bila kujua kwamba ilikuwa ni namba ya mtu hapo awali hivyo anaanza kupokea simu na message nyingi zisizo muhusu, hii ikiwa ni pamoja na kupigiwa simu kuitwa kwenye vikao na vikundi ambayo ahusiki navyo. Lakni kwa Upande mwingine mmiliki wa hiyo simu hapo mwanzo anapoteza kabisa mawasiliano yake ya namba hiyo kwa kuwa umiliki unaama na kuwa wa mtu mwingine,  lakini mara nyingi WhatssApp inabaki kwa mtu wa zamani na mmiliki mpya anaweza kutumia message za kawaida na kupiga simu pamoja na huduma za miamala. Mara nyingi kwa kuwa namba hii inakuwa imetumika kwenye mifumo mingi, mmiliki mpya hawezi kuitumia hiyo namba kwenye mambo mengi na kujikuta anasajili namba mpya.Kwa watu wanaowasiliana na namba hiyo, mfano umetuma ujumbe wa kawaida unakwenda kwa mmiliki mpya, lakini ukitumia WhatsApp message inakwenda kwa mmiliki wa zamani. Hasara na hatari ya suala Hili masuala na taarifa nyingi za mmiliki wa zamani zinakwenda kwa mmiliki mpya, hivyo kama mmiliki mpya ni tapeli anakuwa amepata taarifa nyingi sana zikiwemo za kibenki na kadhalika. Hili suala linalalamikiwa sana, wengi wanasema namba inapofungwa asipewe mtu mpya bali iachwe mpaka itakapo sajiliwa tena na mmiliki yule yule, kwa sababu kuna watu wanafika hatua wanashindwa kumiliki simu ya mkononi hivyo kutotumia laini ya simu hiyo kwa muda, kuna watu wanasafiri nje ya nchi, wengine wanaugua na kuzima simu kwa muda, namba hizo zote zinafugwa na kuuzwa tena. Sheria  hii inahitaji kuboreshwa ili kulinda usiri wa watumiaji wa simu na mifumo ya kidigitali. Changamoto ya laini isipotumiwa kwa miezi mitatu laini hiyo inatolewa au kuuzwa kwa mtu mwingine. Muda wa miezi mitatu ni mchache sana kwa kitendo kama hicho kufanywa na makampuni ya simu. Kuna sababu za msingi ambazo zinaweza kupelekea mtumiaji wa laini kutokuwa hewani kwa miezi mitatu kama vile Magonjwa , kusafiri kibiashara, kufilisika, kuwa maeneo yasiyo na mtandao husika , kukaa mahabusu, kuwa mashuleni kwa wanafunzi au kupitia changamoto ambazo unakuwa huna simu ya mkononi kwa wakati huo, hivyo si sahihi Laini ya simu kuuziwa mtu mwingine. Kwa mfano  benki  usipotumia akaunti inafungwa lakini jalada linabaki kuwa lako, wanaweza kutoza kiasi chs fedha kurudisha hiyo akaunti baada ya kuandika barua au kuwataarifu kuwa unaomba akaunti yako irudishwe, lakini namba ya SIMU yenye mawasiliano na taarifa nyingi za mtu inaweza kuuzwa baada ya miezi mitatu.  Ni hali ya kushangaza kwamba unawezaje kuuza namba ambayo tayari imetumika? Inafahamika mtu anaposajili laini ya simu anatumia kitambulisho cha taifa ambacho kina taarifa zake zote, pili kipindi cha matumizi ya laini hiyo watu hutunza mambo mbalimbali katika simu zao ambayo pengine ni ya siri kutoka kwa mwajiri wake, mchumba wake, mkewe au mumewe, Daktari wake nk. Ni jambo lisilowezekana kwa mtu laini yake inapouzwa au kufungiwa kueleza watu wote kwamba yeye si mtumiaji wa simu hiyo tena.  Kufungwa kwa laini ndani ya miezi mitatu ni faida mojawapo waliyoipata matapeli wa mtandaoni kutapeli watu, watu hao wakijua wanatuma pesa kwa mtumiaji wa namba aliyepita ambaye wanamfahamu kumbe siye na namba hiyo kapewa mtu mwingine. Sheria mbovu za mawasiliano  zimeleta mkanganyiko mbaya sana katika jamii, ili hali tuna Waziri anayeweza kushughulikia changamoto hii mara moja. Ingekuwa ni vyema namba zinazovunjwa kuwekwa kando na kama mtumiaji wa namba hiyo akitaka kuirudia namba yake iweze kufufuliwa na kuendelea na matumizi yake. Hii inasidia kulinda haki za mtumiaji ambazo zimeainishwa na sheria.  Hali hii inasababisha watu kusajili namba mpya kila mara na hii inauwa uimara, muendelezo  na utulivu wa mawasiliano. Hii ni hasara pia kwa makampuni ya simu kuzalisha laini kwa gharama kila wakati. Sheria hii haijazingatia ustawi wa kiuchumi na jamii kwa undani, tunaamini mawasiliano imara ndio nguzo kubwa ya mambo mengi ya kiuchumi, mtu anapapota changamoto ya kutotumia laini ya simu kwa miezi mitatu ni wazi watu wake wote wa biashara walimtafuta kwa namba hiyo hivyo anahitaji kufanya mwendelezo wa alipoishia ili kuepuka kupoteza muda na kukosa watu wengine ambao kisingi wana mchango katika harakati za uchumi kwake. Ni wakati wa kufanya mageuzi ya sheria mbovu hii ambayo haijazingatia vizuri haki za watumiaji wa laini za simu. Tunatakiwa kuzingatia usiri wa Taarifa za Watanzania  #ChangeTanzania Download Now

Read More Download Document

UKATILI WA VIONGOZI WA KISIASA KATIKA JAMII

Hivi karibuni kumekuwa na taarifa kuhusu aliyekuwa Naibu waziri wa Katiba na Sheria kutuhumiwa kunyanyasa mfanyakazi wake kijinsia,  #ChangeTanzania tunalaani tendo hili, Tukio hili la ukatili liliamsha mjadala mkubwa sana  katika mitandao ya kijamii hasa mtandao wa X kuhusu video iliyosambaa ya kijana H.A ( jina la kutunga kuficha utu wake)  akielezea ukatili aliofanyiwa na kundi la vijana wawili kwa maelekezo ya  aliyekuwa Naibu Waziri wa sheria na Mbunge wa Babati Pauline Gekul na waziri huyo ikielezwa alikuwepo wakati tukio lote linafanyika . Kijana  Anadai Gekul aliamuru Vijana hao wamuingizie chupa njia ya haja kubwa kijana H.A au wampige risasi kwa madai kuwa ametumwa kimkakati kwenda kwenye hotel inayomilikiwa na Gekul iitwayo Paleii Lake View Hotel. H.A  alikuwa ni mmoja wa wafanyakazi wa hotel hiyo. Baada kufanyiwa kitendo hicho cha udhalilishaji ndipo Pauline Gekul aliita polisi kuja kuwachukua yeye pamoja na mwenzake na kupelekwa kituoni ambapo walikaa siku nne bila dhamana na msaada wowote wa kiafya. Pia kuna video nyingine ambayo inaonyesha Gekul akimhoji kijana H.A , video hiyo ikiaminika kuchukuliwa na Pauline, Video inaonekana H.A  akiwa uchi bila suruali na kumlazimisha akubali tuhuma zake kama ilivyoonekana katika video hiyo. Video hii inathibitisha kwa kiwango cha juu kwamba kulikuwa na tukio kati ya H.A na Gekul  lakini pia inafanana kwa kiwango kikubwa sana madai anayotoa H.A kufanyiwa na Gekul  Na pia usambazaji wa video hizo katika mitandao ya kijamii kulisaidia kueneza tukio hili la kikatili kwa haraka. Tunashukuru sana waliosambaza walizingatia utu wa kijana huyu kwa kuficha sura yake mwanzo wakati video zimeanza kutoka  Wanasheria, wanaharakati, wanasiasa na Wananchi wa kawaida wapenda haki wamekemea na kulaani vikali tukio hili akiwemo Mwanaharakati Maria Sarungi nae amezitaka mamlaka kuchunguza tuhuma hizo na  kuchukua hatua stahiki juu ya sakata hilo. Alisema kupitia mtandao wa X “ Kijana huyu amedaiwa kulawitiwa na kuteswa na mbunge wa viti maalum mwanamke na naibu waziri! Polisi wanafunika na kijana huyo hana pa kugeukia isipokuwa mitandao ya kijamii Tuhuma hizi nzito zinapaswa kuchunguzwa,  Rais Samia Suluhu - naibu waziri ndiye mteule wako! Ikiwa madai hayo ni ya uwongo ithibitike katika mahakama ya sheria”  Jeshi la polisi limepokea mashtaka hayo na kutoa wito kwa mtuhumiwa kufika kituo cha polisi kwa mahojiano na yupo nje kwa dhamana. Jeshi la polisi   limesema kuwa linafanyia uchunguzi suala hilo. Wengi wamelalamikia utendaji kazi wa jeshi la polisi kuwa linafanya vipi uchunguzi huku mtuhumiwa akiwa hajakamwatwa, au kwa vile tuhuma za kosa hilo zimefanywa na kiongozi mkubwa katika nchi hii? Swali lingime wananchi wanajiuliza mbona viongozi wakikamatwa dhamana huwa ni haki ya kisheria ila ikija kwa wengine ni ngumu sana? Kama H.A  na mwenzake walikaa ndani bila kupewa dhamana kwa nini Pauline Gekul asingekaa ndani kipindi anachunguzwa kwa mashtaka hayo yanayomkabili? Tatizo kubwa hapa ni mfumo mzima wa jeshi la polisi kuwa mbovu na sheria zetu hazina kipengele cha kuwawajibisha polisi endapo watavunja sheria ya kumkalisha zaidi ya masaa 24 mtuhumiwa ndio maana Hashim alikaa kwa takribani siku nne bila kuwepo kwa taratibu yoyote ile kisheria. Viongozi wote wa juu wa jeshi la polisi wapo lakini Gekul anapata wapi nguvu ya kufanya kitendo hicho bila kuogopa madhara yanayotokana na uvunjifu huo wa sheria na haki za Hashim Ally na mwenzake.  Katika usambazaji ya video ya H.A , Bi  Paulina Slaa Narsis amehusika ili kupaza sauti ya H.A  isikike na kupata haki zake, ametoa taarifa za kutishiwa kuuwawa kwa kuchinjwa na kupigwa risasi na Emmanuel Gekul ambaye ni mdogo wa Pauline Gekul, lakini hadi sasa hakuna hatua yoyote imechukulia na jeshi la Polisi. Bila shaka RPC anajua vizuri hili suala. Emmanuel Gekul anasema jeshi la polisi Manyara kwake siyo lolote na haogopi. Je, ni kweli familia ya Gekul imelishika jeshi la polisi Manyara? Hii inaashiria kuwa jeshi la polisi Manyara na Babati, wanakula njama za kutenda uhalifu kwa kushirikiana na familia ya GEKUL, wachukuliwe hatua za kinidhamu na kisheria. Hatutakiwi kuwa na watu katika utumishi wa jeshi la polisi wanaoshirikiana na wahalifu kutenda Uhalifu wa kutisha kwa binadamu wenzao. Hatua ya kwanza ambayo imechukuliwa katika kumuwajibisha Pauline Gekul kwa tuhuma za ukatili na udhalilishaji ni uteuzi wake kutenguliwa na Rais Samia kutoka kuwa Naibu Waziri na kuwa kubaki kuwa mbunge.  Safari hii chama cha Umoja Wa Wanawake Tanzania (UWT) kimetoa tamko na kukemea vikali tukio hili lililofanywa na mwanachama wao na kusema kinafanya uchunguzi juu ya tukio Kumekuwa na historia ya viongozi kama Mawaziri Wakuu wa Wilaya na Mikoa na wengio kufanya ukatili kwa wananchi na kukaliwa kimya bila kuchukuliwa hatua yoyote au hatua ikichukuliwa wanaishia kushinda na kuendelea na maisha yao kama  kawaida. Tunakumbuka tukio la aliyekwa Mkuu wa Mkoa Wa Dsm Paul Makonda alipovamia kituo cha kazi cha habari cha Clouds alibaki huru hata hatua zilipojaribu kuchukuliwa ilishindikana na hakuwajibika kwa Tukio hilo Mfumo wa kuwajibisha viongozi umekuwa mgumu sana kutekelezeka pale ambapo mkuu wa nchi hii hajapenda au kuruhusu taasisi husika kama jeshi la polisi na mahakama kufanya uwajibishaji, hivyo suala la uwajishaji kwa viongozi wakubwa linabaki kuwa la kumpendeza Rais na si wananchi. Hata katika sakata hili la Mbunge Pauline Gekul Rais ana uwezo wa kutotengua katika nafasi yake Na kuviomba vyombo vya uchunguzi kufanya kazi yake, lakini hii haikufanyika hivyo, Pauline bado ni mbunge na mwanachama wa chama cha mapinduzi, na sasa kuna habari kutoka Babati kwamba Pauline Nasra aliyesaidia sana kutoa taarifa za ili tukio anashikiliwa na polisi eti kwa tuhuma za kuomba Rushwa kwa Gekul ili kuzima ili tukio, Pauline Nasra amepitia vitisho vikali wakati wote, lakini yeye ndiye anayeshughulikiwa na jeshi la polisi na sio Gekul anayeripotiwa kufanya tukio, Tunajua tuhuma za rushwa zinataratibu zake, kuna namna ya kuhakikisha TAKUKURU inapata ushahidi, lakini tukio hili eti Polisi wamepewa tu shutuma na Gekul na kumkamata Pauline Nasra na kumuweka ndaniMiongoni mwa matukio mengine aliyofanya Gekul ni kukataa kufanya mahojiano na mwandishi wa habari wa Gadi TV, akimtaka aende ofisini kwake, alipofika ofisi kwa Gekul alikamatwa kwa tuhuma kwamba Naibu huyo wa Waziri wakati huo alikuwa na mashaka na maisha yake, na mwandishi alikamatwa kwa kufika hapo  ofisini, wakati mwandishi huyo alikuwa anakwenda kuchukua taarifa ya upande wa Gekul kuhusu tukio ilo, kwa maana nyingine Gekul alikuwa anakwepa kuongea na vyombo vya habari na polisi wakamsadia kukwepa wajibu huo. Tukio hili linatumbusha wananchi kuwa vita ya kutafuta #KatibaMpya lazima iendelee kwa kasi ili kurekebisha mifumo yote ya haki jinai pia kupunguza madaraka ya Rais ambaye hufanya uwajibishaji atakavyo na si kwa maoni ya wananchi au hata udhibiti wa sheria ndogo ndogo za maadili zilizopo nchini. #ChangeTanzania Download Now

Read More Download Document

NGUVU YA UMMA KATIKA KULETA MABADILIKO.

NGUVU YA UMMA KATIKA KULETA MABADILIKO Nguvu ya umma ni namna ya wananchi wa kawaida hupigania haki zao, uhuru, na usawa kwa njia halali za kisheria bila kutumia njia za hatari. Hii ni haki iliyoainishwa na Katiba yetu ya Tanzania 1977. Wananchi wanapotumia nguvu ya umma wanakuwa na malengo ya kujenga Taifa lenye demokrasia, na kurudisha mamlaka kwa wananchi , Kuna mambo ambayo yanaweza tafsiriwa kama nguvu ya umma, kwa mfano  migomo, kususa, maandamano makubwa na hatua nyingine,  yakiwa na malengo ya mabadiliko makubwa ya kijamii, kisiasa na kiuchumi. Mara nyingi nguvu ya umma  ni mapambano au shinikizo la kudai haki kwa njia ya amani kwa nguvu ya raia,  wananchi huungana kwa sauti moja  kupambania kile wanachoamini ni haki yao na haitekelezwi na watawala, Kuna wakati Nguvu ya umma inaweza tumika kuondoa utawala ulipo madaraka kama wananchi wana hoja ya kuondokana nao, au wamechoshwa na uzembe, ukatili au kupuuzwa na watawala. Tanzania historia ya watu kutumia nguvu ya umma kuleta mabadiliko uzoefu wa mara kwa marai sana kwa kuwa wananchi kila walipoamua kuandamana kudai haki au kupinga mambo yanayofanywa na serikali waliishia kukumbana na fujo za vyombo vya  dola na maandamano hayo kuzuiwa. Mwaka 2018 katia maandamano ya CHADEMA polisi  wakipiga risasi za moto na  kusababisha kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwilini. Mfano mwingine wa hivi karibuni ni maandamano ya kupinga mkataba wa bandari baina ya Tanzania na DP World yaliyondaliwa na kijana wa Bavicha Deusdedith Soka lakini licha ya maandamano hayo kufuata hatua zote za kisheria lakini walizuiwa na jeshi la polisi na waandamanaji  hao wengine kukamatwa na kupelekwa kituo cha polisi.  Ni wazi katiba katika ibara ya 8 inatoa mamlaka kwa wananchi yaani #WenyeNchiWananchi, hivyo wana haki ya kuamua mambo muhimu yanayoendelea katika Taifa hili.ukweli kwa namna serikali yetu inavyoendesha mambo kwa sasa hatuwezi kuikomboa nchi hii bila nguvu kubwa ya umma, nchi nyingi zimefanikiwa kufika sehemu nzuri kwa wananchi kujitambua. Kuacha hofu na woga nyuma na kuchukua hatua, mfano Kenya mwaka 2007 katika kudai #KatibaMpya,  matumizi ya nguvu ya umma yalisaidia sana katika kutokomeza ubaguzi wa rangi Afrika Kusini, Mwaka 2005, Walebanoni kwa kupitia maandamano makubwa ya amani walikataa majeshi ya Syria kuendelea kutawala nchi yao . Hivi karibuni Tanzania imeingia mkataba wenye masharti magumu na hatari kwa rasilimali ya bandari zetu zote nchini. Serikali inaonyesha kuutetea mkataba huu japo ya watu mbalimbali wasomi kwa wasio wasomi kuukosoa mkataba huu kwa kuwa hauna maslahi kwa Taifa letu lakini serikali imeonyesha kutojali maoni ya wananchi ili kufuta mkataba huu baina ya Tanzania na DP World. Kwa kuwa katiba inatoa wajibu kwa wananchi kulinda maliasili na rasilimali, wananchi wameonyesha juhudi hadi za kwenda Mahakamani wakiwakilishwa na Wakili  Boniphace Mwabukisi  na wenzake kuupinga mkataba huu lakini mahakama nayo imeegemea upande wa serikali na kutofanikiwa. Vivyo hivyo hata kuhusu  #katibaMpya,  serikali imekuwa ikizunguka na kuchelewesha mchakato wa kupata #KatibaMpya ambayo itaweka mifumo ya nchi hii sawa na kuwa na mfumo wa utawala wa sheria yenye meno na kudhibiti kikamilifu ubadhirifu wa mali za umma. Wananchi tumejipanga vipi katika kuhakikisha tunatetea maslahi  ya Taifa? Je ni sawa kuendelea kukaa kimya huku rasilimali zetu zikiendelea kupotea? Mahakama pekee iliyobaki kupinga mkataba wa bandari na kupata #KatibaMpya ni mahakama ya wananchi kutumia nguvu ya umma. Wachache wamekuwa wakijitoa kutetea maslahi ya umma lakini wananchi walio wengi wamekuwa wakishindwa kuunga mkono juhudi hizo kwa kuhofia madhara. Umoja wetu ndio utakaotuokoa kwa kuwa maandamano yenye kutumia nguvu ya umma yanaogopesha na hufanya watawala kutii nguvu ya umma inachotaka, kwa sababu hukusanya watu wengi pamoja kupinga uonevu na mateso yenye kuletwa na viongozi kwa kuleta dira mpya ya jamii yenye uhuru na haki zaidi na pengine kwa kutoendelea kuwaunga mkono wale walioidhinisha katiba yenye mifumo isiyofaa au ya zamani. Watu wengi wanapoamua kutounga mkono utawala mbaya, ufanyaji kazi wa mfumo unaanza kuwa mgumu sana. Pale watu wanapoamua kutotii mfumo ni lazima uanguke.. Hata kama serikali ikiamua kupinga  nguvu ya umma kwa sababu wana  silaha na fedha za kutosha, hawawezi  kukabiliana na maandamano yenye idadi ya kutosha kama wananchi wakisimama pamoja kudai haki kwa amani Kama kupinga mkataba wa bandari na kudai #KatibaMpya.   #OkoaBandariZetu #KatibaMpya.   #ChangeTanzania

Read More

KULAANI VIKALI UBAGUZI NA UNYANYASAJI ULIOFANYWA NA JESHI LA POLISI DHIDI YA WANAHARAKATI.

Mtandao wa #WenyeNchiWananchi unaohusisha wananchi mbalimbali wakiwemo wanaharakati inalaani vikali vitendo vya ubaguzi na unyanyasaji vilivyofanywa na jeshi la polisi dhidi ya wanaharakati na wasomi waliofika Mwanza kwa ajili ya Kongamano kuhusu Katiba Mpya na kupinga mkataba mbovu wa DP World wa kuchukua bandari zetu (Kampeni #OkoaBandariZetu)Kwa mujibu wa wajumbe kati ya tarehe 02 hadi 04 Oktoba 2023, wao binafsi na wahusika mbalimbali wakiwemo watoa huduma walinyanyaswa na kuhujumiwa kupitia vitisho vilivyofanywa na Jeshi la Polisi. Baadhi ya matukio makuu muhimu yalikuwa yafuatayo: Download

Read More Download Document

KUKOSEKANA KWA UMEME  NCHINI

KUKOSEKANA KWA UMEME  NCHINI  Tatizo la uhaba wa umeme nchini linaathiri maisha ya watu na shughuli za kiuchumi, serikali ya  imekiri kupungua kwa kasi ya uzalishaji umeme hali inayopelekea kupatikana kwa umeme wa mgao katika maeneo tofauti ya nchi. Rais anasema kutokarabatiwa kwa mitambo ni sababu iliyosababisha kukosekana umeme, ametoa maelekezo kwa mkurugenzi mpya kwenda kupambana na changamoto na zimalizike kwa miezi 6 !! , Swali kubwa la kujiuliza ilikuwa mitambo ya umeme ikakosa ukarabati? Je kuna wanasiasa wowote walihusika? kuna wataalamu wamewajibika na hili tatizo la kutengeneza? Kwa nini wananchi wapata matatizo kwa matatizo ya kutengenezwa? au kutokana na uzembe wa watu? Mapema Mei mwaka huu aliyekuwa Waziri wa Nishati, Januari Makamba, alisema Serikali  ipo katika mikakati kwa kipindi cha  miaka miwili kuhakikisha kuwa tatizo la upatikanaji wa umeme nchini linakuwa historia. Makamba aliyasema hayo kwenye maonyesho ya Wiki ya Nishati, alikiri kwamba  umeme bado ni changamoto na  bado haijawekwa sawa lakini kupitia mpango walio nao litamalizika na kuhusu uzalishaji wa umeme nchini, Makamba amesema umeongezeka kwa asilimia 11 kwa mwaka, ikilinganishwa na mwaka 2022 ambako kulikuwa ongezeko la asilimia 5. Haikupita muda July 2023 Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la umeme nchini (TANESCO) ,Maharage Chande alisema katika kuongeza ufanisi uwajibikaji na utendaji wa kazi Shirika la Umeme nchini TANESCO, wamedhamiria kumaliza changamoto ya umeme ifikapo mwezi June 2024.  https://bit.ly/3ET9qHy Kauli hii inaonekana kuwa kama ghelesha kwa kuwa wanachopitia wananchi sasa hakisadifu maneno ya mkurugenzi huyo wa Tanesco kwa umeme umekuwa ukikatika kwa zamu katika maeneo yote ya nchi kwa muda mrefu hadi kufikia masaa 12. Hivyo Tanesco wanaposema wana mkakati wa kumaliza tatizo la umeme mpaka June 2024 ilitakiwa kuonekana juhudi za  kumaliza Tatizo kwa kuboresha huduma zaidi na si kurudi nyuma kwa hatua kadhaa. Kukatika kwa umeme ni matokeo ya siasa ambazo zimesababisha maamuzi makubwa ya kitaalam yafanyike kisiasa, jinsi tatizo la umeme nchini Tanzania lilivyo kubwa na jinsi ambavyo ahadi zinazotolewa katika kila uchaguzi kuu na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, (CCM) kuhusu tatizo la umeme kuwa historia zilivyokuwa na siasa au tatizo la umeme kutumika kukidhi malengo ya kisiasa. Kwa miaka mingi sasa Tanzania imekuwa na tatizo sugu la siasa kuathiri mfumo wa umeme ambalo linaturudisha nyuma kila kukicha . Tangu wawekezaji binasfi waliporuhusiwa kuzalisha umeme mwanzoni mwa miaka ya 1990. Baadhi ya kampuni za wazalishaji binafsi wa umeme (Independent Power Producers) zilizoingia Tanzania zilikuwa ni IPTL, Richmond na Dowans. Wengi wa wazalishaji hawa huru walihusishwa na siasa za chama tawala, CCM. Lakini kuja kwao kuligubikwa na tuhuma za rushwa zilizosababisha kujiuzulu kwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa mwanzoni mwa 2008. Hata hivyo Lowassa akizungumza Bungeni kabla ya kujiuzulu, alilalamika kuwa alionewa kwa kutuhumiwa na kuhukumiwa bila kusikilizwa, hivyo alijiuzulu ma maslahi ya chama chake na serikali.https://bbc.in/3ESoe9h Tanzania imebarikiwa kila aina ya chanzo cha kuzalisha  umeme kwa maji, jotoardhi, na hata kwa upepo. Mradi wa kuzalisha umeme kwa nguvu ya upepo mkoani Singida haukuwahi kuanza. Pia nchi nzima ina fursa ya kuzalisha umeme kwa jua, uwezo wa kuzalisha umeme kwa gesi pia upo wa hali ya juu  kwa zaidi ya futi za ujazo trilioni 60. Upatikanaji wa madini ya urani nao pia unaipa Tanzania nafasi ya kuzalisha umeme wa nyuklia kama serikali ikitaka. Tafiti zilizothibitishwa zinaonesha kuwa kuna madini ya urani katika mikoa ya Ruvuma, Dodoma, Singida, Manyara na Arusha japo hayajaanza kuchumbwa. Kwa kifupi Tanzania haitakiwi kuwa na matatizo ya umeme. Inatakiwa iuze umeme nchi za nje. Lakini rasilimali kama hizi huwa haziwezi kuifaidisha nchi kama siasa zake hazikidhi mahitaji na kuleta tija kwa manufaa ya watu wake.  Hivi karibuni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa September 20, 2023 amefungua Kongamano la Tano na Maonesho ya Nishati Tanzania na amesema kwamba Serikali imedhamiria kuwa Mzalishaji mkubwa wa nishati na kuwa na umeme wa kutosha utakaopatikana kwa urahisi na nafuu na ziada itauzwa nje ya Nchi. amesema serikali inaendelea na utafutaji wa gesi, tunataka tuwe Wazalishaji wakubwa wa nishati, tuwe na umeme wa kutosha utakaopatikana kwa urahisi na nafuu na ziada tutauza nje ya Nchi. Kwa kauli kama hizo inaonyesha kuwa serikali imekuwa ikifanya mambo tofauti na kuongea tofauti. Hali ya umeme imezidi kuwa tete nchini na kusababisha hasara kwa wananchi na hasa sekta ya kiuchumi, lakini Waziri Mkuu anasema kuwa tutuaza umeme nje. Nchi hii imekuwa na miradi mingi ambayo inaendelea nchini ambayo inahitaji na itahitaji umeme wa kutosha ili kuleta ufanisi katika utendaji wake. Mfano treni ya umeme na mingineyo.  Kwa hali hii ya kusuasua kwa umeme je tutafanikiwa kuibadili Tanzania na kuwa moja kati ya nchi zilizoendelea?  Kila mara zimekuwa ni sababu za kimazingira ambazo zinazochangia uzalishaji wa umeme kushuka, Je serikali yetu imekosa kabisa ubunifu wa namna ya kupata umeme licha ya kuwa na vyanzo tofauti tofauti vya kuzalisha umeme? Ingekuwa ni vyema Serikali ikawajibika kwa maslahi mapana ya wananchi kwa kuzingatia wakati uliopo na vizazi vijavyo. Nishati ni chanzo muhimu cha kuleta msisimko wa uchumi.  Nchi yetu imebarikiwa vyanzo vingi vya kuzalisha umeme lakini ifike mahali vinufaishe Watanzania na hata mataifa jirani. Ili kufanikisha hayo tunatakiwa kupata katiba bora ambayo itakuwa na meno kwenye suala zima la uwajibikaji na wananchi kuwa na mamlaka, wasiporidhishwa na utendaji wa kiongozi huyo wawe na mamlaka ya kumtoa kwenye uongozi. Kwa kufanya hivyo tutapata uwajibikaji katika sekta zote na kuwa na Taifa bora. #KatibaMpya ni sasa. #Change Tanzania Download Now

Read More Download Document

CRIMINAL APPEAL CASE NO 87 OF 2023, PETER MICHAEL MADELEKA VERSUS THE REPUBLIC OF TANZANIA.

On the trial between The Appellant, Peter Michael Madeleka vs The Republic, the appellant was wa challenging the previous judgment on the two grounds That, the Honourable Court's (sic) erred in law and fact in holding that consequent to the nullification o f plea bargain agreement the parties are reverted to the old charge before amendment that containing (sic) non bailable offenses; and That, the Honourable trial magistrate erred both in law and fact by denying the Appellant bail on the basis o f non-existing charge.  The appellant has been released on bail by signing a bond of shillings One Million only (TZS 1,000,000/=); . The Appellant shall have one surety bearing a proper identification from a reputable Institution. The surety to sign a bond of shillings One Million only (TZS 1,000,000/=) Download Now

Read More Download Document

Tamko la Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kuhusu mkataba wa uboreshaji wa bandari za bahari na maziwa Tanzania.

Tamko la Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kuhusu mkataba kati ya Jmuhuri ya Muungano wa Tanzania na Emirate of Dubai juu ya ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa maendeleo ya uboreshaji wa bandari za bahari na maziwa Tanzania. Download Now

Read More Download Document

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. MWIGULU LAMECK NCHEMBA MADELU (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2023/24.

Makadirio ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2023/24 yameandaliwa kwa kuzingatia nyaraka na miongozo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ikiwemo: Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/22 - 2025/26) ambao umezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025; Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020; Dira ya Maendeleo ya Afrika Mashariki 2050; Ajenda ya Maendeleo ya Afrika 2063; Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030; Mwongozo wa Ushirikiano wa Maendeleo Endelevu wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2022 - 2027; makubaliano mengine ya kikanda na kimataifa ambayo Tanzania imeridhia. #ChangeTanzania Download Now

Read More Download Document

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. MWIGULU LAMECK NCHEMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA MWAKA 2023/2024

Mh Waziri Mwigulu Lameck Nchemba aliwasilisha Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2022/23 pamoja na Mwenendo wa Utekelezaji wa Vipaumbele vya Wizara Kukusanya, kutafuta na kudhibiti mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka unaofuata 2023/2024. Pia  Kufanya tathmini ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na maandalizi ya Dira 2050.  #ChangeTanzania Download Document

Read More Download Document

TIBAIJUKA : URAIA PACHA..CHANZO CHAKE , .. TANZANIA TUNAKOSEA KUVUA WATOTO WETU URAIA.

Anaandika Prof. Anna Tibaijuka, aliyekuwa Waziri TIBAIJUKA : URAIA PACHA..CHANZO CHAKE : Wakati tunapata uhuru wageni walikuwa na nguvu sana kiuchumi kisiasa na kitaalamu. Wengine wallimiliki Ardhi kubwa… settlers. Wengina viwanda vikubwa hasa waasia huku wakiwa na uraia wa Waingereza. Ikaonekana wakipewa uraia huku waAfrika wakiwa bado wanapambana na "umaskini maradhi na ujinga" wanaweza wasije ambulia chochote kiuchumi. Watakuta ardhi na rasilimali nyingi zimehodhiwa na waTanzania wakuasili wenye uraia pacha. Ikaamuliwa kuupiga marufuku. Wageni wasifukuzwe lakini wachague kati ya Tanzania na huko walikotoka. Mapinduzi Zanzibar nayo yakaongezea chachu…. raia walioikimbilia nje wakiwa na uraia pacha wangeliweza kusumbua. Mwalimu Barbro Johanson ni kati ya Wazungu wa TANU walioungana na Mwalimu Nyerere kupigania uhuru yeye akiwa Mbunge wa Kwanza wa Kanda ya Ziwa Magharibi…. yaani Mwanza katika legislative council ambapo kila chama kilitakiwa kuwa na Mwafrika mmoja… Mzungu mmoja na Muhindi mmoja. Mama Barbro alinieleza kuwa yeye ndiye alipendekeza sera hiyo kwa mwalimu na ikakubaliwa. Sasa mwaka 1993 aliporejea Sweden akiwa raia wa Tanzania aliomba lakini alinyimwa resident permit ya kuishi Sweden na idara ya uhamiaji kwa sababu aliambiwa Sweden haitambui uraia pacha kwa raia wake. Ukizaliwa raia wa Sweden na ukirudi Sweden automatically wewe ni mswidi umerudi nyumbani. Hayo ya uraia pacha ni adventure zako duniani kulingana na hali yako. Mama Barbro alifadhaika sana juu ya jambo hili. Alikuwa mzee wa miaka 86. Akamwambia Balozi (wakati huo mme wangu Hayati Wilson Tibaijuka) kwamba atakuja fanya kituko cha ajabu kwa sababu amenyanyaswa na hawezi kusaliti nchi yake Tanzania. Tukahofia kwa utu uzima huo anaweza hata kujinyonga au kukataa kula. Wakati huo Mama Barbro asingeweza kurudi Tanzania kwa sababu Mwalimu Nyerere alishamuomba asirudi huku Tanzania kwani utaratibu mzuri wa kumtunza haukuwepo. Nilikuwa ninahangaika naye peke yangu nikiwa mwalimu UDSM. Balozi Tibaijuka alimaliza swala hilo la resident permit ya Mama Barbro kidiplomasia. Wizara ya nchi za nje ya Sweden ikamugongea Mama Barbro 'resident permit" kwenye passport yake ya Tanzania kama alivyotaka lakini kihalisia ilikuwa ni kumtuliza tu. Kwa kifupi kisheria Mama Barbro na wenzake wengi waliojaribu kukana uraia wao hawakufanikiwa. Nchi zao hazikukubali. Sisi tumevuka mpaka hadi kuwanyanyasa watoto wetu kwa kuwaondolea uraia wao. NOT RIGHT AT ALL Kwa sasa tumeelimika. Sababu za miaka 60 kuzuia uraia pacha hazipo tena hasa kwa watoto wanaozaliwa wakiwa raia wa nchi hii. Kumbuka kundi hili kimsingi hawakuwepo miaka hiyo.Tujielimishe. Mama Tibaijuka ChangeTanzania #WenyeNchiWananchi

Read More

Maasai Delegation to Meet European Leaders in a Bid to End THE FORCED Evictions and Human Rights Abuses THEY ARE FACING in Tanzania.

The Maasai have lived for generations in the Serengeti ecosystem in Tanzania and have shaped and protected these lands, preserving wildlife and biodiversity in areas such as Loliondo, the Ngorongoro Conservation Area and the now Serengeti National Park. However, they have been systematically marginalised and violently evicted from their ancestral lands to make way for conservation projects, tourism, and trophy-hunting schemes, severely violating their human and constitutional rights. This has also happened with the support of conservation NGOs like the Frankfurt Zoological Society (FZS) and European funding.22.05.2023, A high-profile delegation of Maasai representatives starts a tour in several European countries this May, seeking international support to halt the ongoing forced evictions and human rights abuses against the Maasai people in Tanzania. Read more

Read More Download Document

Walionipiga risasi wako wapi? Amepatanisha nini wakati maridhiano yana giza kali – Lissu.

“Mara ya mwisho nilipokuja kufanya mkutano ilikuwa ni mwezi Julai mwaka 2011 tena nilikuja na katibu wetu Dk Slaa , ile siku tuliyofanya mkutano hapa kijana anayeitwa Ally Zona aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi wakati wakituzuia tusifanye mkutano hapa (miaka 12 imepita tangu siku hiyo). Nilipokuja kipindi kile hawakuwa wananiita Chiba ila leo wananiita Chiba kwa sababu ya mambo mabaya yaliyofanyika katika nchi hii, Kuna watu wengi waliouawa toka tumefanya mkutano tangu Ally Zona  alipouawa hapa ni wengi hawana idadi. Wengine wamepotea wamechukuliwa katika famila zao na nyumba zao hatujui walipo hadi leo.Nchi imejaa mabango kila mahali kuwa ameunganisha nchi, ameondoa uhasama swali;  Je hawa waliouwawa wameuwawa na nani?  Waliomteka Ben Saananae mpaka leo hatujui alipo ni akina nani?  Tumeunganishwaje wakati hatuambiwi watu waliouwawa wameuawa na akina nani waliomuua yule mwanafunzi Akwilina siku ile viongozi wetu wamekamatwa, alipigwa risasi mchana kweupe, je hao ndugu zake wamepatanishwa lini?   Je mjane wa Alphonce Mawazo aliyekatwa mapanga saa tisa za mchana amepatanishwa lini?   Watu zaidi ya 400 wameuwa Kibiti, Rufiji na Kuna mtu alikuwa na kiwanda cha madawa hapa Dar Es Salaam amekamatwa kiwandani kwake mchana kweupe na hajaonekana mpaka leo. Na walionifanya mimi leo  naitwa Chiba ni akina nani na mimi nimepatanishwa lini?Sasa haya mabango ni ya nini? Nimeona nimewekwa kwenye mabango Dar Es Salaam nani aliyewaambiwa mniweke mimi kwenye mabango kwamba nimepatanishwa?  Mwenyekiti wetu Freeman Mbowe alikuwa Gaidi mwaka jana tu eti leo amepatanishwa, sasa kuna upatanisho au kuna kusanifiana tu? Tunapatanishwa au tunapangwa tu ili tukubali kufunika makombe maharamia yapite? Hakuna dhambi mbaya katika nchi iliyopitishwa kama tulikopitishwa sisi, tusidanganyane. Askari polisi waliostaafu 2020 hawajalipwa stahiki zao za kustaafu na nauli za kurudi makwao mpaka leo. Na sio polisi tu ni kila mfanyakazi wa nchi hii.Kuna mahali panaitwa Kiegea hapa Morogoro wananchi wananyang’anya ardhi zao na mkuu wa mkoa anaongoza polisi kwenda kunyang’anya watu mashamba yao. Maelfu ya watu kule Mbarali Mbeya wananyang’anywa mashamba yao vijiji karibu 20 na zaidi, wanapelekewa jeshi na nyumba zinachomwa moto, ukihofu unawekwa ndani na polisi. Wananchi wanaumizwa na serikali yao ukiuliza kwa nini badala upewe majibu wanakazana kupamba mabango ya upatanishi nchi nzima. Watu wanatekwa na hivi karibuni nimepewa taarifa kuwa watu wanaoishi Dar Es Salaam kule Mabwepande upande wa Wazo wanaambiwa waondoke lile eneo ni la DDC (Dar Es Salaam Development Cooperation) wakati ilianzishwa mwaka 1971 na kufungwa mwaka 1974, sasa hivi watu wanapelekewa Jeshi na Amos Makala ( mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam) kuwa wahame. Tukija Ngorongoro peke yake takwimu zinasema watu elfu na ishirini waondolewe kwa nguvu wapelekwe mahali panaitwa Msomera,  Handeni  Tanga . Serikali ilipewa pesa shilingi bilioni 35 ya kuhamishwa Maasai kuwapeleka Msomera na ikaliwa, waliokula pesa wanajulikana ila ukihoji unaambiwa nani kama mama. Mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu nchini Tanzania katika ripoti yake mwaka huu ukijumlisha wizi na uchafu wote uliofanyika tunapata jumla ya zaidi ya Trilini  mbili za kitanzania. Ukipita msamvu hapo kuna bango la TRA lina picha ya mama linasema lipeni kodi ili tujenge nchi pamoja, sasa najiuliza nilipe kodi ili tujenge nchi au  nilipe kodi ili walaji wale?  Hii nchi inaupigaji mkubwa, wanaposema kazi iendelee wanataka kazi ipi iendelee? Maana ufisadi wa mwaka huu ni mkubwa kuliko ufisadi wa mwaka  jana na ufisadi  wa mwaka jana ni mkubwa kuliko ufisadi wa mwaka juzi. Kila mwaka ufisadi unazidi na unafanywa na watu wale wale ambao wanatuambia kazi iendelee. Sasa kampeni ya uchaguzi wa mwaka 2025 zimeanza na zimeanza kwa katiba hii hii tuliyonayo ina maana hawataki kubadilisha katiba. Sisi tunataka #KatibaMpya  ili twende katika uchaguzi ujao tukiwa na #KatibaMpya , Tume mpya huru ya uchaguzi , sheria mpya za uchaguzi na majimbo mapya ya uchaguzi. Mfumo wetu wa uchaguzi ni uchafu mtupu ambao lengo lake ni kuhakikisha CCM inabaki madarakani Tumepeleka mapendekezo ya maridhiano na tumenza mazungumzo toka mwaka jana mwezi Mei , sasa ni Mwaka umepita  , Lakini mapendekezo tuliyopeleka  kitu gani kifanyike? Na tumeweka wazi kabisa kwamba nini kifanyike na nani afanye nini? Na kifanyike vipi ili tupate #KatibaMpya , lakini   Tangu tunepeleka mapendekezo hatujajibiwa hata moja mwaka ujao ni uchaguzi wa serikali za mitaa na vijiji , unafikiri tutakwenda kugombea kwa sheria ipi kama sio ile enguaengua ya mwaka 2009? Na tukienda kwa sheria hiyo tutegemee nini? Mpaka sasa hakuna mwenye matokeo ya urais ya Magufuli na Samia Hasssan 2020 hayapo , hivyo hakuna Rais aliyechaguliwa ni ametangazwa tu kwa sababu kura zinatakiwa kuwepo katika gazeti la serikali lakini mpaka leo hakuna, Na katika uchaguzi ule wa 2020 Morogoro ndio iliyoongoza kwa wabunge waliopita bila kupingwa.  Kuna jimbo linaitwa Misungwi lina kata 27 tuliweka mbunge na madiwani kataka kata hizo lakini wote walienguliwa na CCM ikapita bila kupingwa. Hivyo ninaPozungumzia suala la kupata katiba mpya ni ili haya yasijirudie.Matatizo yote tunayopitia mfano suala la uporaji wa ardhi, maisha magumu, kuporomoka kwa viwanda ni kwa sababu ya walioko madarakani na chama chao. Viongozi waliopo madarakani wanapenda sana kumsema Magufuli kwa sababu amekufa , lakini ukweli ni kwamba wote ni washiriki wa hii dhambi ( matatizo yanayoendelea kuwapa wananchi nchini) dhidi ya watanzania  Kwa mujibu wa katiba ya sasa na sheria zote za nchi hii Rais wa sasa ni MUNGU mtu kwa sababu Rais akiamua jambo lolote hata liwe baya  linatekelezwa. Mfano akimua wananchi wachukuliwe fedha zao zilizotengwa na Bunge zinachukuliwa na zimechukuliwa.  Ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa Serikali kabla haijapelekwa bungeni anakabidhiwa Rais kwanza halafu ndio anaagiza ipelekwe bungeni hivyo anayejua wizi uliogunduliwa na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa serikali ni Rais , je mpaka leo amechukua hatua yoyote? Jibu ni Hapana na marais wote waliopita hawajawahi kuchukua hatua yoyote katika hili , hivyo ninapozungumza katiba mpya nataka mtu mmoja asipewe nguvu ya kufanya maamuzi ambayo yanaweza kutuumiza kama ambavyo tunaumizwa . Tunataka tupate katiba ambayo kama tunamtaka mkuu wa mkoa au wa wilaya tuwachague wenyewe na wakishindwa kutekeleza majukumu tuwaondoe wenyewe. Kama kweli kuna maridhiano mchakato wa katiba mpya uko wapi? Utaratibu wa kupata katiba mpya mwaka ujao kama tulivyopendekeza uko wapi?  Tuwe na kauli moja kuwa tusipokuwa na katiba mpya kabla ya uchaguzi ujao hapatakalika, tusidanganyane.  Ujumbe wangu ni kuwa tudai katiba mpya na mfumo mpya wa uchaguzi, mfumo mpya wa Haki zetu kabla ya uchaguzi mkuu ujao. Tukienda katika uchaguzi mkuu ujao kwa katiba hii hii iliyopo yatatokea ya 2019 na ya 2020, anayetuambia kuwa wamebadilika kwani Magufuli aliyafanya yote peke yake ? aliosaidiana nao ni akina nani na wako wapi? Hivyo tusikubali maneno ya upatanisho wakati hakuna chochote unachokiandaa kutupatia katiba mpya”. —   Tundu Lissu  #KatibaMpya #ChangeTanzania   https://www.youtube.com/watch?v=9xAXFCcQBqA

Read More Download Document

Rasimu ya mitaala ya Elimu ya awali, msingi, sekondari na ualimu.

SERIKALI imeamua kutoa rasimu ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023 na rasimu ya Mitaala Mipya ya Elimu ya Awali, Msingi,Sekondari na Vyuo vya Ualimu hadharani ili kupata maoni ya wananchi. Read More

Read More Download Document

Mapendekezo ya mabadiliko kwa mfumo wa Elimu.

Serikali imekusudia kuleta mapinduzi ya kijamii na kiuchumi ili kuibadili Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Sekta ya elimu na mafunzo, kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025 na Mpango wa muda mrefu wa Maendeleo ya Taifa 2011/12 hadi 2024/25, inatarajiwa kuleta maendeleo ya rasilimaliwatu kwa kutayarisha Watanzania mahiri walioelimika na wapendao daima kujielimisha ili kuliletea Taifa maendeleo na kuliweka kwenye uchumi shindani. Ili kufikia lengo hilo, mfumo wa elimu na mafunzo unaotumika nchini lazima utoe fursa za kutosha kwa watu wengi zaidi kuelimika na kuendelea kujielimisha. Kadhalika, mfumo huu unawajibika kutoa elimu na mafunzo yenye ubora unaokubalika na kutambulika kitaifa, kikanda na kimataifa. Katika kufanikisha hili, Serikali imekuwa ikitekeleza mipango na programu mbalimbali za elimu na mafunzo. Hata hivyo, katika kipindi cha utekelezaji wa Sera cha 2015-2022, changamoto mbalimbali zimekuwa zikichangia katika kushuka kwa ubora wa elimu na mafunzo nchini. Changamoto hizo ni pamoja na udhaifu katika mfumo na muundo wa elimu na mafunzo; uhaba wa walimu; uhaba wa zana, nyenzo, vifaa na miundombinu ya kufundishia na kujifunzia; na mapungufu katika ithibati na uthibiti wa ubora wa shule na vyuo. Toleo la Sera la mwaka 2023 linabainisha masuala ambayo Serikali, kwa kushirikiana na wadau katika elimu na mafunzo, itayawekea mkazo zaidi ili kuweka mazingira mazuri ya kufikia malengo ya mipango ya maendeleo. Masuala haya ni pamoja na kuinua ubora wa mfumo wa elimu na mafunzo ili uwe na tija na ufanisi, kutoa fursa za elimu na mafunzo kwa usawa na kuendelea kuinua ubora wa mitaala ya elimu na mafunzo kukidhi mahitaji ya maendeleo ya Taifa. Aidha, Serikali itaendeleza matumizi ya lugha za Kiswahili, Kiingereza na Alama, pamoja na lugha nyingine za kigeni katika elimu na mafunzo. Vilevile, itaendelea kuinua ubora wa mfumo wa upimaji, tathmini na utoaji vyeti katika ngazi zote, ikiwa pamoja na utoaji wa ithibati za ujuzi katika ngazi mbalimbali. Serikali itaimarisha uwezo wa uongozi na utawala katika sekta ya elimu na mafunzo na kupanua wigo wa ugharimiaji wa elimu na mafunzo. Dira ya elimu na mafunzo nchini ni “Kuwa na Mtanzania aliyeelimika na mwenye umahiri ikiwemo maarifa, stadi, uwezo na mtazamo chanya utakaomwezesha kuchangia katika kuleta maendeleo ya Taifa”. Vilevile, Dhima ya Sera ni “Kuinua ubora wa elimu na mafunzo kwa kuweka mifumo na taratibu zitakazowezesha kupata idadi kubwa ya Watanzania walioelimika na wanaopenda kujielimisha zaidi ili waweze kuchangia katika kufikia malengo ya maendeleo ya taifa”. Ili kufanikisha utekelezaji wa Sera hii kwa ukamilifu, kunahitajika ushiriki wa wadau wote wa elimu na mafunzo katika ngazi zote, zikiwemo sekta binafsi, Asasi za Kiraia na washirika wengine wa maendeleo. Napenda kuwashukuru wale wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika mchakato mzima wa kukamilisha toleo hili la pili la Sera ya Elimu na Mafunzo.

Read More Download Document

Barua ya Umoja wa Mataifa kuhusu Ukatili wakati wa  kuhamishwa kwa Maasai Ngorongoro.

Kamati ya Kutokomeza Ubaguzi  iliandika barua 28 Aprili, 2023 ya Umoja wa Mataifa Wa Haki Za Binadamu umeujulisha Umoja wa mataifa kuwa Kamati ilizingatia habari ilizilizopokelewa juu  ya onyo lake kuhusu  utaratibu wa hatua za dharura, unaohusiana na hali ya Maasai na wazawa katika maeneo ya Ngorongoro na Loliondo nchini Tanzania.  Kulingana na maelezo yaliyopokelewa ni kwamba Jamii za Maasai imeendelea kunyanyasika kutokana na kutolewa katika maeneo yao ambao ni mpango ya Serikali ya kupanua utalii i na maeneo ya hifadhi uwindaji wa wanyama pori  kaskazini mwa Tanzania ambao unasababisha kulazimishwa Uhamisho wa Wamasai wapatao 150,000 kutoka katika ardhi zao za jadi katika Hifadhi ya Ngorongoro (NCA) na Loliondo. Mpango huo wa serikali ya Tanzania umefanyika bila kuhusisha maoni  ya wakazi husika yaani Maasai na kupanga namna watakavyokubaliana juu ya eneo lao hilo ambalo linachukuliwa na serikali licha ya kuwa sheria bado zinawalinda Maasai hao. Kitendo hicho kimepelekea uvunjifu wa amani, kuondolewa kwa Maasai katika maeneo yao na mamlaka za Polisi wa eneo la Ngorongoro   kwa nguvu, kupewa vitisho, kuwekwa kizuizini kiholela na kutendewa kinyama wanapoandamana kulinda ardhi zao za kimila dhidi ya vitendo hivyo katika maeneo ya Ngorongoro na Loliondo. Maasai pia wamekuwa ni waathirika wa kubaguliwa kwa matamshi ya kibaguzi kimuonekano , ikiwa ni pamoja na kijamii, vyombo vya habari, watendaji wasio wa Serikali, baadhi ya mamlaka za umma za Serikali na chama tawala. Kwa kuzingatia hayo hapo juu, Kamati inaomba upande wa mkoa  kusitisha mara moja mipango ya kuhamishwa na kufukuzwa kwa nguvu kwa jamii za Kimasai kutoka kwa jadi zao ardhi Loliondo na Hifadhi ya Ngorongoro, na kusisitiza  nia ya Kamati ya kuendelea kushiriki katika mazungumzo yenye kujenga na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa nia ya kuhakikisha utekelezaji wa Mkataba huo unatekelezwa kwa ufanisi kwa maslahi mapana ya jamii ya Maasai. #ChangeTanzania #WenyeNchiWananchi

Read More Download Document

Open Letter to Vice President of the United States of America Kamala Harris

March 20, 2023Dear Vice President Kamala Harris, Please receive warm greetings from the Maasai of northern Tanzania. As you plan your visit to Tanzania later this month, we would like to share with you two major issues that are causing irreparable harm to our community. Firstly, the demarcation of a new protected area in Loliondo that is permanently taking critical land from the Maasai people to protect foreign trophy hunting, and secondly, the involuntary relocation of Maasai people from the Ngorongoro Conservation Area (NCA). Together these two efforts will force most of the Maasai from this region to abandon their way of life. An estimated 70,000 people have been evicted from 14 villages within Loliondo and another 10,000 people have left Ngorongoro. 90,000 Maasai inNgorongoro are without access to basic services such as healthcare. Some 600,000 livestock have been killed by drought due to restricted access to water and grazing and ten thousand others have been auctioned by the Tanzania government.Although some government officials and some conservation organizations say that this action is necessary, most researchers agree that there is no ecological, economic or political justification for these actions. This crisis was created by government agencies and not local communities. It is well documented that the Maasai people from this region are one of the most sustainable and resilient communities in all of Africa.We request your assistance in advocating for a sustainable and equitable solution that meets the reasonable needs of the hundreds of thousands pastoralists of the region, whose livelihoods rely on access to grazing lands and water. This letter provides background information and possible actions the US government can take to address this important issue. We respectfully request you to intervene in this matter of great concern to the indigenous Maasai peoples of Loliondo before we are all displaced and become refugees.(1) Evicting Maasai for a New Hunting Reserve in LoliondoThere has been an ongoing struggle between indigenous Maasai people of Tanzania and the Tanzanian Government since 1992. It revolves around repeated attempts by the Government to take Maasai village land and designate it as a game reserve for trophy hunting. The Royal Family from Dubai through a lease to the Otterlo BusinessCorporation has had exclusive rights to hunt in this area since 1992. Critically, the disputed land is prime grazing land during the dry season, the main source of water and saltlicks for livestock, and contains many pastoralists ritual sites.Having already given up our rightful claim to land in order to establish the Serengeti.National Park in 1959, we reasonably expected that the government would abide by the agreement to defend our customary land use rights. On each of three occasions, in 2009, 2017 and 2022, Maasai people have been forcibly evicted from land previously.legally accessible to them for grazing cattle and building their rudimentary homes (bomas) and civic infrastructure, such as primary schools, clinics, and dispensaries. On May 25, 2022, the community submitted to the Prime Minister a report and request for dialogue after suggestions of new evictions from ancestral Maasai land, previously registered to pastoralist villages. On June 7, 2022, a paramilitary group of around 700 people, mostly police, park rangers, military and other Government funded armed security forces arrived at Loliondo, instigating social unrest and public panic. This operation ended with over one hundred Maasai arrested with trumped-up charges that have subsequently been dismissed by local Courts. Many others were wounded by live bullets fired against civilians by paramilitaries deployed by the Tanzania government.Despite all attempts to stop the process, by the end of June 2022, the Tanzanian state forcefully and against the will of the community re-demarcated 1,500 km2 of ancestral land, prohibiting use by Maasai people and their cattle, with harsh punishments, including beatings, jail, and cattle seizure, for those that disobeyed. Over 400 military rangers from a special unit remain in Loliondo, confiscating cattle daily and cracking down on activists and human rights defenders. (2) Evicting Maasai People from the Ngorongoro Conservation AreaThe Ngorongoro Conservation Area (NCA) is a multiple land use Area covering 8,392 square kilometers, with 98,000 Maasai pastoralists. Both the community of NCA and Loliondo were evicted from the Serengeti by the British colonial government in 1959. Subsequently, they were assured of continued occupation and that they would not be moved again out of the NCA which was part of their vast land in the Serengeti-Ngorongoro-Mara ecosystem. In the past five years some government agencies and officials have suggested without evidence that the Maasai population should be moved out of Ngorongoro because of population growth. In 2022 the government began a strategy they call “voluntary” relocation. There is no scientific evidence to support these claims.Since then, the government has undertaken many actions that impede pastoralism and most negatively impact women and youth. The Tanzanian Government has:1) Stopped providing funding to support essential services like health dispensaries and schools. Suspended operation of the Makao Mapya dispensary and removed doctors from Endulen, dramatically reducing essential public health services in what was the only hospital with capacity to admit patients.2) Evicted 3450 people from their homes. Closed four nursery schools, nine permanent water sources, including nine dams, and six health mobile clinics.3) Provided poisoned saltlicks to Maasai pastoralists resulting in the deaths of an estimated 10,365 cows, 9,541 goats, 16,574 sheep, and 394 donkeys.4) Implemented a policy resulting in the daily starvation of livestock from 28 villages.The government levies fine equivalent to US$ 45 for each cow. This significant penalty has led to hunger, especially for women and children, a sharp decline of the number of children attending school, significant rural to urban migration, and environmental destruction as communities turn to cut trees to feed their livestock.5) Continued to support existing military efforts to intimidate political and traditional leaders from speaking out against human rights violations.6) Violated the rights of Maasai indigenous peoples to free, prior, and informed consent. We were not consulted, nor did we consent to the on-going police evictions or acquisition of our grazing lands to create a hunting reserve.7) Reallocated funds previously sought and obtained to other districts as an effort to dismantle service provision in Ngorongoro.8) Suspended operation of Flying Medical Service, a charitable organization which has been providing highly needed health care to communities throughout Maasailand from the 1960’s to 2022 when they were grounded as part of the same effort to paralyze lifesaving services, such as vaccines in Ngorongoro District. What You Can Do to HelpVice President Harris, Maasai women and children are the most affected in this conflict. We know the American people to be sympathetic to global injustice and that you personally have expressed empathy and commitment to gender equity in education and other civic spaces, to respecting the rights of indigenous peoples, lifting up the voices of marginalized women and youth and taking action on behalf of the disaffected.Given the prevailing situation we request that you encourage the Tanzanian government to: Observe national and international law, especially regarding human rights that recognize our rights to own and protect our lands. The government should respect international instruments, obligations, and good governance principles, especially to respect pastoralism as a viable way of life. Immediately stop the ongoing seizure, auction, and forfeitures of Maasai livestock and to restore Maasai grazing rights. Halt the plan to take further Maasai areas to expand protected areas in Tanzania that has significantly impacted the Maasai community more than the rest of over hundred tribes joined together. The government should instead provide essential services to NCA residents and immediately restore grazing rights to pastoralist in Ngorongoro and Loliondo. Establish a commission or inquiry, supported by the US Government, to examine disputed lands, displaced people and to assist in the restoration of peace and compensation for rights infringements and losses by starting meaningful dialogue between the Tanzanian Government and Maasai pastoralists; and Immediately cease the military special task force stationed in Loliondo that.intimidates and harasses anyone advocating for basic rights and seeking justice.We write this letter in confidence and hope that you will act swiftly to help us neutralize the violent situation and restore land to the indigenous Maasai peoples of Loliondo and Ngorongoro.

Read More Download Document

Miaka Miwili Bila Magufuli, Miaka Miwili na Samia 20 MARCH 2023.

Miaka miwili bila Magufuli Imetimia miaka miwili tangu kifo cha Rais wa Awamu ya Tano John Pombe Magufuli. Kuna mengi sana yanazungumzwa na Watanzania wengi wanakumbuka awamu ya tano kutokana na mfumo wake wa utawala au namna walivyoendesha nchi, awamu ya tano ilitambulika kama awamu ya maamuzi bila kujali sheria au kwa kutunga sheria mpya ili kuzifuata hizo sheria ambazo nyingi zililalamikiwa na watu, awamu ya tano kwa kifupi ni aina ya utawala ambao ulikuwa na mikakati ya kuwa na sheria ambazo walizijenga kwa misingi ya kujipambanua kama utawala wa sheria, lakini sheria nynigi zilikuwa na utawala mkubwa na ziliumiza watu,Awamu ya Tano ilitunga sheria nyingi kwa wakati mmoja baada ya kupata changamoto kutoka kwa wadau mbalimbali kwa kusema ulikuwa utawala wa kidikteta, ili kujinasua na hali hiyo walitumia mbinu ya kutunga sheria zinazoendana na kila wanachotaka kufanya, sheria nyingi lizikuwa zinalenga watu, taasisi au mfumo au biashara au kundi la watu, malengo ya kuwa na hizo sheria ni kama tulivyoeleza ilikuwa ni kujenga utawala wa sheria yaani utawala unaofuata sheria lakini sheria za namna gani basi ni hizo walizotengeneza wao kwa malengo maalumu.  Moja ya sheria iliyobadilisha ilikuwa ni sheria ya kampuni na NGOs na hapa walikuwa wakilenga NGOs na mashirika binafsi ambayo yalikuwa akifanya kazi ya uraghbishi, sheria ilizuia makampuni yaliyokuwa yakifanya uraghbishi nchini na kuyalazimsha yote kuwa NGOs, na sheria ya NGOs ilibadilishwa ili kumpa msajili wa NGOs nguvu kubwa ikiwemo kufuta NGOs kwa kadri anavyotaka bila nguvu ya mahakama, tukumbuke kwamba sheria ya makampuni walau inaruhusu makampuni kwenda mahakamani kama yataonewa au usajili wake utafutwa, makampuni yana haki ya kwenda mahakama ya biashara, lakini kwa NGOs kwa sasa hali ni tofauti zinaweza kufutwa tu pale msajili anavyotaka na hakuna nafasi ya kwenda mahakamani. Lengo kubwa hapa ilikuwa ni kujenga mazingira ya serikali kuwa na nguvu kufanya chochote kwenye hizi NGOs.Sheria nyingi iliyotungwa ilikuwa ni sheria ya uhujumu uchumi na pia kukiri makosa ya jinai, lakini sheria hii ilijengwa kwenye mazingira magumu kwa watuhumiwa, mfumo wake ilikuwa inalenga kupora haki za watu kunyanyasa watuhumiwa, malengo makubwa ikiwa ni kuipa nguvu serikali kudhibiti wafanyabishara, wanasheria na wanaharakati mbalimbali nchini.  Sheria nyingine mbaya ni ile ya vyombo vya habari na sheria ya masuala ya uharifu wa kimtandao, malengo makubwa yakiwa ni kukwamisha ukosoaji na pia kuondoa habari za uchunguzi, sheria zote mbili ziliondoa kwa kiasi kikubwa sana haki ya wananchi kupata habari na kuruhusu upande mmoja wa serikali kutoa taarifa ambazo zilikosa kitu kinachoitwa check and balance, kila ilichosema serikali ndicho kilikuwa ukweli, hakuna habari za uchunguzi ambazo ziliruhusiwa sababu magazeti mengi sana yalifunngiwa kwa wakati huo. Hii ilitoa nafasi kubwa sana kwa serikali kupotosha kwa masuala mengi na kupotosha kuhusu miradi mingi na hakuna namna zaidi ya  wananchi kupata habari  za upande mmoja tu. Moja kubwa ambalo utawala wa awamu ya Tano ulifanya ilikuwa ni pamoja na kudhibiti mikutano ya vyombo vya habari, suala hili ilikuwa ni kuondosha kabisa hali ya uhuru wa watu kukusanyika, mikutano mingine yote iliathirika pia, baada ya zuio hili mikutano mingine kama ile ya AZAKI kuelimisha wananchi nayo ilidhibitiwa kimya kimya, japo ile ya vyama vya siasa ilikuwa ni agizo la waziwazi,  Serikali pia ilitunga sheria ya TAKWIMU, sheria hii ni moja ya sheria mbaya sana kuwahi kutoka nchini, sheria hii ilimpa nguvu MTAKWIMU kumiliki takwimu zote, hakuna mtu aliyeruhusiwa kufanya tafiti bila kibali chake, hakuna takwimu zinaruhusiwa nchini bila kupewa kibali, na kibali hiki ni kuanzia wakati wa kufanya utafiti na wakati wa kutoa takwimu zenyewe, kwa maana nyingine mtakwimu ndiye anayeendesha kila kitu kunzia utafiti wenyewe na mpaka kutoa takwimu yenyewe, hii inaondoa uhuru wa watu kufanya tafiti bila kuingiliwa na serikali, hakuna uhuru wa kutengeneza taarifa bila serikali kuweka mikono hivyo kudhibiti mambo yote ambayo serikali haivipendi. Sheria hii imetumika sana kusaidia serikali kuwa na taarifa za kiuchumi na maendeleo bila mbadala wa vyombo huru pia kufanya tafiti na namna hiyo bila kuingiliwa na serikali.Serikali ya awamu ya tano pia ilithibiti watoto wa kike kupata haki ya elimu, kupitia maagizo ya Rais Magufuli kulipigwa marufuku kwa watoto wa kike kurudi shule baada ya kujifungua , ndipo kampeni ya #ArudiShule ilipoanza na ile ya #ElimuBilaUbaguzi kampeni zote mbili zilikuwa na madhila kwa walioshiriki kuzifanya zikiwemo NGOs, kuna NGOs zilifungiwa kwa kushiriki kampeni hizi lakini pia pamoja na hayo imekuwa kampeni endelevu kudai haki ya watoto wa kike kupata elimu hata wakati huo mgumu wa Rais MagufuliHaya ni baadhi ya mambo ambayo yaliyoyafanywa katika utawala wake yake ikiwemo  Marufuku za Rais Magufuli ambazo ziliathiri wananchi,  uhuru  na Haki zao:  Kupingwa Mafuruku Matangazo mubashara ya bunge;  Mwanzoni mwa 2016, serikali ya Magufuli iliminya matangazo hayo kwa kuanza na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) na baadae mpaka kwa televisheni binafsi. Matangazo mubashara ni yale ya kipindi cha maswali na majibu tu. Mijadala haiKkurushwi mubashara tena. Nape Nnauye, ambaye alikuwa waziri wa habari wakati huo, aliitetea uamuzi huo akisema kuwa ilikuwa ni mzigo mzito kifedha kwa TBC kurusha matangazo hayo mbashara. Alisema kwa siku moja TBC ilikuwa ikiingia gharama ya Tsh 4.2 sawa na dola milioni 1.8. Pia alidai kuwa Tanzania si nchi ya kwanza katika Jumuiya ya Madola kufanya hivyo.Lakini Rais Magufuli alikuwa akizunguka na TBC nchi nzima na kila mahali anapokwenda bila vikwazo vyovyote vya gharama kwa shirika ili  Wanafunzi wanaopata ujauzito;  Serikali ya MagufulI iliendeleza katazo la wanafunzi wanaopata ujauzito kuendelea na masomo baada ya kujifungua. Hata hivyo, Magufuli amezuia jitihada za kuondosha katazo hilo ambalo limedumu kwa muda mrefu hadi sasa. https://drive.google.com/file/d/1QgZgR9nedV3DKQW0V38HFMzbbNQvbxh4/view?usp=share_link Mikutano ya siasa Mara baada tu ya kuingia Ikulu, Magufuli aliweka wazi msimamo wake kuwa hatopenda kuwaona wanasiasa wakizunguka nchi nzima kufanya mikutano ya hadhara. Kuanzia hapo mikutano ya hadhara na majukwa ya siasa kwa ujumla yalizuiliwa kwa wapinzani na kupelekea Chama kikuu cha upinzani cha Chadema kutangaza operesheni ya kupinga kile walichokiita Udikteta Tanzania (UKUTA) na kudhamiria kufanya maandamano ya nchi nzima mwaka 2016, lakini waliisitisha kabla ya kuanza. Toka kipindi hiko, polisi waliwashughulikia  viongozi wa upinzani wanaodaiwa kukaidi marufuku hiyo - na takriban wabunge 17 wa upinzani walifikishwa mahakamani kukabiliana na mashtaka. Aliminya uhuru wa habari na kujieleza kwa ujumla wake. Kwa kutunga sheria kandamizi dhidi ya uhuru wa habari, pia  vyombo vya habari kadhaa vilifungiwa kwa muda tofauti kwa kutangaza ama kuchapisha taarifa ambazo mamlaka inadai kuwa ni 'chonganishi' ama zenye 'kupotosha' umma. Lakini pia mwaka 2017 aliwaonya wamiliki wa vyombo vya habari kuwa wajiangalie, na kuwa hawana uhuru kwa kiasi wanachofikiria. Kutekwa, kupotezwa, kuumizwa na kubambikiwa kesi kwa wanasiasa na wanaharakati  - Wasiojulikana kufanya kazi bila wasiwasi Baada ya kuingia madarakani Magufuli alitengeneza mkakati kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kuwaumiza wananchi wote ambao walikua wakikosoa ama kwenda kinyume na utawala wake. Wanaharakati mfano, Tito  Magoti na  Theodory Giyani, walifikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakikabiliwa na mashtaka matatu ya uhujumu uchumi. Mwandishi wa masuala ya uchunguzi nchini Tanzania Eric Kabendera aliwekwa mahabusu kwa zaidi ya miezi sita kwa kesi ya kukwepa kodi, Azory Gwanda, Ben Saanane na wengineo.  Serikali ya Rais Magufuli haikufanya juhudi zozote kuondoa wasijulikana, wala kufanya operation ya kutafuta wasiojulikana , Lakini tuliona akiibuka mtu aliyetambulika kama Mwanaharakati Huru Musiba akitisha watu na kutukana watu, akapewa mpaka fursa ya kutengeneza gazeti ambalo lilikuwa na wadhamini likiwemo SHIRIKA la Ndege ATCL ambalo likuwa na matangazo kwenye gazeti hili, Gazeti ambalo lilikuwa linaendika uzushi na kuchafua watu, lakini pia watu wote walioumizwa hakuna aliyelipwa fidia au kusakwa kwa watu waliowaliohusika Kupigwa Risasi , Moja ya tukio baya sana kuwahi kutoka nchini  katika siasa ni kupigwa risasi kwa mwanasiasa Tundu Lissu, lakin serikali ikakataa kumpa huduma ya matibabu, bunge likaondoa haki zake zote za malipo na matibabu, lakini serikali ikasema haihusiki na shambulio hilo, japo matendo yake yalileta maswali mengi, imekuje basi ikagoma kumtibia? Imekuwaje basi ikamuondolea haki zake za malipo kama mbunge wakati ambao akahitaji sana fedha kwa kujitibia na kujikimu ? Katiba Mpya ;  katika utawala wa Magufuli  aliweka wazi kutoendelea na mchakato wa katiba mpya ambao ulinzishwa na Rais wa nyuma yake Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Magufuli alikataa kabisa michakato ya kuboresha sheria nchini , hakutaka nchi kupata msiingi bora ya utawala.  Miaka miwili  ya Mama Samia madarakani:  Samia Suluhu Hassan ndiye mwanamke wa kwanza kuwa Rais nchini Tanzania. Samia aliapishwa siku ya Ijumaa tahere 19/03/2021  katika ikulu ya jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, Rais Samia Suluhu Hassan atahudumu kwa kipindi kilichosalia cha muhula wa Urais wa Awamu ya Tano, Japo kuna watu wanasema hii ni Awamu ya Sita kitu ambacho kinazua sana mjadala mpaka, kwa sababu katiba inasema wazi makamu atamaliza kipindi kilichobaki na sio kipindi kipya cha awamu, lakini ili tutalicha kuwa mjadala wa siku nyingine,Baada ya  kifo cha Rais John Pombe Magufuli na Rais Samia kuingia Madarakani alianza kwa mambo yote ya Magufuli na kusema yeye ni sawa na Magufuli, alichukua sheria zote zote za Magufuli ambazo zinaendelea mpaka leo, alichukua miradi yote ya Magufuli na wateule wote wa Magufuli pia aliendelea nao, Rais Samia hajawahi kuteua waziri Mkuu kama Katiba inavyotaka, na kisha yeye na waziri Mkuu kushauriana kuunda baraza la mawaziri hii hajafanya pia, kwa maana nyingine kuna ukakasi kikatiba kwa namna alivyounda baraza la mawaziri kwa sababu waziri mkuu wa sasa Kasimu Majaliwa hana kiapo kwa Rais Aliyepo madarakani, aliapa kwa katiba na kutia Rais Magufuli sio Samia. Hili tatizo lipo mpaka leo na ni tatizo la kikatiba. Katika kipindi cha awamu ya 5 Rais Samia alikuwa ameshika wadhifa wa makamu wa Rais, kipindi ambacho kilikuwa na ukiukwaji wa haki na demokrasia, haki za binadamu na kutungwa sheria ngumu na mbaya sana kuwahi kutokea nchini, ukiukwaji ulikuwa ni  kwa kiwango kikubwa sana, watu waliporwa mali zao na wengine waliumizwa vibaya sana na vyombo vya dola na mamlaka ya mapato TRA.   Mara baada ya kuingia madarakani, Rais Samia alianza kujipambanua kama yeye ni Magufuli yeye na Magufuli ni sawa, baada ya changamoto za uchumi kuzidi na msukumo wa umma, tuliona kidogo kidogo alionyesha kwa umma ahadi ya kutafuta uwanja wenye usawa kidemokrasia, alianza na msema wa 4R, kisha akaunda KIKOSI KAZI, kikosi kazi ilikuwa ni moja ya mbingu chakavu ambayo ilipingwa sana na umma, mwanzo alisema watamsaidia kuboresha masuala ya kidemokrasia na ushauri kuhusu sheria zinazokwamisha demokrasia nchini, kwa bahati mbaya sana aliunda kikosi kazi na kuweka watu ambao kwa asilimia kubwa walikuwa ni dhaifu na pia walioshangilia uchaguzi 2020 Mfano Mkandara kupitia Redit walisema uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, Baadaye alikutana na vyama vya  siasa hasa CHADEMA ambao waligoma kushiriki katika kikosi kazi, kwa malengo ya kutaka kujenga  demokrasia, umoja na  amani na kuweka mazingira sawa ya kisiasa. Kuna matokeo kwenye hili vyama vya siasa kwa sasa vinaweza kufanya mikutano yao ya kisiasa, Hii ikiwa ni moja ya agizo la Rais Samia alipoingia madakarani akijaribu kutumia mbinu za Magufuli, lakini alishindwa na kuruhusu mikutnao ya vyama vya siasa kufanyika Katika kipindi cha miaka miwili ya Rais Samia kuna masuala ambayo bado anayapa kisogo ambayo hayaonyeshi nia ya dhati ya kulikomboa Taifa hili. Nayo ni kama yafuatayo #KatibaMpya : katika awamu zote za utawala wa CCM katika nchi hii suala la katiba mpya limekuwa likipigwa danadana na kusogezwa mbele na wakati mwingine mchakato kuanzishwa na kuishia njiani kwa kuwa ni dhahiri kuwa katiba hii ni dhaifu na ina mapungufu mengi na kupelekea kila serikali inapoingia madarakani kuwa na utawala wa kibabe kwa nguvu kubwa ambayo anakuwanayo Rais. Katika hotuba yake ya hivi karibuni ambayo aliitoa katika mkutano wa wanawake BAWACHA, alipokuwa mgeni rasmi Rais alisema kuwa suala la mabadiliko ya  katiba ni la mageuzi na ni la taratibu huku akiahidi kuuanza kulifanyia kazi bila kutaja wakati mchakato huo utakapoanzia. https://www.youtube.com/live/2cxJTxMxclo?feature=share HAKUNA sababu za msingi mpaka sasa kwa nini mchakato wa #KatibaMpya umeshikiliwa na serikali ya Rais Samia wakati huo huo akisema yeye anapigania demokrasia Uhuru wa Mahakama; uhuru wa mahakama bado unaonekana kuingiliwa kwa maslahi serikali na chama cha mapinduzi, kwa kiasi kikubwa sana  serikali inajisafisha sana kupita mahakama, mfano mzuri ni Kesi ya Ugaidi ya Mbowe na Kesi nyingi za mashekhe, serikali ikitaka kufanya suala baya kwa mtu kutumia mahakama na ikitaka kukandamiza mtu pia tumeona mahakama inatumika, kuna Watanzania wengi wako mahabusu kwa miaka mingi kwa sababu serikali inataka iwe hivyo, na siku serikali ikiondoa nia ya kesi hizo kesi zinafutwa, hakuna siku mahakama imetoa maagizo kufuta kesi zenye mwelekeo usio na ushahidi wa kutosha ambazo zinajulikana kama tunaendelea na UPELELEZI,  HALI HII BADO INAENDELEA hata wakati huu wa Rais Samia akiwa madarakani, lakini hivi karibuni aliyekuwa mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema wakati anataka kurudi Rais Samia alisema kwamba alimwambia aje na akamfutia kesi, haya ni maneno ya Rais mwenyewe kwamba kwa mazingira yaliyopo ni yeye anayeweza kutaka kesi iendelee au iondolewe, Kwa kauli ya  Rais alimuahidi kuzifuta na hatimae akarejea nchini, hii ni katika hali ya kutaka kuonyesha kuwa sasa maridhiano ya kisiasa yanaendelea vizuri, lakini hii sio sawa katika misingi ya utawala bora kwa sababu hakuna Mtanzania anayetakiwa kuwa na kesi sababu Rais ametaka hivyo au kufutiwa kesi kwa sababu pia Rais amependa hivyo, lakini kwa upande mwingine katika siku ya wanawake alipoulizwa kuhusu hatma ya wabunge wanawake 19 alijibu kuwa suala lipo mahakamani na hawezi kuingilia mahakama, hivyo bado kuna mkanganyiko wa uhuru wa mahakama nchini. https://www.youtube.com/live/2cxJTxMxclo?feature=share na bahati mbaya zaidi suala la Wabunge 19 sio la kimahakama ni suala la Spika kutaka wabunge hao mahakamani, hakuna kesi mahakamani inayozuia wabunge hao kuondolewa, wabunge hao wanakesi mahakamani dhidi ya chama chao wakitaka kurudishiwa uanachama, lakini kwa sasa hawana unanachama wowote hivyo kupoteza sifa ya kuwa wabunge. Wanafunzi wanaopata ujauzito; Tangu Rais Samia aingie madarakani wanafunzi wanaopata ujauzito HAWAJAPATA nafuu yeyote, Rais wa sasa kuwa Mzanzibar ambapo huko watoto wanarudishwa shule baada ya ujauzito na kuwa mwanamke hili suala lilionekana kuwa jepesi sana kwake, lakini kumekuwa na propaganda kubwa sana kuhusu suala hili ila ukweli ni kwamba watoto wake hawana haki ya kuendelea na masomo baada ya kujifunga, hakuna mfumo wa kuondoa na kurudisha watoto hawa shulenu kama ilivyo kwa Zanzibar, inawezekana vipi Rais anayetoka upande moja wa Muungano ambao una utararibu mzuri kurudisha watoto shule (http://idc-tz.org/news/the-spinsters-and-single-parent-children-protection-act-2005) ameshindwa kufanya hivyo kama suala la Muungano? Mpaka sasa hakuna  mswaada wowote bungeni kuhusu utararibu na sheria ya kuwarudisha shuleni wanafunzi wa kike waliopata ujauzito baada ya kujifungua . Uhuru wa habari na kujieleza; katika kipindi cha miaka miwili ya Samia alipongia tu madarakani alifungua magazeti japo kwa masharti ya kwenda kuzungumza na waziri, hakuna uwazi wa nini kilichozungumzwa huko, lakini pia tumeshuhudia mikasa ya vyombo kupigwa faini na vingine kunyimwa leseni, Vyombo vya habari vilivyokuwa vimefungiwa katika kipindi cha awamu ya tano ilitumika sheria ambayo mpaka sasa bado iko na serikali ya Samia haijafanya juhudu yoyote kuondosha sheria mbaya za vyombo vya habari na ile ya matumizi ya mitandao au makosa ya mtandao ,Changamoto ya pili kwa vyombo vya habari ni agizo la Waziri wa Habari Nape, kwamba vyombo vya habari viwe makini katika kutoa habari za mikutano hiyo, na ikiwezekana wasirushe mubashara wafanye record na kisha kuhariri na kurusha, hii ni ishara ya kukosa uhuru wa habari kwa sababu tishio hili la waziri linawanyima wanahabari haki ya kutoa habari kama zilivyotokea lakini kuzihariri kama anavyopenda waziri. Hii imefanyika wakati huu wa Serikali ya Rais Samia, alichomaanisha waziri wa habari Nape Nnauye alivionya vyombo vya habari kuchuja maudhui na wasilete habari kama zilivyo. Kauli hiyo haikukoselewa na Rais hiyo ikionyesha kukubaliana na hicho kilichosemwa na waziri huyo. Pia gazeti la Demokrasia february 27, 2023 lilizuiwa  kusambazwa kwa siku hiyo likiwa tayari limeshachapwa kufuatia tukio hili bado uongozi wa Samia una changamoto katika suala zima la uhuru wa habari na kuzuia habari ambazo wanahisi wao zitawaharibia utawala wao.https://drive.google.com/file/d/1rTlzswaajRwbzQEkPd_qZvcojgsggqnb/view?usp=share_link. Kuna muendelezo wa matukio ambayo yamekuwa yakiashiria kuwa katika utawala wa Samia hadi sasa bado wananchi wanaokosoa serikali wanawekewa vikwazo mtangazaji Gerald Hando alikosoa suala la Rais kukopa sana pesa nje na ilipelekea kupoteza ajira yake lakini alikuwa ana haki kikatiba ya kutoa maoni juu ya suala hilo.https://drive.google.com/file/d/1fE0lT-aU8ZyL5dC9t5aHWaJoGj3No5_l/view?usp=share_link Suala la utekaji na wasiojulikana; katika kipindi cha miaka miwili ya Samia inaonekana bado kuna muendelezo wa matukio ya kutekwa kwa watu na tuhuma muda mwingine zikienda kwa polisi na watu hao kutoonekana tena kama vile tukio la vijana watano waliotekwa Kigamboni, https://twitter.com/mariastsehai/status/1495637621393043460?lang=en na kijana Williaam sije ambaye alichukuliwa na polisi na kutoonekana tena na  Baba yake mzazi alipita ngazi zote kutaka kujua mtoto wake yuko wapi lakini hakuna kilichoendelea. https://drive.google.com/file/d/1Fuvfb_kP-eg1fsBeD2xhMsK76wSVoTMU/view?usp=share_link. Pia matishio kwa wanasiasa wa upinzani walioonekana kukosoa serikali yameendelea kama ilivyotokea kwa kijana Nicholaus clinton wa NSSR Mageuzi alipotekwa na wasiojulikana na baadaye kupatikana akiwa  na hali mbaya na hakuweza kuzungumza chochote.  https://twitter.com/MariaSTsehai/status/1620379360325931010 Hii inafanya tuone kuwa utawala wa Samia bado una mapungufu yale ambayo yapo katika awamu zote zilizoongoza Chama Cha Mapinduzi. Kutobadili sheria kandamizi zilizopitishwa awamu ya tano; katika kipindi cha awamu ya tano kulipitishwa sheria ambazo ziliongeza kinga kwa watu ambao hawatakiwi kushtakiwa, hii inashusha uwajibikaji na kuongeza kasi ya watumishi na viongozi kutokuwa waadilifu wakijua fika kuwa hawawezi kuwajibishwa popote pale. sheria ya Mtandao ambayo ilitumika zaidi kuuzima uhuru wa kujieleza kwa wananchi. Katika kipindi hiki cha Samia hakuna sheria iliyobadilishwa na zote zinaendelea kutumika kukandamiza Watanzania. Kuna sheria nyingi kandamizi zilizotungwa wakati wa Magufuli lakini mpaka leo sheria zote hizo bado ziko na zinaendelea kutumika.  Tume Ya Haki na Maridhiano ya Kitaifa;  Wakati wa Rais Magufuli watu wengi waliumizwa , watu kutoka jamii zote walipata changamoto kuna wanaharakati, wafanyabiashara pia wanasiasa, kwa bahati mbaya sana serikali ya Rais Samia imeshindwa kabisa kuponya Taifa na makundi yote yaliyoathirika, tunaona kuna juhudi ya kuweka sawa mambo ya wanasiasa lakini kuna ukimya na giza kubwa sana kwa makundi mengine yaliyoumizwa na awamu ya tano, Je hii ina maana gani? Kwa nini Rais anashindwa kuondoa vikwazo kwa watu waliowekewa redflag kwenye passport zao, Mfano Prof Wajakoya aliyekuwa Wakili wa Lema na Watanzania wengine wengi waliokuwa wanatafutwa na serikali ya Rais Magufuli kutokana na kutofautiana na serikali yake. Mauaji Ndani ya jeshi la Polisi; Kuna malalamiko mengi sana kutoka kwa wananchi kuhusu mauaji ya polisi, Mwaka Jana tuliona video kutoka Serengeti Polisi wamefanya mauaji ya mzee mwenye familia, ambaye ni ndugu wa aliyekuwa Mbunge Catherine Ruge, Baadaye aliibuka Mzee William Sije naye akilalamika kuhusu mwanae kupotezwa na Jeshi la Polisi , amefuatilia sana bila mafanikio, lakini haya yamefanyika wakati wa serikali ya Rais Samia Kuporwa Ardhi Maasai wa Loliondo; Chini ya Rais Samia tumeshuhudia ukatili mkubwa sana kwa wakazi wa Ngorongoro hasa Loliondo, Wananchi wameporwa ardhi yao kinguvu, nguvu kubwa ya dola imetumika na kusababisha watu kukimbia nchi na wengine kusadikiwa kupoteza maisha wakikimbia maporini, sheria ya ardhi haikuheshimiwa kabisa na serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, masuala ya wananchi kuporwa ardhi yameenea sana mpaka huko Mbarali katika mabonde ambayo wananchi wamekuwa wakilima mpunga na kulisha nchi kwa miaka mingi. Mwisho na kwa umuhimu sana ni miaka miwili ya Rais Samia bila mchakato wa katiba mpya , hakuna dalili njema mpaka sasa kuelekea kupata #KatibaMpya  Kwa mambo hayo kadhaa yanayoendelea nchini ili Rais Samia aonekane ana nia thabiti ya kulikomboa Taifa hili jambo la kwanza la muhimu kuliko yote analotakiwa kufanya ni kubadili katiba hii ya sasa na kuleta katiba itakayoleta haki, uhuru na usawa kwa wananchi wote na kuondoa changamoto zote ambazo  zinaonekana zipo kwa ajili ya uwepo wa sheria mbovu nchini. #WenyeNchiWananchi #ChangeTanzania  #KatibaMpya

Read More Download Document

Changamoto za mabadiliko ya mfuko wa bima (NHIF  – TOTO AFYA);

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) imetangaza kusitisha utaratibu wa matumizi ya Toto Afya Kadi kwa watoto wakiwamo wanafunzi wa Shule ya msingi. Toto Afya Kadi ni kifurushi maalumu ambayo watoto walipatiwa huduma mwaka 1kwa gharama ya Sh50,400/= , BIMA hii ilikuwa mkombozi kwa Watanzania wenye kipato cha chini, gharama ya bima hii ilikuwa nafuu kwa wengi na ni moja ya huduma ambayo ilipokelewa kwa shangwe ya Watanzania walio wengi, lakini kutokana na maboresho mfumo huo umesitishwa. Mabadiliko haya yalitolewa siku ya  Jumatatu Machi 13, katika taarifa ya NHIF kwa umma. Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bwana Bernad Konga alisema kama baba hana bima sasa anaruhusiwa kukata ili amjumuishe na mwanawe katika bima hiyo.Hii ni kasoro ya kwanza, Kwa nini NHIF wanashinikiza Waziza kuwa na BIMA ili watoto wapate bima? Vipi kama mzazi kwa wakati huo hana fedha za kutosha kukata bima yake na ya watoto? Na kwamba angependa kuchukua bila ya watoto kwanza wakati anajipanga kuchukua bila yake? Huduma za afya zinapofanya kwenye mfumo wa kuangalia namna ya kutengeneza wateja ( wazazi kuchukua bima kwanza ndipo watoto wapate bima)  Haki ya huduma ya afya kwa watoto imeingia kwenye suala la utata sana, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), umetangaza kuwa watoto ambao awali walikuwa wakisajiliwa kupitia utaratibu wa bima ya afya ya ‘Toto Afya kadi, sasa watasajiliwa kupitia vifurushi vya bima ya afya au shule wanazosoma. Ili ni Tatizo la pili, kuna watoto wadogo wengi sana ambao hawajaanza kuingia kwenye masomo, je watakosa bima sababu hawako shule? Hii ina maana gani kwa watoto wachanganya? Kwa nini mfumo huu usiunganishwe na serikali za mtaa na iwe kwa watoto wote.Kwa nini tunasema mfumo wa kutumia shule unaweza kuwa na changamoto? Je ni watoto wote wanazaliwa wakiwa na uwezo kushiki masomo katika shule? Vipi kama mtoto ana changamoto ambazo awezi kujiunga na masomo katika shule za kawaida na katika umri wa kawaida? Mfumo huu umeleta changamoto ya ubaguzi kwa watoto wengi sana. Hii inaonyesha wazi kuwa Serikali kupitia  wizara husika hawajajipanga, waangalie njia nzuri ya maboresho, kufanya hivi kutapelekea watu wa kipato cha chini kushindwa kumudu gharama za Bima kubwa ambazo zitajumuisha na watoto wao na kupelekea watoto wengi kukosa matibabu.  Taarifa ya NHIF haijaweka bayana kuwa huduma hiyo imesitishwa kwa muda gani, uamuzi huu ni kinyume cha kifungu cha 8 cha Sheria ya Mtoto No 21 ya 2009 ( https://www.lecriconsult.co.tz/files/SHERIA%20YA%20MTOTO%20YA%20MWAKA%2020141.pdf ) kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019 ambayo inasisitiza mtoto anapaswa apate haki ya huduma ya afya na kinga katika kustawisha ukuaji wake na pia ibara ya 24 ya mkataba wa Kimataifa wa Haki za mtoto 1989, ambayo inasisitiza haki ya mtoto ya kufurahia kiwango cha juu kinachoweza kufikiwa kiafya na vifaa kwa ajili ya matibabu ya magonjwa na maslahi ya mtoto kwa afya (https://www.ohchr.org/sites/default/files/Documents/ProfessionalInterest/crc.pdf).  bara ya 14 ya mkataba wa Afrika wa haki na ustawi wa mtoto 1989 pia inasisitiza kila mtoto ana haki ya kufurahia kupata haki kwa maslahi ya kiafya. ( https://au.int/sites/default/files/treaties/36804-treaty-0014_-_african_charter_on_the_rights_and_welfare_of_the_child_e.pdf ) Kulikuwa na ulazima gani kwa mabadiliko kabla ya NHIF kuwa tayari kuanzisha mfumo mpya? Suala la bima ya afya sio suala la kuvurugwa namna hii, hakuna sababu kubwa zilizopo sasa zilizopeleka uhalaka wa kufanya mabadiliko haya na kuweka watoto wengi katika hatari ya kukosa huduma ya matibabu bila sababu za msingi.  Serikali imemua kukandamiza wazi watoto HAKI yao ya bima ya afya. Kilichofanyika kama mzazi hana uhitaji au uhiari wa kuwa na bima ya afya na mtoto anakosa haki ya kupata bima hiyo jambo ambalo linakwenda kinyume na matakwa ya sheria. Serikali inataka kufanya wananchi wake wawe na maisha magumu zaidi. Bima za afya ni ghali sana na haiendani na hali ya uchumi wa wananchi walio wengi. Mapendekezo;  Taarifa ya NHIF iweke bayana kuwa huduma hiyo imesitishwa kwa muda gani na kwa sababu gani. https://drive.google.com/file/d/1QxUaoGb8oX0aoV5Xn16yZopjnXJeAHdL/view?usp=share_link Toto Afya Kadi ingeachwa iendelee huku wakiendelea na maboresho mpaka pale watapokuwa na mfumo mpya utaratibu mpya. Bima kwa wote izingatie na uchumi au kipato cha mwananchi, kwani maboresho mengi yamefanywa  kwa ongezeko la gharama na sio uboreshwaji wa huduma. Mfuko wa Bima ya Afya utafute chanzo kingine cha kuwawezesha kuzalisha kipato ili kufikia hadhi ya kuchangiwa kwa kiasi kidogo tu badala ya kutegemea chanzo cha mapato kutoka kwa wananchi pekee kwa ajili ya kuendesha mfuko huo wa Bima ya Afya, kwa sababu serikali ina wajibu wa kutoa huduma kwa jamii. Athari  Watoto wengi watakosa huduma ya afya kwa sababu wazazi wengi wanashindwa kumudu gharama za Bima kubwa ambyo inaweza kumjumuisha na mtoto. Bima ya Afya kwa wote itaathiri upatikanaji wa huduma zingine nyingine kutokana na masharti yaliyowekwa ikiwemo sharti la kutopata huduma nyingine kama leseni, viza, usajili wa wanafunzi mashuleni na vyuoni kama huna bima ya Afya.  #ChangeTanzania

Read More Download Document

Makala juu ya matumizi ya nishati chafu  yanavyoathiri watanzania.

Serikali kupitia wizara ya nishati inayosimamiwa na Mbunge January Yusuph Makamba imekuwa ikiwataka wananchi kutumia  nishati safi badala ya nishati chafu kwa kuwa inaathari nyingi kuanzia kiafya, mazingira na zaidi kwenye athari za mabadiliko ya tabia ya nchi. Zaidi ya asilimia 80 hutumia nishati chafu kwa matumizi ya kupika majumbani . Kwa mujibu wa takwimu za afya zinaonyesha  watanzania 33,000 wanapoteza maisha kila mwaka kutokana na matumizi ya nishati chafu ikiwemo mkaa, kuni, mabaki ya mazao kama vile  magunzi ya mahindi na kinyesi cha wanyama takwimu hizi zinaonyesha hali ni mbaya kuliko watu wanaokufa kwa, Malaria na hata kifua kikuu. Hii inaashiria kuwa matumizi hayo yanaathiri sana Watanzania wenye kipato cha chini wasioweza kumudu gharama za nishati safi na mbadala kama majiko ya gesi na majiko ya umeme au makaa ya kutengeneza bila kutumia miti. https://jikopoint.co.tz/jiko-news/matukio/nishati-safi-ya-kupikia-kunusuru-maisha-ya-watu-33000-kila-mwaka-tanzania Waziri wa nishati nchini mnamo Oktoba 25, 2022, alielezea kuwa athari za matumizi ya nishati chafu ya kupikia, pia alizindua  kampeni ya nishati safi ya kupikia. Katika kuangalia utekelezaji wa kampeni hakuna mabadiliko makubwa yaliyofikiwa na kampeni hiyo, lakini pia hakuna mwendelezo wa kampeni hiyo, Kikubwa kilichofanyika ilikuwa ni kongamano la mjadala  matumizi ya nishati safi ambapo Rais  Samia Suluhu Hassan aliagiza mamlaka za serikali kuunda kikosi kazi cha Taifa cha wataalamu kitakacho tengeneza mpango mkakati wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa kupikia. http://www.swahili.people.cn/n3/2022/1102/c416585-10166472.html Baada ya hapo hakuna kingine kilichofanyika mpaka kufikia mwaka  2023, hii inaonyesha dhahiri hakuna juhudi ya  serikali kudhibiti matumizi ya nishati chafu kwa wananchi moja kwa kuweka mazingira ya kufanya nishati safi kuwa nafuu, pili kutoa elimu kwa nguvu kwa kutumia majukwaa mbalimbali . Swali ni je serikali imejipanga vipi kuwezesha katika kuhakikisha Watanzania wote wanatoka kwenye matumizi ya nishati chafu kupikia? Je nishati safi ni nafuu vya kutosha kulingana na uchumi wa Watanzania walio wengi ? Serikali imejipanga vipi katika kumshawishi Mtanzania ambaye anatumia nishati inayotokana na kuni anayoitafuta bure au mkaa ambao ni bei rahisi kuingia kwenye matumizi ya nishati safi ambayo atailipia na ina bei ghali? Serikali imekuwa ikiweka mikakati  mizuri bila utekelezaji na mipango kubaki kwenye makaratasi, awali mwaka jana mwezi wa 8, Waziri January Makamba alibainisha mpango wa kuwezesha wananchi kumudu gharama za gesi na kuepukana na matumizi ya mkaa na kuni kwa utaratibu wa kumruhusu mteja kuinunua kwa bei ndogo kulingana na mahitaji yake. Alisema wananchi wengi wanashindwa kumudu kutokana na gharama kubwa zilizopo, moja ya vikwazo kwa Watanzania kutumia gesi ni kwamba lazima uwe na fedha nyingi kwa mkupuo. Wanataka kuleta teknolojia inayoruhusu mtu kununua gesi ya Sh 500 au Sh 1,000. Wataileta  sokoni ili watu waanze kununua gesi kama wanavyonunua kopo la mkaa au fungu la kuni, hivyo mchakato wa kuzipunguza unaelekea ukingoni ili kulifanyia mapinduzi suala hilo. https://bongo5.com/waziri-wa-nishati-january-makamba-amesema-serikali-kuja-na-kifurushi-cha-gesi-ya-kupikia-08-2022/ Serikali pia kupitia wizara ya afya, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu  21 Februari, 2023 aligawa mitungi midogo ya gesi kwa wajasiriamali wanawake 600 amesema kuwa matumizi ya nishati ya kuni na mkaa yamekuwa yakisababisha   saratani ya mfumo wa chakula. Ummy ameshauri kutumia nishati ya gesi kuepuka na madhara hayo. https://habarileo.co.tz/waziri-ummy-tumieni-gesi/ Kugawa mitungi ya gesi pekee haitoshi kwa kuwa hili ni jambo endelevu na pia ni matumizi ya kila siku si kwa wamama wajasiriamali tu bali watu wote majumbani na mahotelini ambapo nishati hiyo hutumika zaidi, serikali inatakiwa kuweka mifumo wezeshi ambayo kwa kiwango kikubwa itawawezesha wananchi kumudu matumizi ya gesi kwa kuwa inapatikana kwa wingi nchini, kwa nini bei iwe kubwa kiasi cha watu kushindwa kumudu? Matumizi ya nishati chafu hasa ya kuni maeneo ya vijijini imekuwa ni changamoto sana kwa kuwa kuni zinatafutwa maporini na kupelekea watafutaji wa nishati hiyo kupoteza muda mwingi kutafuta huku shughuli zao nyingine zikilala. Pia inapelekea watoto wa kike kuwa hatarini na kutendewa vitu vibaya kama kubakwa au kupata mimba za utotoni, pia kunasababisha uharibifu mkubwa wa misitu na mazingira kwa ujumla. Serikali inatakiwa kujua hii yote inapelekea kuzorota kwa uchumi na kutengeneza Taifa tegemezi na maskini muda wote. Sote tunaona namna mfumuko wa bei nchini Tanzania ulivyoshika kasi, Watanzania hasa wenye uchumi wa kati na chini imekuwa ni changamoto wao kumudu matumizi ya nishati safi. Wengi  wao hawamudu moja kwa moja wanatumia nishati safi pamoja na nishati chafu kwa kuwa hawawezi gharama na wengine hawawezi kabisa na kubaki kwenye matumizi ya nishati chafu. Vitu kama hivi serikali imeonekana kutoitilia mkazo katika kushughulikia matokeo yake wanaoumia ni wananchi, kama nishati safi haina madhara kiafya serikali ingehakikisha kwa namna yoyote ile wanapunguza au kumaliza kabisa tatizo hilo Uchumi wa Taifa letu unategemea sana watu wenye afya bora ili kusisimua uzalishaji katika nyanja zote za kiuchumi, hatuwezi kuwa na Taifa imara na kusonga mbele kama afya zetu zinazorota na magonjwa mbalimbali ikiwemo yanayotokana na matumizi ya nishati chafu ambayo yanagusa Watanzania walio wengi zaidi. Ni wakati wa serikali sasa kuonyesha kuwa wana nia ya dhati ya kuliondoa Taifa katika madhira haya na kulitoa Taifa kwenye umaskini na kuleta mbinu stahiki za kujikwamua kiuchumi, kielimu na kijamii. #ChangeTanzania

Read More Download Document

Uhuru wa mahakama uko wapi?

Ibara ya 107A.-(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema, “Mamlaka ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano itakuwa mikononi mwa Idara ya Mahakama na Idara ya Mahakama ya Zanzibar, na kwa hiyo hakuna chombo cha Seriikali wala cha Bunge au Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki.” "Mdogo wangu Lema amerudi, aliniambia anataka kurudi nikamwambia rudi, akasema Mama nina kesi, nikasema nazifuta rudi"-- Rais Samia Hassan Suluhu , Rais wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Hii inathibitisha wazi kuwa mahakama zetu haziko huru, majaji na watumishi wa mahakama wanaongoza kesi kwa kufuata amri za mhimili wa Serikali (Rais), hii ni hatari kubwa sana kwa sababu mahakama ni chombo cha kutenda haki na kusimamia haki za wananchi. Mara kadhaa Rais amekuwa akizungumzia masuala yaliyopo mahakamani kana kwamba yeye ndiye anayetoa hukumu na kuamua mwenendo wa kazi, yaani akiamuru kesi mbalimbali zisizo na msingi au za kubambikizwa zifutwe au kuendelea, huu sio utaratibu wa kikatiba hata kwa katiba ya sasa imeweka uhuru wa makahama kwa kiasi furani, Kwa kurejea mambo kadhaa yanayoonyesha kwamba kunakuingiwa kwa mahakama ni hivi karibuni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa Usa River Mkoani Arusha tarehe 04 Machi, 2023 akiwa katika kikao kazi cha Mawaziri na Makatibu Wakuu siku alisema  "Mdogo wangu Lema amerudi, aliniambia anataka kurudi nikamwambia rudi, akasema Mama nina kesi, nikasema nazifuta rudi"-Rais Samia Hassan Suluhu  https://www.youtube.com/watch?v=z453XSuveQI Lakini pia Viongozi wa dini walishawahi kutumia mkutano wao na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kumuomba atumie busara kumaliza kesi inayomkabili kiongozi wa Chama cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake wengine.  https://www.dw.com/sw/rais-samia-aombwa-kufuta-kesi-ya-mbowe/audio-60997390  lakini pia kiongozi wa ACT wazalendo Zitto Kabwe aliwahi kufanya maombi kama haya, na Rais akajibu huyo mwenzenu kuna makosa amafanya na yatashughulikiwa kwa mujibu wa sheria, lakini baada ya kelele nyingi za wananchi , Mbowe aliachiwa kwa kile kinachoonekana ni maagizo ya Rais, siku aliyotoka alikwenda Ikulu moja kwa moja usiku wa siku hiyo hiyo, hivyo kuwe mazingira kwamba Rais ameamua kesi yake kutoendelea, kwenye mjadala wa maridhiano pia kuwa mwanachama wa CDM wameachia wakiwa na kesi mbalimbali toka nyakati za uchaguzi 2020, CHADEMA wanasema ni kutokana ma mazungumzo hayo ndio maana wanachama wao wametolewa magerezani, Hii ina maana gani? Pamoja kwamba ni jambo zuri kwa watu wasio na hatia kuachiwa huru, lakini hii inaacha mashaka namna mfumo wa haki inavyoshindwa kuwatendea haki wananchi, na kinachotokea ni kwamba bila fadhila ya rais basi haki zao upotea, hii sio sawa kwa Taifa huru, Taifa ambalo linaendeshwa kwa misingi ya kidemokrasia  Nini kifanyike… #KatibaMpya ni suluhisho la uhuru wa mahakama, katiba iliyopo imemapa Rais na mhimili wote wa serikali nguvu ya kuingilia mihimili mingine ikiwemo Bunge na Mahakama, hivyo katiba hii ni hatari kwa maisha ya watanzania wote. Hayati mwalimu Julius Nyerere alishawahi kusema   “Tujenge utamaduni wa kudhibiti viongozi wetu kama wanavunja sheria ya nchi, tusiogope. Mkianza kuwa na woga, nawaambia mtatawaliwa na dikteta. Kama haifanyiki wanadhibitiwa, wale ambao wanavunja Katiba wanadhibitiwa na kusema kweli kabisa lazima tuwe serious katika jambo hilo. Katiba haiwezi kupuuzwa. Akishachaguliwa mtu ataapishwa kuilinda Katiba ili tuweze kumshtaki aliyeikiuka. Mtu yeyote ambaye hawezi kuilinda wala kuisimamia Katiba baada ya kuchaguliwa, hatufai, Udikteta ni Serikali ya mtu mmoja au kikundi cha watu wachache na wao ndiyo huwa sheria. Anayepinga watakayo, basi huonyeshwa cha mtema kuni,”- Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Ni wakati sasa wa kupata katiba mpya ili tujenge nchi kwa misingi ya Demokrasia, sheria na kwa ajili ya wananchi.   #ChangeTanzania

Read More Download Document

Je serikali ina nia ya kuleta unafuu kwenye mawasiliano? Hali ya upatikanaji na unafuu wa huduma.

Waziri wa habari, Teknolojia na mawasiliano  Nape Nnauye kipindi cha serikali ya awamu ya 5 aliwasilisha hoja Bungeni ya kuondosha a kurusha matangazo live kwenye televisheni na serikali ikafanikiwa kuyafunga matangazo, hii iliuzunisha wananchi wengi sana, hoja ilikuwa ni kwamba wabunge wengi wanaonge mambo kwa kutafuta sifa, kwamba wanafanya siasa, lakini sasa matangazo live yamerudi, utetezi wa kurudisha ni kwamba TBC zamani ilikuwa inapata hasara kubwa kurusha vipindi hivyo vya bunge, kwamba TBC ilikuwa inapata hasara ya billioni 4 , lakini ni TBC hiyo hiyo ilikuwa inazunguka na Rais Magufuli nchi nzima na kurusha matangazo yao, ila Bunge kama mhimili ikaonekana ni hasara kurusha matangazo yake, Wakati huu tena akiwa na dhamana hiyo hiyo ya Waziri wa habari Teknolojia na mawasiliano ameufungia mtandao maarufu wa Clubhouse. https://drive.google.com/file/d/1_FIrJUmiIf1GCxU_-NBVuoGFC7XJqhzL/view?usp=share_linkKampuni la kimataifa BlockNet walithibitisha hilo,  alisema wazi kwamba CLUB HOUSE ilikuwa imefungiwa nchini Tanzania, Waziri Nape alijitokeza na kupinga baadaye ya kutoa kauli yake lisaa limoja mbele Club House ikafunguliwa, TCRA wakasema kulikuwa na hitilafu, lakini Club House haiwezi kupata hitilafu Tanzania pekee yake, kwa sababu ana mifumo yake hapa nchini, kama ingekuwa na mifumo hapa nchini ingeweza kueleweka. Mtandao wa Clubhouse, ni mtandao ambao watu popote pale walipo duniani huingia kujadiliana mada mbalimbali za maisha yao, ikiwemo uchumi, mambo ya kijamii, siasa kwa uwazi na uhuru wa hali ya juu. Mtandao huu  umekuwa ukitumika  kwa kiasi kikubwa kutoa  elimu ya kuwaamsha watu na kuwapatia maarifa makubwa Watanzania, Hii ndio sababu kubwa ya  serikali ya CCM kuogopa na kuona  tishio la mtandao huu,  Mara nyingi serikali imekuwa pambana sana wakosoaji na pia  kukwepa uhuru wa wananchi kuikosoa serikali. https://drive.google.com/file/d/1HUsfb6jtfCUv7MvjNWbhN9zqdN6nkZZN/view?usp=share_link   Tukumbuke kuwa katika kipindi cha miaka 7 cha kuzuiliwa haki ya kukusanyika ambayo ipo kikatiba wananchi waliona ni vyema kutafuta njia mbadala za kutoa maoni yao na kupata uhuru wa kujieleza ambayo ni pamoja na  mtandao wa club house. Hivyo lengo la kufungia mtandao wa Clubhouse ili Watanzania wasiweze kukusanyika na kujadili mambo muhimu ya nchi yao. Tukumbuke Nape Nnauye ndiye  alikuwa kinara wa kutetea sheria kandamizi ya vyombo vya habari wakati alipokuwa waziri wa habari kipindi cha Magufuli.  Haiwezekani Rais Samia anasema kuwa anataka kuifungua nchi na uhuru wa maoni uwepo na kukosoa utawala wake ruksa, Lakini Waziri bila kuutarifu Umma anafungia mitandao na pia kwa nini Rais anaonekana kukereka na ukosaoji?.  Kwa hivi sasa bila kuwasha VPN huwezi kuupata mtandao huu kwa sababu Nape Nnauye kaufungia na bado anasisitiza kuzuia VPN, je lengo hasa ni nini?. https://drive.google.com/file/d/1jttifXXS-uFDl-gT81NWIE1ozQUnMjqb/view?usp=share_link Kwa nini serikali bado ina nguvu ya kukandamiza haki ya #UhuruWaKujieleza na kuweka kwa kuweka vizuizi hivyo? Hii mitandao kwa sasa ndio sehemu pekee ya kupaza sauti kutokana na hali mbaya ya watu kupotea mikononi mwa polisi na pia ilitumika  kumtetea Nape Nnauye kipindi kile katolewa bunduki njenje. Je kwa nini serikali haijifunzi?  Hii si mara ya kwanza kwa mitandao kupata tatizo nchini, iliwahi kutokea hivyo kwa mtandao wa Twitter, muda mchache kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka 2020. Kuna manufaa mengi kama mitandao ya jamii itatumika vizuri, hutumika kukuza na kutangaza biashara na hivyo wananchi kujipatia kipato. Serikali ilitakiwa kuweka urahisi zaidi katika kutumia mitando hii kwa kuweka unafuu wa bundle na kuhamasisha matumizi sahihi ya mitandao kwa maendeleo ya taifa. Mfano kutokana na uzinduzi wa mradi wa "Smart Kigali" unaoungwa mkono na serikali, watu nchini Rwanda sasa wanapata intaneti bila malipo kupitia vifaa vinavyowezeshwa na Wi-Fi. Mradi huo unaoendana na Dira ya 2020 ya Rwanda, unaashiria hatua nyingine ya kufikia matarajio ya taifa hilo la Afrika Mashariki ya kuwa kitovu cha IT kikanda katika mustakabali uliojengwa juu ya uchumi unaotegemea maarifa ili kuvutia uwekezaji zaidi kutoka nje. Sakata la Starlink Waziri Nape Nnauye amesema kuwa Kampuni hiyo inayomilikiwa na Elon Musk haijakidhi vigezo ilivyowekewa na serikali ikiwamo kufungua ofisi nchini Tanzania ili waweze kulinda data za watumiaji na kuwajibika kwa watanzania.  Starlink Wataleta Huduma Ya Internet Kwa Gharama Nafuu Kuliko Ilivyo Sasa kwani gharama za internet nchi zimekua kiasi cha GB 1 kufikia Shiling 3000 kwenye makampuni mengi ya simu. Maeneo mengi hususani vijijini yatanufaika kwani ni maeneo machache ya vijijini ambayo yamefikiwa na mtandao. Itatengeneza ajira, na pesa nyingi kutokana na leseni watakayopewa walitengenezea Taifa pesa nyingi zinazotokana na kodi. Starlink sasa inapatikana Nigeria Waziri wa Mawasiliano na Uchumi wa Dijitali, Isa Pantami, alisema kuwa Nigeria imepata asilimia 100 ya mawasiliano ya mtandao wa intaneti kutokana na uzinduzi wa huduma ya satelaiti. Starlink ilipokea leseni za kufanya kazi nchini Nigeria na Msumbiji mwaka jana. Hatua ya Waziri Nape Nauye hakusema kwanini kampuni ya Starlink kugoma kukubaliana na masharti ya kufungua ofisi pamoja na kuonyesha kwa namna gani watalinda data za wateja wao.  Hii imezua maswali mengi kwa wananchi mojawapo ikiwa wanahoji kuwa kuna mitandao mingi ya kijamii kama Twitter, Instagram Facebook na mingineyo mbona yenyewe ipo na inatumika kwa wingi nchini na hakuna hata mmoja mwenye ofisi nchini na hatujaona hatua zozote zilizochukuliwa na waziri kuzitaka ziwe na ofisi? Tukizungumzia suala la wawekezaji kuwa na ofisi nchini serikali imepitisha sheria ngumu ambazo si rahisi mwekezaji ambaye ana lengo la kufanya biashara na kupata faida anaweza kufikiria kua na ofisi nchini, mfano sheria ya kodi ya manunuzi ni 18%, lakini kwa nchi Kama Marekani haijawahi kuzidi 9%, kwa mfano huo mdogo, bado tunahitaji ukarabati madhubuti wa sheria ili kupata wawekezaji na kukuza uchumi wa Tanzania  #UhuruWaKujieleza #ChangeTanzania

Read More Download Document

Ubovu Wa Miundombinu Ni Changamoto Katika Elimu

Sekta ya elimu ni  nyeti katika ukuaji na maendeleo ya nchi. Sekta hii ipo chini ya Wizara ya Elimu. Licha ya kuwa na umuhimu katika Taifa sekta hii inakabiliana na changamoto kadhaa ikiwemo miundombinu bora na vifaa vya kujifunzia  wanafunzi, hali ya  madarasa sio bora na vitendea kazi kwa walimu na wanafunzi vinakatisha tamaa sana , Vyoo vya shule (Matundu ya choo) bado ni mtihani katika nchi yetu hasa baada ya miaka 61 ya uhuru tumeshindwa kumudu matundu ya vyoo katika shule zetu. Hivi karibuni tuliona Shule kongwe ya msingi ya Kibeta iliyopo ndani ya Manispaa ya Bukoba yenye jumla ya wanafunzi 967, ikikabiliwa na changamoto ya upungufu wa madawati , ambapo baadhi ya wanafunzi  wanakaa zaidi ya wawili katika dawati moja huku wengine wakikaa sakafuni. https://drive.google.com/file/d/1CxhcWgG0-CMGtgT_Y8u4f5HirJl8jIGS/view?usp=share_link  hii ni hali ya kawaida sana katika shule zilizo nyingi. Shule ya Mvinza Kagerankanda haina madarasa wala madawati. Shule ipo Wilayani Kasulu, Kigoma ina Wanafunzi 2,111, wengi wanasomea nje huku waliopo Darasani wakikaa chini. Madarasa yapo 12, yanahitajika 46 ili kukidhi mahitaji  Madawati ni 694 yapo 184 tu. https://drive.google.com/file/d/1UQtJdmi20gEt5aN1zgS7UZrxc4UKiIZm/view?usp=share_link  Hii ni mifano bora ya shule duni, watoto wetu wanakosa fursa ya kusoma katika mazingira bora kwa sababu serikali haijaweka kipaumbele, kwa sababu wazazi wameacha suala la elimu na kulitelekeza kwa serikali, wameshindwa kuisukuma serikali kupeleka huduma bora katika maeneo yao, mabadiliko ya kwenye kwenye mfumo wetu wa elimu yatachangiwa na wazazi wenyewe, bila wananchi kuona kwamba tuna dhamana ya kusimamia elimu na tukategemea tu maafisa ya serikali, nchi itaangamia, vipaumbele vya watumishi wa umma vinajulikana ni maslahi yao, ndio maana pamoja na shule kuwa na hali mbaya kama hivi lakini Mkurugenzi wa halmashauri na mkuu wa wilaya lazima watakuwa na V8 na zinajaa mafuta kila mwezi tena kwa matumizi yasiyo na tija au matumizi binafsi. Shule ya msingi Galigali kuna changamoto nyingi kadiri ya taarifa ya uongozi wa shule Jumla ya Watoto wapo 656 na walimu ni  6 tu. Pia  kuna uhaba mkubwa wa madawati watoto kukaa sakafuni ilihali shule yenyewe Ina msitu wa miti ya kutosha. https://twitter.com/lifeofmshaba/status/1627567114964828160?s=20  Tarehe 17 Februari 2023 Madiwani wa halmashauri ya jiji la Mwanza waliiomba serikali itatue changamoto ya upungufu wa madawati, matundu ya vyoo pamoja na madarasa kwa shule za msingi zilizopo katika halmashauri huyo. Diwani wa kata ya Isamilo Charles Nyamasiriri amesema katika shule ya msingi Makongoro kuna matundu sita ya vyoo ambayo hadi sasa hayajaisha wanafunzi wanapata shida ya kujisaidia huku diwani wa kata ya Igoma Musa Ngolo akisema katika shule ya msingi Mandela bado wanafunzi wanakaa chini hakuna madawati.  https://drive.google.com/file/d/1s2BQP5r9HviRBfUoGA4u2Ok3tuVhP3h8/view?usp=share_link #ChangeTanzania  #WenyeNchiWananchi

Read More Download Document

Tozo Kwa Abiria Na Watumiaji Wa Kituo Cha Mabasi Cha Magufuli.

Moja ya mapato ya Halmashauri au majiji ni tozo kwenye stand za mabasi, tozo ziko za aina nyingi sana, moja ni tozo wanayotozwa abiria wenyewe ticket kuingia kupanda bus, lakini tozo kwa watu wanaosindikiza abiria, na tozo kwa mabus kuingia kwenye stand hizo na tozo kwa wafanyabiashara kwenye eneo la stand. Hakuna maswali kuhusu tozo za mabasi na wafanyabiashara na pia watu wanaosindikiza abiria, lakini cha ajabu ni TOZO ya mabus na pia kwa abiria, bus limelipa tozo na abiria amelipa tozo hii ni kodi mara mbili kwa abiria, lakini pia nauli aliyotumia abiria tayari kuna tozo au kodi za serikali, hizi ndio zile wataalamu wanasema kodi za kivuli, unategeshea kodi kwenye huduma fulani kutokana na kushindwa kubuni vyanzo vingine vya mapato. Kibaya zaidi TOZO hizi na kodi sio kwa ajili ya maendeleo ya Stand husika, nyingi zinakwenda kutumika kwenye Halmashauri kwa mambo mengine kabisa ikiwemo vikao na safari, na kuacha stand hizi za mabasi zikichakaa, kuwa na huduma mbaya za choo na parking zenye mashimo kwa mabus, lazima mambo mawili yabadilike, moja ni TOZO zote za stand zitumike kwa ajili ya maendeleo ya stand hizo , kutoa huduma ya vyoo na ulinzi, kuboresha hali ya nishati kwenye stand zetu , kwa maana hiyo ndio maana tunasema;   MFUMO MPYA WA KUINGIA STENDI YA MAGUFULI UNANYONYA WANANCHI. Jumatatu, February 20, 2023 Manispaa ya Ubungo, ilianzisha utaratibu mpya wa kuingia na kadi katika stendi ya kimataifa ya mabasi ya Magufuli wakisema nia na madhumuni ni kudhibiti upotevu wa mapato kwa abiria wanaoingia katika kituo hicho kilichopo Mbezi Luis. Hakuna hatuna pingamizi na kuanzishwa mfumo wa kadi kwenye malipo, lakini hoja ni fedha hizi zinakwenda wapi? Kuna uwazi kwenye matumizi ya fedha hizi? Hata hivyo mfumo huu umekosolewa vikali na wananchi mbalimbali kwa kuwa inaonekana kama serikali haikujiandaa kuingia kwenye mfumo huu lakini pia suala la abiria wenye tiketi kulipa ushuru wa kuingia stendi limepingwa vikali na wananchi mbalimbali kwani tiketi hizo tayari zimeshakatwa tozo katika mabasi yanayosafiri kwenda mikoa mbalimbali.  Ticket za mabasi zilitakiwa kuwa na code maalumu ambayo abiria atatumia ili kuingia kwenye standard, au kila Ticket iwe na punguzo sana na tozo za kuingia kwenye stand hizo ili kupunguza mzigo kwa abiria.  Mawakala wa mabasi pia wamelalamikia utaratibu huo huku wakiomba wapewe vitambulisho maalum vitakavyowaruhusu kulipia mara moja kwani mfumo uliopo unawafanya walipe pesa kila watakapoingia kila wakati hivyo wanajikuta wanatumia pesa nyingi. https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/mawakala-walia-na-kadi-za-kuingia-stendi-ya-magufuli-4131792  MFUMO WA N-CARD BADO UNA CHANGAMOTO SANA Mfumo huu wa N-Card umekuja kuumiza pia abiria wengi kuchelewa safari zao na kuachwa na mabasi kwani zipo mashine licha ya upya wake zimekuwa zikisumbua yaani hazifanyi kazi kwa wakati fulani. Hata hivyo madereva wameendelea kulalamika kwamba hata mabasi yanachelewa sana kutoka katika muda husika kutokana na mfumo huo wa N-Card.  https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/mfumo-mpya-kuingia-stendi-ya-magufuli-walalamikiwa-kuchelewesha-abiria-4133038 Lakini pia hata wanaoutumia mfumo wa N-Card kupitia kivuko cha kigamboni una changamoto kubwa hasa mashine kushindwa kufanya kazi na kusababisha wananchi kuchelewa katika shughuli zao. Ni vyema serikali ingeangalia upya uwekaji wa mfumo huu, Kwanza kuwaondoa abiria ambao tayari wamekata tiketi zao ili kuepuka kulipa ushuru mara mbi kwani mabasi yanatoa ushuru huo na kila tiketi inakatwa Tozo na serikali. Pia serikali inapawa kuboresha mifumo hiyo ya N-Card ili kusiwe na usumbufu wa kuharibika haribika kila wakati, Na mwisho mawakala wa mabasi watengenezewe vitambulisho maalumu ambavyo vitawasaidia kulipa mara moja pale wanapoingia ili kuepusha gharama ya wao kulipia kila wanapoingia ndani ya stendi ya mabasi ya Magufuli. #ChangeTanzania

Read More Download Document

Ubadhilifu ukarabati Kivuko cha Kigamboni.

Tarehe 9 January 2023 Kivuko cha MV. KAZI kilirejea eneo la Magogoni Kigamboni kwa ajili ya kutoa huduma baada ya kukamilika kwa ukarabati wake uliogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 4.4 za Kitanzania,  Kivuko cha MV. KAZI kiliondolewa kwenye maji baada ya kufikia muda wake wa ukarabati mkubwa na kuanza rasmi kukarabatiwa mwezi Juni mwaka 2022 na mkandarasi Songoro Marine Transport Boatyard katika Yadi yake iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Ikumbukwe kivuko cha MV. KAZI Ujenzi wake umegharimu Shilingi Bilioni 7.3. Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA)Tarehe 19 Februari 2023 imesaini mkataba wa ukarabati wa kivuko cha MV. MAGOGONI wenye thamani ya shilingi Bilioni 7.5.  https://mwanzotv.com/2023/02/16/bilioni-7-kutumika-kukarabati-kivuko-cha-mv-magogoni/ Mkataba huo umesainiwa katika eneo la kivuko cha Magogoni Kigamboni jijini Dar es Salaam kati ya Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Lazaro Kilahala na Mkandarasi African Marine and General Engineering Company Ltd ya  Mombasa nchini Kenya. MV Magogoni kilinunuliwa kwa Euro 5,287,800 Sawa na Tsh 9.3 billion Mwaka 2008.  https://www.temesa.go.tz/news/7-5-billion-set-for-mv-magogoni-ferry-rehabilitation  hivyo kuibua maswali mengi inakuwaje MV Magogoni inakarabatiwa kwa gharama sawa na manunuzi yake, TEMESA wanasema gharama za ukarabati wa MV Magogoni ni pamoja na kununua ingini 5, Kivuko hicho kinatumia ingini 4 wanasema kwamba ingini ya 5 itakuwa kama akiba kama moja ya hizo nne italeta matatizo, lakini hakuna ufafanuzi kwamba mchakato wa kubadilisha injini ni mwepesi kwa kiasi gani, na kama mchakato huo wa kubadilisha ingine ni rahisi hapo inaibua swali kwa nini wanapeleka kivuko Mombasa kwa kazi hiyo hiyo? Tunauliza hivyo kwa sababu kuna faida gani ya kununua injini ya akiba kama huwezi wa kuzibadilisha injini hizo tumepeleka kivuko Mombasa kufanyiwa kazi hiyo, kazi ya kubadilisha nchi inachukuwa 75% ya kazi yote inayogharimu billion 7.5Suala la pili linaloleta utata kuhusu kununu injini 5 badala ya 4, ni je injini zote 4 za sasa zinazosukuma kivuko hicho mpaka Mombasa hazifai tena kwa kutumia kwa miaka 14 tu? Ni sahihi kusema injini za vivuko zinadumu kwa miaka 14 kisha kuondolewa na kutupwa? TEMESA wanaweza kufafanua kuhusu injini za zamani wanakwenda kufanyia kazi gani? TEMESA pia wameongelea masuala kama mfumo wa umeme na mabadiliko ya mfumo wa uokoaji kwamba wananunua mfumo mpya kutoka India, je ni kweli hatuna mafundi ndani ya TEMESA wenye uwezo wa kufanya kazi hiyo? Kazi zote ambazo wametoa kwa wakandarasi zisingeweza kufanyika ndani ya TEMESA au nchini kwa bei nafuu na kwa ufanisi? Lakini pia muuzaji wa injini 5 asingeweza kuzifunga yeye mwenyewe kwa bei nafuu zaidi kutokana na injini kununuliwa kwa bei kubwa na nyingi kwa wakati mmoja? Wananchi walio wengi wamehoji dhana ya ufisadi kushamiri nchini na kwamba haiwezi kuondoka kirahisi kutokana na masuala yenye harufu ya ubadhilifu yanayofanywa na maafisi wa  serikali ambayo kwa sasa kwa asilimia 99% ni serikali ya  CCM sababu Bunge kama chombo cha usimamizi limefulika wabunge wa chama hicho.  Wananchi Walio wengi wamejiuliza ni kwa nini ukarabati unafanyika Kenya , Je nchini hakuna kampuni zenye uwezo wa  kufanya shughuli hizo? Tanzania tumezungukwa na bahari, maziwa na mito mikubwa kuliko Kenya, inawezekanaje Kenya kuwa na Kampuni zenye ubora kuliko sisi ambazo kuna eneo kubwa lenye fukwe zinazotumika kwa usafiri?Mbunge wa Kigamboni Dkt Faustine Ndugulile (Mb) aliliomba Bunge kupitisha azimio la kubinafsisha huduma za vivuko nchini.  Dkt Ndugulile alisisitiza kwamba nchini kuna taasisi  zenye uwezo wa kukarabati na kujenga meli ndogo ndogo. Hivyo, kufanya ukarabati wa MV Magogoni nje ya nchi, utapelekea kufanya malipo kwa fedha za kigeni na kuathiri ajira ambazo zingetumika kwenye ukarabati huo.  Wananchi ambao ndio walipa kodi pamoja na tozo mbalimbali hawakutamani kusikia kuwa Serikali inataka kukarabati kivuko cha Mv. Magogoni kwa bil.7. wakati bei ya kuunda kivuko kipya ni kati ya bil.8.5 - 9, Kwanini kisingenunuliwa kivuko kipya ambacho kitakuwa bora zaidi ya hiko na kuipatia tenda kampuni ambayo ni mzawa kutengeneza Kivuko hiko kwa wakati huu?  #ChangeTanzania 

Read More Download Document

Mifumo Ya Haki Na Sheria Katika Nchi Yetu.

Tanzania tumekuwa na mifumo mibovu ya Haki na Sheria ambayo kwa kiasi kikubwa ina athiri maisha na ustawi wa wananchi katika nyanja zote , Sheria nyingi tulizo nazo na mifumo ina malengo sana na wakati wa mkoloni. Watu wengi hawaelewi kwamba utawala wa sheria sio lazima uwe utawala wa haki au utawala bora, hasa kama sheria hizo zimewekwa zikiwa na malengo kandamizi au kuzuia haki kwa kundi furani katika jamii au jamii yote kwa ujumla, Sheria nyingi tulizo nazo ni kandamizi na zina ukoloni mkubwa ndani yake sababu zina asili hiyo ya ukoloni, kwa maana nyingine kilichotokea tumebadilisha tu rangi ya mkoloni..   Hivi karibuni Makamu wa Rais Dr Philip Mpango amekiri wazi kuwa mifumo ya Haki bado ni changamoto kwa kuzingatia matukio yaliyotokea siku za   karibuni kuhusu familia moja ambayo kijana wao alipotea kwa mwezi na nusu huku ndugu zake  wakikosa msaada wa polisi na baadaye  walitangaza msiba wa kijana wao ndipo  polisi wakajibu kuwa wanamshikilia kijana huyo ,wako naye hii ni baada ya makamu wa Rais kuingilia kati, je ni watu wangapi wanapotezwa au kutekwa kwa namna hii na wanapotea moja kwa moja kutokana na jeshi la polisi kuwateka na kuwafundia ndani ya kuta za magereza, huu ni sawa na uharifu mwingine, jeshi la polisi linatakiwa kufuata sheria za nchi, mfumo wa ukamataji ni pamoja na muhusika au mtuhumiwa kutoa taarifa kwa ndugu zake kueleza yuko kituo gani na amekamatwa kwa kosa gani, mtu ametekwa na jeshi la polisi mpaka inafikia hatua ndugu wanatangaza msiba ndio jeshi lijitokeze kusema liko naye? , Je kwa nini mifumo hii ina ujasiri wa kwenda kinyume na sheria? Ni kwa faida ya nani? https://drive.google.com/file/d/1CHBYBeqFDmBFTcgcEFJSy95TuwIHRhQy/view?usp=share_link Jeshi la polisi pia mifumo yake ya utendaji kazi ina mianya inayoruhusu Haki za wananchi kupokwa, Tumesikia  Rais  anasisitiza kuwepo kwa uvunjivu wa haki za binadamu katika jeshi hilo akasema  "Tunataka mifumo yetu isomane, kwamba mtu akikamatwa na jeshi la polisi kisha akitoa maelezo, hayo maelezo DPP ayaone kwake moja kwa moja. Polisi asipate muda wa kuibadilisha, au mtu anawekewa kirungu anaambiwa asaini hapa, tuangalie hilo"- Rais Samia Suluhu  https://drive.google.com/file/d/1jx7TwwxNluFqvTfUBehkzkJt_Ipd9QLP/view?usp=share_linkLakini swali kubwa linakuja kama Rais naye analalamika kama sisi ni nani atatanzua mifumo hii? Japo ni Rais huyo huyo pia anapinga pinga mchakato wa wananchi kupata #KatibaMpya , Je Rais ana nia ya kweli kuboresha mifumo? Dhamani ya dhati inapimwa vipi kama kauli zinabishana? #KatibaMpya ingeweza kuwa zana nzuri kwa Rais kuweka sawa haya anayolalamikia kama sisi tunavyolalamika, tupate #KatibaMpya kuondokana na huu ukatili wa jeshi la polisi, Kukataa mchakato wa katiba ni sawa na kunufaika na hali ya ukatili wa jeshi hilo, huwezi kataa upatikanaji wa sheria bora bila kuwa mnufaika wa mfumo wa sasa. Kwa hali ya sasa Taasisi nyingi za serikali  zimekosa imani ya wananchi na kutokana na tuhuma mbalimbali ikiwemo kukosa  uadilifu kazi. Mfano Rais alisema akiwa ikulu katika kuzindua Taasisi za mifumo ya haki, Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kuna tuhuma za baadhi ya Maafisa kuwategeshea dawa za kulevya Watu wasiokuwa na hatia na kisha kujifanya wanaenda kuwakamata na kuwabambikia kesi. https://www.youtube.com/live/ut0G7jOwoa4?feature=share Hivyo mifumo ya utoaji Haki iliyopo mingi inakinzana na sheria na inapelekea uvunjivu mkubwa wa Haki za Binadamu nchini. MAPENDEKEZO; Kupatikana kwa #KatibaMpya ambayo kwanza itaweka mgawanyo wa madaraka ambao utafanyika kivitendo zaidi kuliko kuainishwa tu  kwenye katiba kama ilivyo ya sasa ambapo katiba hiyohiyo inaipa nguvu mamlaka nyingine kuingilia madaraka ya Taasisi nyingine. Mfano katika mhimili wetu wa serikali uningilia sana na mahakama, kama Rais kuteua Majaji hii inaua sana utendaji kazi huru kwa kuwa Jaji anaweza kufanya kazi yake kwa upendeleo au kwa maagizo ya aliyemteua kwa kuhofia kutenguliwa kama akienda kinyume. kuwepo na sheria itayoibana mifumo yote ya Taasisi zinazotoa Haki zote kwa ajili ya uwajibikaji na uadilifu katika utoaji Haki na utendaji kazi. Iundwe tume huru ambayo wananchi wataweza kwenda kutoa malalamiko yao moja kwa moja  au wengine kuwawakilisha kwa vitu kama haki zao zitakandamizwa na serikali au mtu mwingine yoyote. Taasisi kama jeshi la polisi kufungwe CCTV CAMERA pamoja na polisi kufungwa kamera mabegani au kwenye kofia zao wanapokuwa kwenye kazi nje ya kituo  kwa ajili ya kuzuia matumizi ya nguvu na mateso kwa watuhumiwa ili kuwe na usawa katika utoaji haki na ushughulikiaji wa watuhumiwa kabla ya kufikishwa mahakamani na pia kuwe na mifumo ya kijitali katika kutunza kumbukumbu mara tu mtuhumiwa anapokamatwa ili kuepusha tatizo la watuhumiwa kupotelea mikononi kwa polisi.  Serikali kupitia #KatibaMpya ilete mfumo ambao utalenga kuimarisha uwajibikaji wa kidemokrasia (uwajibikaji wa kijamii na kisiasa kwa pamoja) katika utoaji wa huduma katika demokrasia zinazoibukia na demokrasia zilizokomaa. Kwa vile demokrasia hasa inahusu udhibiti wa wengi juu ya kufanya maamuzi na usawa wa kisiasa, serikali iandae mbinu itayoruhusu mchakato mpana na shirikishi wa tathmini unaoendeshwa na kumilikiwa na wananchi Mfumo wa uwajibishaji pia ni muhimu sana kwa kuwa kuwawajibisha maafisa wa serikali ni kitovu cha Demokrasia. Uwajibikaji wa kidemokrasia unawapa wananchi na wawakilishi wao nafasi na njia ya kutoa maoni yao na kupatiwa maelezo kuhusu utendaji kazi wa maafisa wa kuchaguliwa na wale wasio wa kuchaguliwa, na inapobidi wanashauri hatua za kuchukua kwa maafisa walioshindwa kutekeleza majukumu yao. Mabadiliko ya katiba yataweza kusaidia mifumo ya utoaji haki kuongeza uwajibikaji katika utendaji wake kwa kuwa uwajibikaji unapima kiwango ambacho Taasisi hizo katika kuelezea na kuhalalisha maamuzi yake kwa umma. Ufanisi mkubwa wa uwajibikaji unaainishwa kwa namna ambavyo wadai haki wanaelezea mahitaji yao, lakini pia unahusiana na nafasi, uwezo na utayari wa maafisa kuwajibika kwa matendo yao. Ili kuhakikisha mifumo ya haki na sheria inafanya kazi kwa ufanisi inatakiwa kuwa na usikivu, utekelezaji, uwazi na  ushirikishi katika shughuli zake zote na vyote hivyo vitaletwa na #KatibaMpya . #KatibaMpya #ChangeTanzania

Read More Download Document

Baadhi Hawajaripoti Kazini Katika Teuzi Za Ukuu Wa Wilaya.

Teuzi za  wakuu wa wilaya zilizofanywa na Rais hii ikitokana na  mamlaka yaliyopo kwenye Katiba ya Jamhuri wa Tanzania 1977, Tanzania ina jumla ya wilaya 139, Katika uteuzi uliofanyika hivi karibuni wanawake 42 waliteuliwa na wanaume 97, asilimia kubwa ya wakuu wa wilaya wakibaki kwenye vituo vyao na baadhi kubalidilishwa vituo, ni asilimia 26% tu ndio wakuu wa wilaya wapya walioteuliwa kinyume kabisa na matalajio ya wengi hasa kwa hoja iliyokuwa imeenza kwenye halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi kwamba wanakwenda kufanya mabadiliko makubwa ilikupata timu inayoenda na mabadiliko, lakini tunaona 26% ndio mabadiliko na wengine wakiwa wale wale, katika hiyo asilimia 26% ya walioteuliwa wengi ni vijana wa chama waliokosa nafasi za ubunge au viongozi UVCCM.  Suala ambalo lilikuwa ni la kushtua kidogo ni namna ambayo Rais alifanya mapinduzi ya uongozi wa juu wa CWT kwa kuwasukuma viongozi wote kwenye teuzi ya ukuu wa wilaya, kitu tunachokiona sasa ni kwamba viongozi hao wa CWT hawakuwa wamehusishwa kwenye mchakato wa kuteuliwa kwao, ni waziri serikali inataka waondoka katika nafasi zao za CWT kwa njia ya mapinduzi kwa kutumia ujanja wa UTEUZI? Kuna wakati Teuzi zimekuwa zikitumiaka kama rushwa au namna ya kunyamazisha watu ambao serikali inaogopa sauti zao kutokana na misimamo yao kwa umma,Lakini katika TEUZI hizi za wakuu wa wilaya hivi karibuni tumeona baadhi ya watu waliokuwa wamepewa TEUZI kimkakati wakishindwa kutokea kwenye tukio la KIAPO, Kutoapishwa kwa wakuu wa wilaya hao kumekuja na maswali mengi, lakini kukiwa na tukio la mmoja ya wateuliwa Japhet Maganga ambaye ni KATIBA wa CWT, kushikiliwa na polisi na kuhojiwa kwa dakika 50 huko Tanga . Wateule hasa ambao ni viongozi wa ngazi za juu wa Chama Cha Walimu Tanzania ( CWT ) walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya hawajaripoti vituo vyao vya kazi na hawajaapishwa ili kuanza majukumu yao, Rais wa CWT, Leah Ulaya pamoja na Japhet Maganga ambaye ni katibu wa chama hicho  wao wapo Tanga wakiongoza mkutano wa viongozi wakuu wa CWT. Kuna hoja nyingi zinaibuka lakini moja ikiwa ni kwamba nafasi wanazoshirikia sasa wanapokea mishahara mara mbili ya kile wanacholipwa wakuu wa wilaya, lakini hoja ya pili iliwa kwamba dhamana ya madaraka waliyonayo sasa ni kubwa sana kulinganisha na ukuu wa wilaya Hii inaibua hoja ya madai ya #KatibaMpya kutoka na hizi changamoto zinazoibuka kwenye teuzi, uteuzi unaonekana kutozingatia sifa ya mtu na utayari wa kufanyakazi husika, hii inapelekea viongozi kukosa ufanisi au kwenda kutumia maliasili za umma vibaya na ubadhirifu, ni wajibu wa mamlaka za uteuzi kuzingatia hadhi ya sifa ya mtu na nafasi yake, lakini pia kabla ya mtu kutangazwa ameteuliwa ni muhimu akashirikishwa kwenye mchakato ili awe na utayari ya kuchukua nafasi husika au kukataa, Kwenye #KatibaMpya nafasi hizi za uteuzi wananchi wanapendekeza watu wagombee, lakini pia nafasi zisizo na tija ziongoleweLakini pia kubwa na linazozua mashaka ni hili la  mahojiano kati yao na polisi na maafisa wa upelelezi na Japhet ? kulikuwa na ulazima gani wa kumhoji Japhet kama yeye hana nia ya kuchukua nafasi ya Ukuu wa wilaya? Mahojiano ya dakika 50 yalihusu nini hasa kwenye uteuzi wa Japhet?  Japhet alipohojiwa na waaandishi wa habari “kwa sasa nimeziba mdomo labda usubiri tutakapomaliza kikao ndipo nitazungumza kuhusu nafasi ya U-DC na CWT." Pia Rais wa chama Bi Leah Ulaya hakutoka kuongea chochote na pia maofisa wa chama hicho hawakuruhusiwa kuongea na chombo chochote cha habari. https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/dc-mteule-ahojiwa-na-polisi-dakika-50-rais-cwt--4104640 Katika kikao kinachohisiwa kuwa cha siri au kisicho rasmi Rais wa chama cha walimu amesikika akisema kuwa chama hicho kipo kwa kuwa wenye nchi wametaka kiwepo na sio walimu kama inavyotarajiwa, hivyo anajaribu kueleza kuna ubabe wa aina fulani unaendelea serikalini, hii ina maana anasihi Tanzania tunatakiwa kuwa na Taasisi huru kama Taasisi bila kufungana na chama chochote cha siasa. https://drive.google.com/file/d/1JBv_dtc_LiH3RotEHqjLQcLDVnARMq0u/view?usp=sharing Je hii inajaribu kuashiria kuwa hawako tayari kutumikia wananchi au kuna kitu wanakwepa ambacho wanahisi kitawagharimu baadaye?  Je hii inaweza ikahusishwa na maslahi yao hasa ya kifedha? Je inawezekana kuwa ilikuwa ni namna ya kuwatoa madarakani CWT ili wengine wapate nafasi hizo pia?  Jambo la kukataa teuzi limeibua mijadala mingi mitandaoni na kwa wananchi walio wengi wao wakijiuliza maswali ,Tanzania hakuna haki za kiuchumi , #UhuruWaKujieleza, uhuru kamili  mtu kuchagua ni kazi gani anataka kufanya? Kuna nini kinaendelea CWT kiasi cha kushambuliwa hivi kwa kutumia uteuzi . Mjadala mkubwa kuhusu Jambo hili pia linahusishwa na mambo ya kimaslahi zaidi katika suala zima la mishahara kati ya nafasi hizo mbili yaani ukuu wa wilaya na Ukatibu au Urais wa Chama Cha Walimu huku inakadiriwa mshahara wa ukuu wa wilaya ni Tsh million tatu pamoja na marupurupu mengine na ukatibu wa chama hicho unasemekana kuwa ni shillingi  7.8 pia kuna marupurupu mengi ambayo wanaona ni bora kubaki katika nafasi zao. Kitu ambacho wananchi wengi wanasema hata wao wangechukua maamuzi ya kukataa nafasi hizo za ukuu wa wilaya. Lakini pia nafasi hizi za Ukuu wa wilaya zinachukuliwa kama nafasi za makada wa chama, hivyo kuondoa kuaminika kwa viongozi au kwamba muda wote walikuwa wanafanya kazi za chama. . Yote hayo yanatokea lakini ukitafuta chimbuko la kadhia yote hiyo ni ukosefu wa katiba bora ambayo watu hawa kama wakuu wa wilaya wanachaguliwa na kutenguliwa na Rais na na sio kuchaguliwa na wananchi. Ingefaa zaidi wananchi kuchagua mtu ambaye wanamuona anafaa kuwatumikia kulingana na vipaumbele vyao. Ni muhimu Rais apunguziwe madaraka ili kuweka utawala bora. #KatibaMpya  #ChangeTanzania

Read More Download Document

 Madaraka Ya Rais Yapunguzwe Katika Suala La Teuzi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana madaraka makubwa hasa katika uteuzi ambayo yanapelekea kukwamisha uwajibikaji na utendaji kwa manufaa ya wananchi. Suala la madaraka na majukumu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, limezua mvutano katika baadhi ya kamati za Bunge Maalum la Katiba na kusababisha kuziweka kiporo ibara za 72 na 73 za sura ya saba ili kutoa fursa kwa wajumbe kutafakari zaidi. Mojawapo ya ibara hizo ni ile inayohusu madaraka ya Rais katika uteuzi wa viongozi wa umma, ambayo akitaka anaweza kuchagua hata marafiki zake katika nafasi anazohitaji. Lakini pia hivi sasa tumeona Rais anaweza kuteua watu ili awaondoe katika nafasi fulani kwa malengo maalum, kama ambavyo tumemsikia mwenyekiti wa CWT Bi, Leila Ulaya https://drive.google.com/file/d/1a8P4lEDiRVhaC_aLNFZxJpYTyrRvRyzc/view?usp=share_link  Rais anahitaji kupunguziwa madaraka kwa sababu; Kumpunguzia madaraka ina maana ya kumwekea mipaka ya kazi yake na vyombo vya check and balance. Kumpunguzia madaraka ni kwa lengo la kuwa na serikali inayozingatia katiba, kufanya kazi kwa ushirikiano na vyombo vingine huku kila kimoja kikiwa watch dog ya kingine. Kuwe na check and balance. Ni katika hiyo check and balance ndipo Rais atakapolazimika kuteua watendaji ambao baada ya kuthibitishwa si wake tena, watawajibika sehemu nyingine. Hii itatoa nafasi za umakini katika kupata viongozi na kumpa Rais ''unafuu'' wa kuwaondoa kwani yeye hatahusika tena. Hebu fikiria yanayotokea hivi sasa ya watu kugomea teuzi. Lakini pia kumpunguzia madaraka kunalenga kuongeza ufanisi kwa Rais kwa kumpunguzia kazi zisizo za lazima na zingine zinazomtia katika kashfa. Kwanini Rais wa nchi kubwa kama Tanzania ahangaike na uteuzi wa wakurugenzi wa miji au bodi za mashirika na vyuo? Kwa ufupi kumpunguzia madaraka Rais haina maana ya kumyang'anya nguvu za kiutawala bali kumpa nguvu za kiutawala kwa kuzingatia, sheria, taratibu na maadili. Ni kumpa uwezo wa kufanya mambo ya kitaifa zaidi, kumwepusha na migongano isiyo ya lazima na vyombo vingine hata wananchi. https://drive.google.com/file/d/1a8P4lEDiRVhaC_aLNFZxJpYTyrRvRyzc/view?usp=share_link Ni njia ya kumpa nafasi ya kuiangalia nchi kwa ujumla wake na kusimamia majukumu yake.  Kupunguziwa madaraka kutazuia ''office abuse'' na kumfanya afikirie kwa umakini kila jambo linalogusa wananchi, rasilimali na usalama wao kila sekunde na dakika. Hatuhitaji kiongozi tunahitaji uongozi na uongozi ambao hautengenezwi na jeshi la mtu mmoja bali collective responsibility ya kila mmoja wetu katika nafasi yake. Kuna nafasi zilipaswa kuwa za kitaaluma zaidi kuliko uteuzi, hivi karibuni tumeshuhudia wakuu wa wilaya wakiteuliwa wengi wakiwa ni makada wa CCM, hivyo ni wazi kuwa wanaenda kuwa watekelezaji wa maagizo ya Rais kuliko kuwatumikia wananchi . Muhimu ni Rais atambue kuwa yeye ni mtumishi namba moja wa umma na wala si mtumikiwa namba moja.  #ChangeTanzania

Read More Download Document

Mgogoro Wa Ardhi Mbarali Mbeya

Serikali ya awamu ya sita chini ya  Rais Samia imeendelea kutekeleza  uonevu mkubwa na uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu katika suala zima la umiliki wa ardhi ( Haki ya kiuchumi)  katika maeneo mbalimbali nchini,  Matukio yalianza huko Arusha eneo la Loliondo na Ngorongoro, kisha kutapakaa kwa kasi maeneno mbalimbali ya nchi, jamii ya Maasai walianza kushughulikiwa  Mapema mwaka 2022. January 2023, huko mkoani Mbeya,   Mkuu wa mkoa wa Mbeya ametoa taarifa kwa vyombo vya habari akiwa na anapiga marufuku maeneo ambayo chanzo cha mgogoro huu ni upanuzi wa Hifadhi ya Ruaha na kuweka mipaka mwaka 2001. Maeneo hayo yote  yalikuwa yakitumika na wakazi wa mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kilimo. yakijumuisha Eneo la Mnazi , na Madibira Phase 2 ambayo yalikuwa yakitumika kwa shughuli za kilimo ambazo ndizo hutegemewa na wakazi wa Jiji la Mbeya kama nguzo yao ya uchumi. Lakini Mkuu huyo wa mkoa wa Mbeya alisema yapo maeneo matano 5 ambayo serikali imepiga marufuku kutokana na huruma ya Rais, Wananchi wameachiwa wafanye kilimo kwa wakati huu mpaka mwezi  April 2023 maeneo hayo ni  (LUHANGA, IYALA, KILAMBO , MSANGA)  Wananchi wamepewa notice mpaka mwezi wa nne wahakikishe wameondoka na kuacha kuyatumia na serikali imekiri kwamba imeweka mipaka tayari. Ikumbukwe mwishoni mwa mwaka 2022 serikali kupitia Baraza la Mawaziri ilifuta vijiji vyote vitano vya Kata ya Luhanga na vitongoji 47 kutokana na uharibifu wa mazingira pasipo kusikiliza maoni ya wananchi na kuwashirikisha katika uamuzi huo, ujumla eneo la kilimo linaloathirika ni hekta 14 ambalo ni kubwa na litaathiri watu zaidi ya 40,000 wanaojihusisha na kilimo. Udhaifu wa suala hilo la Rais kuchukua haki za watu za kumiliki ardhi inatokana na ukweli kwamba Sheria zetu za ardhi zimempatia mamlaka makubwa Rais ya kuwa msimamizi mkuu wa ardhi nchini suala ambalo Viongozi wengi hulivunja na kwenda mbali zaidi kwa kupora haki za wananchi pasipo kuwapatia stahiki zao zikiwemo fidia. https://drive.google.com/file/d/1emmOpbRzNkbTP6uVmDxctDtIPf9yoRIe/view?usp=share_link https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/serikali-yamaliza-mgogoro-wa-ardhi-bonde-la-usangu-4088848    #ChangeTanzania 

Read More Download Document

Utawala Bora Na Rushwa Ya Madaraka.

Pamoja na changamoto nyingi  tulizonazo Tanzania, kukosa huduma muhimu  maji,  umeme, huduma mbovu za afya, miundombinu isiyozingatia viwango vya usalama, tozo, na mengine mengi katika nchi yetu, Lakini tuna tatizo lingine kubwa ambalo  tumesababishiwa na watalawa kwa manufaa yao wenyewe  kukosa utawala bora ambao chanzo chake kikubwa ni vyeo vya kupeana kama shukurani, kuna wengine wanasema ni RUSHWA ( fursa, fedha na madaraka)  iliyokithiri na inayoendekezwa na watawala. Dhana ya Utawala Bora ina nguzo kuu sita Katiba ya kidemokrasia;   Ulinzi, ukuzaji na uzingatiaji wa haki za binadamu; Mgawanyo wa Madaraka;   Uhuru wa Mahakama;   Uhuru wa habari na  Uhuru wa vyombo vya habari. Kati ya vitu ambavyo utawala wa Tanzania unakosa ni utendaji wa ukamilifu wa vitu vyote tajwa hapo juu hasa kiutendaji zaidi, kwa kuwa serikali ya CCM imekuwa ikifanya na kuamua mambo yake kibabe pengine bila hata ridhaa ya wananchi. Lakini pia serikali ya CCM imekuwa ikichezea chaguzi, kumekuwa na matukio ya fujo na wizi wa kura wa waziwazi wakati wa chaguzi, wapinzani wamekuwa wakiondolewa kwenye mchakato kwa nji za fitina, lakini wagombea wote wa chama cha mapinduzi wamekuwa wakipitishwa na Tume ya Uchaguzi kugombea bila makosa kwenye fomu, lakini pia tumeona baada ya wagombea wa CCM wakipewa majimbo na TUME ya UCHAGUZI kwa hoja ya kupita bila kupingwa !!! lakini hii yote inatokana na mikakati ya Tume ya Uchaguzi kudondosha kimkakati wagombea kutoka vyama vya upinzani  Katiba yetu ya Tanzania ya 1977 imempa madaraka makubwa Rais ikiwemo nguvu kubwa na nafasi nyingi za teuzi katika nafasi mbalimbali za uongozi kama mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi, makatibu na wengine wengi. Hii ni hatari kwa kuwa mamlaka yanatoka kwa Rias na sio wananchi ambao wataongozwa na viongozi hao, matokeo yake viongozi hao watakuwa wanafanya kumfurahisha Rais ili wapate teuzi na sio kuwatumikia wanachi kama inavyotakiwa. Hivi karibuni Rais ameteua, ametengua na kubadilisha vituo vya kazi kwa wakuu wa wilaya mabalimbali na huku wengine wakibaki katika vituo vyao vya kazi wengine wakibadilishwa vituo ni 26% ya walioteuliwa hii ni idadi ndogo sana kuleta mabadiliko. Katika hali isiyo ya kawaida ambayo ina viashiria vya rushwa ya madaraka na upendeleo tumeona kuwa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) viongozi wake wote wamepewa vyeo hii ina maana gani kwa taasisi hiyo yenye watumishi wengi wa umma? Hii sio namna ya kudhohofisha juhudi ya kuwa na taasisi imara ili kuweka mwanya wa kusubiria teuzi? Kwamba viongozi watakao kuwa kwenye taasisi hiyo wakumbuke kwamba Rais anaangalia hiyo taasisi na ukiwa rafiki kwa serikali yake utapata uteuzi? Huu sio mgongano wa maslahi? , Katika teuzi hizi  Rais wa CWT  Leah Ulaya kateuliwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Mbogwe, Makamu wa Rais wa CWT Dinah Mathani kateuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Uvinza na katibu wa chama hicho Bw Japhet Maganga ateuliwa kuwa mkuu wa Wilaya Kyerwa, Hii inaibua swali kubwa sana kuhusu rushwa ya madaraka.  Hii ina maana gani kwa viongozi wote wa ngazi za juu kuteuliwa kutoka kwenye chama hicho na kupata nafasi hizo? Suala hilo la teuzi hizo za CWT halijatokea kwa bahati mbaya, Moja ya tuhuma ambazo Serikali ya CCM inazo kwa muda mrefu ni kudhibiti uchaguzi huru na wa haki, na kundi kubwa linalotumika kufanya hivyo ni kundi la walimu pamoja na Jeshi la Polisi na yeyote atakayeipa CCM ushindi mnono basi hulambishwa asali kwa kupewa madaraka na nafasi za uongozi, Lakini pia CWT ina idadi kubwa ya watumishi wa umma, wana suala mengi wanayoidai serikali, kukiwa na viongozi ambao wanasubiria teuzi inasaidia sana kupooza maslahi ya wanachama wa CWT, chama iki kinapodhohofisha watawala wanapata manufaa zaidi maana yanayozimwa ni maslahi ya walimu yaani kundi kubwa la watumishi wa umma, Serikali imefanya juhudi kubwa sana kuteka Taasisi za Dini, NGOs, na vyama vya siasa kupitia sheria mbalimbali, hata Tanganyika law Society ( TLS) na chama cha madaktari Tanzania , kinaongozwa na makada wa CCM Huu umekuwa ni mtindo uliozoeleka wa kudhohofisha Taasisi ambazo zinasimamia maslahi ya wannachi wake, na serikali haina mpango wa kushughulikia changamoto zozote zile hivyo inachofanya ni kuvuruga wa uongozi wa hizo taasisi kwa kuweka mapandikizi kwenye hizo taasisi, lakini pia tunajua malalamiko mengi sana kuhusu BAKWATA sasa tunaona vyama vingine vinaingiliwa kwa kasi sana, hili la  sasa  Serikali ya chama tawala kutoa  vyeo kwa mtu ambaye ameshawahi kuvifanya kwa manufaa ya umma  kuendelea kuwepo madarakani,  Rais hateui viongozi hao kwa kuwa wana sifa na vigezo vya cheo husika. Kimsingi jambo hili ndio linachangia kwa kiasi kikubwa kuendelea kukiweka chama tawala madarakani, hii ni mojawapo ya rushwa ambayo inaisumbua nchi kwa kuwa tunazidi kuwa na utawala mbovu kila kukicha. Ili kuwe na utawala bora na kuepuka kadhia za utawala mbovu ulio na rushwa ndani yake ushiriki wa wananchi ni suala muhimu na la msingi sana katika kuchagua viongozi wao na  kujiletea maendeleo yao katika nchi. Mahali ambapo wananchi hawashiriki wala hawashirikishwi kunakuwa na lawama na mizozo mingi kwa viongozi hasa pale ambapo maamuzi yaliyopitishwa yanawaumiza wananchi ndipo tunaona umuhimu wa ukushiriki unajitokeza zaidi. Maamuzi yoyote ambayo serikali inayachukua yanatakiwa kuna msingi wa maoni ya wananchi. Mwarobaini wa matatizo yote hayo ni #KatibaMpya ambayo itapunguza madaraka na mamlaka ya Rais na kuyaweka kwa wananchi ili viongozi wawe na maadili, wasiwe juu ya sheria na wawepo madarakani kwa ridhaa ya wananchi na kuwatumikia wananchi kwa utumishi uliotukuka kwa kuhofia uwajibishwaji. #ChangeTanzania #WenyeNchiWananchi 

Read More Download Document

Utawala Bora na Rushwa Ya Madaraka.

Pamoja na changamoto nyingi  tulizonazo Tanzania, kukosa huduma muhimu  maji,  umeme, huduma mbovu za afya, miundombinu isiyozingatia viwango vya usalama, tozo, na mengine mengi katika nchi yetu, Lakini tuna tatizo lingine kubwa ambalo  tumesababishiwa na watalawa kwa manufaa yao wenyewe  kukosa utawala bora ambao chanzo chake kikubwa ni vyeo vya kupeana kama shukurani, kuna wengine wanasema ni RUSHWA ( fursa, fedha na madaraka)  iliyokithiri na inayoendekezwa na watawala. Dhana ya Utawala Bora ina nguzo kuu sita Katiba ya kidemokrasia;   Ulinzi, ukuzaji na uzingatiaji wa haki za binadamu; Mgawanyo wa Madaraka;   Uhuru wa Mahakama;   Uhuru wa habari na  Uhuru wa vyombo vya habari. Kati ya vitu ambavyo utawala wa Tanzania unakosa ni utendaji wa ukamilifu wa vitu vyote tajwa hapo juu hasa kiutendaji zaidi, kwa kuwa serikali ya CCM imekuwa ikifanya na kuamua mambo yake kibabe pengine bila hata ridhaa ya wananchi. Lakini pia serikali ya CCM imekuwa ikichezea chaguzi, kumekuwa na matukio ya fujo na wizi wa kura wa waziwazi wakati wa chaguzi, wapinzani wamekuwa wakiondolewa kwenye mchakato kwa nji za fitina, lakini wagombea wote wa chama cha mapinduzi wamekuwa wakipitishwa na Tume ya Uchaguzi kugombea bila makosa kwenye fomu, lakini pia tumeona baada ya wagombea wa CCM wakipewa majimbo na TUME ya UCHAGUZI kwa hoja ya kupita bila kupingwa !!! lakini hii yote inatokana na mikakati ya Tume ya Uchaguzi kudondosha kimkakati wagombea kutoka vyama vya upinzani  Katiba yetu ya Tanzania ya 1977 imempa madaraka makubwa Rais ikiwemo nguvu kubwa na nafasi nyingi za teuzi katika nafasi mbalimbali za uongozi kama mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi, makatibu na wengine wengi. Hii ni hatari kwa kuwa mamlaka yanatoka kwa Rias na sio wananchi ambao wataongozwa na viongozi hao, matokeo yake viongozi hao watakuwa wanafanya kumfurahisha Rais ili wapate teuzi na sio kuwatumikia wanachi kama inavyotakiwa. Hivi karibuni Rais ameteua, ametengua na kubadilisha vituo vya kazi kwa wakuu wa wilaya mabalimbali na huku wengine wakibaki katika vituo vyao vya kazi wengine wakibadilishwa vituo ni 26% ya walioteuliwa hii ni idadi ndogo sana kuleta mabadiliko. Katika hali isiyo ya kawaida ambayo ina viashiria vya rushwa ya madaraka na upendeleo tumeona kuwa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) viongozi wake wote wamepewa vyeo hii ina maana gani kwa taasisi hiyo yenye watumishi wengi wa umma? Hii sio namna ya kudhohofisha juhudi ya kuwa na taasisi imara ili kuweka mwanya wa kusubiria teuzi? Kwamba viongozi watakao kuwa kwenye taasisi hiyo wakumbuke kwamba Rais anaangalia hiyo taasisi na ukiwa rafiki kwa serikali yake utapata uteuzi? Huu sio mgongano wa maslahi? , Katika teuzi hizi  Rais wa CWT  Leah Ulaya kateuliwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Mbogwe, Makamu wa Rais wa CWT Dinah Mathani kateuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Uvinza na katibu wa chama hicho Bw Japhet Maganga ateuliwa kuwa mkuu wa Wilaya Kyerwa, Hii inaibua swali kubwa sana kuhusu rushwa ya madaraka.  Hii ina maana gani kwa viongozi wote wa ngazi za juu kuteuliwa kutoka kwenye chama hicho na kupata nafasi hizo? Suala hilo la teuzi hizo za CWT halijatokea kwa bahati mbaya, Moja ya tuhuma ambazo Serikali ya CCM inazo kwa muda mrefu ni kudhibiti uchaguzi huru na wa haki, na kundi kubwa linalotumika kufanya hivyo ni kundi la walimu pamoja na Jeshi la Polisi na yeyote atakayeipa CCM ushindi mnono basi hulambishwa asali kwa kupewa madaraka na nafasi za uongozi, Lakini pia CWT ina idadi kubwa ya watumishi wa umma, wana suala mengi wanayoidai serikali, kukiwa na viongozi ambao wanasubiria teuzi inasaidia sana kupooza maslahi ya wanachama wa CWT, chama iki kinapodhohofisha watawala wanapata manufaa zaidi maana yanayozimwa ni maslahi ya walimu yaani kundi kubwa la watumishi wa umma, Serikali imefanya juhudi kubwa sana kuteka Taasisi za Dini, NGOs, na vyama vya siasa kupitia sheria mbalimbali, hata Tanganyika law Society ( TLS) na chama cha madaktari Tanzania , kinaongozwa na makada wa CCM Huu umekuwa ni mtindo uliozoeleka wa kudhohofisha Taasisi ambazo zinasimamia maslahi ya wannachi wake, na serikali haina mpango wa kushughulikia changamoto zozote zile hivyo inachofanya ni kuvuruga wa uongozi wa hizo taasisi kwa kuweka mapandikizi kwenye hizo taasisi, lakini pia tunajua malalamiko mengi sana kuhusu BAKWATA sasa tunaona vyama vingine vinaingiliwa kwa kasi sana, hili la  sasa  Serikali ya chama tawala kutoa  vyeo kwa mtu ambaye ameshawahi kuvifanya kwa manufaa ya umma  kuendelea kuwepo madarakani,  Rais hateui viongozi hao kwa kuwa wana sifa na vigezo vya cheo husika. Kimsingi jambo hili ndio linachangia kwa kiasi kikubwa kuendelea kukiweka chama tawala madarakani, hii ni mojawapo ya rushwa ambayo inaisumbua nchi kwa kuwa tunazidi kuwa na utawala mbovu kila kukicha. Ili kuwe na utawala bora na kuepuka kadhia za utawala mbovu ulio na rushwa ndani yake ushiriki wa wananchi ni suala muhimu na la msingi sana katika kuchagua viongozi wao na  kujiletea maendeleo yao katika nchi. Mahali ambapo wananchi hawashiriki wala hawashirikishwi kunakuwa na lawama na mizozo mingi kwa viongozi hasa pale ambapo maamuzi yaliyopitishwa yanawaumiza wananchi ndipo tunaona umuhimu wa ukushiriki unajitokeza zaidi. Maamuzi yoyote ambayo serikali inayachukua yanatakiwa kuna msingi wa maoni ya wananchi. Mwarobaini wa matatizo yote hayo ni #KatibaMpya ambayo itapunguza madaraka na mamlaka ya Rais na kuyaweka kwa wananchi ili viongozi wawe na maadili, wasiwe juu ya sheria na wawepo madarakani kwa ridhaa ya wananchi na kuwatumikia wananchi kwa utumishi uliotukuka kwa kuhofia uwajibishwaji. #ChangeTanzania #WenyeNchiWananchi 

Read More Download Document

Je, Rais ameheshimu takwa la katiba kuhusu mikutano ya hadhara kwa nia ya Dhati?

Mnamo tarehe 03 mwezi Januari mwaka 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliruhusu kuendelea kwa mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa amabyo ilizuiliwa na mtangulizi wake hayati Dk John Pombe Magufuli, ikiwa ni takribani miaka 7 bila kuwepo kwa mikutano hiyo. Pamoja na katazo la Magufuli lazima tuweke kumbukumbu kwa usahihi, Rais Samia pia aliweka zuio la mikutano ya vyama vya siasa, akisema ni wakati wa kujenga nchi, kwamba hata nchi nyingine zinapomaliza chaguzi hakua mikutanao ya vyama vya siasa, suala ili sio sahihi, lakini pia ilikuwa ni uvunjifu wa Katiba ya nchi kwa sababu mikutano hiyo ni takwa la kisheria. Kuna baadhi ya wanasiasa walipata changamoto kutokana na kutotii kauli ya Rais Samia ya kuzuia mikutano ya hadhara, Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akiwa ni mmoja wao, alipokwenda Mwanza kufanya mkutano wa hadhara wa chama chake alitekwa, akapotea kwa siku kadhaa, baadaye polisi walikiri kwamba wako naye na kwenye kufanya ukaguzi nyumbani kwake baada ya siku 3, walichukuwa vifaa kadhaa na alifunguliwa kesi ya Ugaidi chini ya serikali ya Rais Samia, Rais alipoulizwa na BBC kuhusu kesi ya Mbowe alisema kweli ni gaidi na IGP pia alisema Mbowe ni gaidi unaweza kwenda kumuuliza kama ni mkristo mzuri atakuambia ukweli kuhusu ugaidi wake.Lakini, kutokana na nguvu ya umma serikali ilishindwa kuendelea na kesi ya Mbowe, Rais akajaribu kwa njia nyingi kuonyesha kwamba yeye anajali siasa za ushindani na kuunda kikosa kazi kwa hoja kwamba kitafanya mwafaka wa namna vyama vya siasa vinaweza kuruhusiwa kufanya siasa katika mazingira mazuri, Ukweli ni kwamba hii ilikuwa danganya toto, Rais Samia alikuwa anafanya juhudi kujinasua kwenye ukandamizaji wa demokrasia alioufanya.  Mwisho tumeona Rais Samia alisema “Uwepo wangu mbele yenu ni kuja kutoa ruhusa kwamba lile tangazo la kuzuia mikutano ya hadhara sasa linaondoshwa, Wanasema ni haki kwa vyama vya siasa kuendesha mikutano yao ya hadhara lakini ndugu zangu tuna wajibu. Wajibu wetu ni kuwalinda mfanye mikutano yenu kwa salama. Wajibu wenu vyama vya siasa ni kufuata sheria na kanuni zinavyosema.” – Rais Dkt Samia Suluhu Hassan https://www.youtube.com/watch?v=y-3FOjzwdzcJe Rais Samia anapata wapi mamalaka ya kuruhusu mikutano ya kisiasa? Je ili sio takwa la kikatiba? Nini kinaendelea sasa !!! Mambo yalijitokeza baada ya kuruhusiwa kwa mikuatano ya hadhara kwa vyama vya siasa bado imeacha mashaka kama kweli serikali ina nia ya dhati kuendelea kuheshimu katiba na kuvumilia siasa ya vyama vya upinzani.Kuna mambo yameibuka ambayo yanajenga mashaka sana kuhusu haki hii ya mikutano kwa vyama vya siasa, kuna dalili za ukandamizaji kwa namna au mbinu nyingine zilizoibuka,  Waziri wa habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Nape Nnauye aliwataka waandishi wa habari kuweka usawa katika uandishi wa habari za mikutano ya hadhara  ya kisiasa ikiwa ni siku chache baada ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan kuruhusu mikutano hiyo kuanza kufanyika nchini. NUKUU : “Ni matumaini yangu kwamba waandishi wa habari mtaweka usawa wa stori zitakazotokana na mikutano hiyo kwa sababu tukibeba hivi hivi tunaweza kupeleka wananchi sehemu mbaya  ambapo habari zingine zinakuwa na matusi uhuru uliotolewa utumike vizuri turekodi yale ambayo yatasaidisha nchi yetu,”  Amesema  Nape Nnauye. Kauli hii inaonekana kwa watu mbalimbali kama ni kauli ya vitisho kwa vyombo vya habari kutekeleza majukumu yao kwa uhuru zaidi. Kauli hii ni wazi sasa Serikali inashambulia mikutano ya hadhara kwa kupitia vyombo vya habari kwa namna kwamba kuna mambo wanaweza kuruhusiwa na kuna mambo hawaruhusiwi kuonyesha, lakini pia ni kama kutishia vyombo vya habari kwamba sio kila habari utakayoitoa utabaki salama kwa sababu serikali kupitia Waziri wa Habari inaonekana kutofurahi kama chombo cha habari kitarusha mikutano ya vyama vya upinzani live.  Siku chache baada ya ruhusa hiyo CHADEMA walianza mkutano wao jijini Mwanza ambapo mambo kadhaa yaliyokea ikiwemo kukamatwa kwa waandishi wa habari siku moja kabla ya mkutano wa CHADEMA,  inasemakana waandishi hao walifuatwa na polisi katika ofisi yao jijini Dar es salaam na kupelekwa kituoni, lakini pia waandishi wengine wakiwa njiani kuelekea jijini Mwanza kwa ajili ya mkutano huo wa hadhara waliibiwa vifaa vyao vya kazi ikiwemo kamera na vingine. Hii inafanya tuweze kupokea taarifa ya kuruhusiwa kwa mikuatano hiyo kwa tahadhari. Ni tumaini letu kwamba, huu ni wakati ambao wananchi wote wanapaswa kushikamana na kupigania haki zote za msingi  #ChangeTanzania #WenyeNchiWananchi

Read More Download Document

Utunzaji wa maliasili zetu.

Maliasili za Taifa ni kitu kinachopaswa kulindwa na kutunzwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi kwa manufaa ya watanzania wote. Lakini katika nchi yetu maliasili hakuna uwazi katika usimamizi wa maliasili, serikali inachukua mikopo kila siku kuendesha miradi, lakini tuna maliasili za kutosha kama zikisimamia vizuri zinaweza kufanya mambo mengi bila mikopo tunayoona kwa sasa, kwa nini kuna usiri mikataba inayohusu maliasili zetu? Nani ananufaika na maliasili hizi pale mikataba inapofichwa? Kama mambo yako safi kwa nini kunakuwa na siriKuna wakati maliasili zetu zimekuwa zikifujwa kwa manufaa ya wageni na watu wachache hasa viongozi bila kushirikisha wananchi, mfano mzuri ni migodi, imekuwa ni machungu kwa wakati wanaoishi karibu na migodi kuliko kupatiwa maendeleo, lakini pia kama Taifa hakuna kikubwa tumepata ukilinganisha na ukubwa wa mashimo tunayoachiwa, athari za mazingira tulizopata, na mbaya zaidi kuna misamaha ya kodi kwenye hizo shughuli, sehemu inapogundulika kuna madini inakuwa mateso kwa wananchi wanaoishi katika hili eneo badala ya kupata manufaa kupitia fidia au uchimbaji wa madini husika.  Lakini pia kama wananchi tuna hili la kujiuliza kuwa, kwanini tukihoji mambo kuhusu usimamiaji wa Maliasili zetu tunaonekana wabaya? Tukihoji tunajibiwa vibaya na uongo na wakati huwa tunajua nini tunachohoji, Hivyo ni wazi tujiulize bila #KatibaMpya je tutaweza kuwa na sauti kwenye maliasili zetu ama tutabaki na maliasili zisizo zetu bali za viongozi wa CCM?  Hivi karibuni tumeona ndege kubwa ya kubebea mizigo iliyoleta utata mkubwa, serikali imeshindwa kutoa vielelezo vya ushahidi wa ndege hiyo ilikuwa imekodiwa na nani, imebeba mizigo gani na ilikwenda wapi, mbaya zaidi pia serikali inasema ndege hiyo ilibeba watalii wakati ni ndege ya mizigo !!! pia uwanja wa ndege KIA kupitia KADCO wanasema ndege ilitua nchi mbalimbali za Afrika, lakini ukiangali record za ndege hiyo kwenye mifumo ya kimataifa , inaonyesha ndege hiyo ilitoka Abu Dhabi na kuja Tanzania kisha ikirudi ilikotoka bila kutua katika nchi nyingine yoyote ile  Imefikia mahali serikali inasema bila wasi kwamba watalii wanakuja nchini wakiwa wamepanda ndege za mizigo kinyume kabisa na sheria za usafiri , inawezekana vipi watalii kutoka uarabuni wanapanda ndege za mizigo halafu ndege zao zinatua kwa siri huko mbugani kusiko kuwa na Uhamiaji wala huduma yoyote zaidi ya kuchimba dawa na kuwinda wanyama  na kwanini watumie uwanja wa mbugani usiokuwa rasmi kwa wageni wanaoingia nchini?Hapa tuna maswali mengi ya kuuliza lakini hata tukihoji au kuuliza tunaambulia majibu ya uongo na yasiyo ya weledi. Kwa mfano msemaji mkuu wa serikali  @MsigwaGerson anataka kutuaminisha kwamba moja ya sababu ya watalii hao wa kiarabu kupanda ndege za mizigo ni kwa sababu wanakuja na makontena? https://twitter.com/MsigwaGerson/status/1612169272477769731?s=20&t=YX_SYt1CXTuDCtlRyik9Sw  na  hayo makontena ni ya kubebea nini? Na pia wanasema kuwa usafirishaji ulisitishwa swali ni je usafirishaji wa Wanyama umesitishwa kuanzia lini na mpaka lini urejee? Kwahiyo tukisema Wanyama wanasafirishwa hatukosei? Je 1502Km2 walizozipora wamaasai Loliondo ni ili kufanya iwe uwanja wa kuwinda na kusafirisha wanyama? Pia maswali mengine ya kujiuliza kuhusu ndege iliyotua mbugani ni haya  Tangu lini  Watalii wakapanda ndege ya mizigo?   Watalii gani hawa tusioelezwa walitoka nchi gani na ni akina nani?   Siku zote tumekuwa tukitangaziwa idadi na kwa picha..... nini kimetokea? Kwa nini ndege kubwa ya mizigo itue kwenye viwanja vya ndani ya hifadhi? Je ndege hiyo isingeonekana na wananchi serikali ingetoka kutoa taarifa juu ya ujio wake? Kwa kadri serikali inavyozidi kutoa ufafanuzi usio na tija ndivyo inavyoendelea Kuibua Maswali Mengi Zaidi Kuliko Majibu. Dawa na tiba ya vyote hivi ni serikali yenye uwazi, sheria nzuri na #KatibaMpya.  #ChangeTanzania  #WenyeNchiWananchi 

Read More Download Document

Internet Shutdown During The 2020 Election

https://preparepreventresist.org/wp-content/uploads/2022/12/Optima-Tanzania-Report-1.pdf While many other African countries with authoritarian regimes have experienced internet shutdowns in the past decade, Tanzania had not until 2020, when the late president Magufuli was seeking re-election. Leading up to the 2020 election, late president Magufuli enacted a series of laws restricting the ability of journalists, CSOs, and citizens to openly share information in an effort to suppress opposition. Tanzania does not have any legislation that explicitly gives the government power to shut down the internet. However, laws such as the Electronic and Postal Communications Act could be used to grant the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) to order service providers to block or filter content. In the days leading up to and after the general election, WhatsApp, Facebook Messenger, Telegram, and Twitter were blocked on multiple networks, also TCRA ordered telecommunications-service providers to suspend access to bulk SMS and bulk voice services and reportedly censored individual messages with election keywords. Together with the fact that Internet shutdowns have a significant impact on democracy and the economy, there have been no acknowledgements or indications from government leadership in Tanzania to express regret about the 2020 internet shutdowns or indicate that shutdowns will not be used again in the future.   President Samia Suluhu’s government has allowed the reopening of news media that had been banned, and she has spoken publicly about increasing media freedoms. However, little has been done to reform existing repressive laws. Awareness about internet shutdowns is high, but knowledge is low. With general elections in 2025, now is the time to determine advocacy strategy, build coalitions, and make the case to powerful actors that internet shutdowns are neither necessary nor proportionate. Tanzanians need to be equipped with an understanding of internet shutdowns, the circumvention tools they can use if applications are blocked. Advocacy to prevent or stop an internet shutdown requires a diverse coalition of stakeholders and the ability to engage and communicate the importance of shutdown prevention to many sectors of society.

Read More Download Document

Rais samia kupinga uanaharakati nchini kwa hoja kuwa ni uadui kwa taifa.

“Tanzania ndio tunaanza mchakato wa Arbitration, Mara nyingi zinafanywa nje Uingereza na kwingine Wanasheria wetu wakifika kule wanakuta mijitu imebobea wanaongea maneno yanatafunwa ndani hawasikii akiangaliwa macho yanakuwa ya bluu au a kijani hiyo scenario peke yake inaanza kumtisha na vifungu vya sheria alivyokwenda navyo vinaanza kuporomoka kwa hiyo kesi nyingi tunazoshtakiwa nje tunashindwa” https://youtu.be/kxpGf9P_WW0  “Miaka 4 iliyopita tulikuwa na Tanganyika Law Society ambayo ukweli kilikuwa sio chama cha wanasheria kilikuwa chama cha wanaharakati na mapambano yao yalikua dhidi ya serikali sasa mimi nikijua wewe ni dhidi yangu nitakushirikisha wapi? Siwezi kuwashirikisha Mpaka unionyeshe kwamba unanisapoti ndio nitakushirikisha nikikuona una uadui wangu sitokushirikisha utatumia sheria zote za kimataifa na mimi nitatumia sheria za ndani kukuvaa (Kama umekuja na mkono mchafu usinitegeshee nikikuona nitarudi nyuma) kama unataka kufanya kazi na mimi come with clean hands” “Tulikwenda kwenye magereza mbalimbali nchini tukagundua kwamba wengi wao wana kesi za kubambikiziwa kuna mtu yupo gerezani miaka mitatu haendi mahakamani haulizwi na hakuna kesi ya maaana” MAONI JUU YA KAULI YA RAIS Wanaharakati wamekuwa wakipigania haki za binadamu, wakipinga ufisadi na kuibua ukatili wa polisi na vyombo vingine vya serikali. Wanaharakati wanataka #KatibaMpya ambayo itajenga misingi ya haki nchini. Wakati Mashekhe wa uamsho walipokamatwa na kuwekwa ndani kwa miaka karibu 10 wanaharakati walisema sio sawa na hakuna mtu anatakiwa kukamatwa na kuwekwa ndani bila hukumu ya mahakama, Mashekhe hawa walikuja kuachiwa na serikali ya Rais Samia hii ina maana bila kelele za wanaharakati haki yao ingepotea  sasa iweje ana chuki na watu wa namna hii? Ukingalia kwa makini masuala wanayozungumza na kutetea wanaharakati ni yale yanayogusa maslahi ya wananchi. Rais wa nchi anasimama kwa niaba ya wananchi, sasa kwa nini anashambulia watu ambao wamekuwa wakikosoa na kueleza serikali kupunguza ukatili kupitia jeshi la polisi? Serikali ya Magufuli ilifunga watu na viongozi wake walikiuka sheria, tumeona Sabaya aliyekuwa DC Hai amekabiliwa na kesi na kukutwa na HATIA, kuna wengi tu wanalalamikiwa na wananchi lakini walau kuna ushahidi kwamba hawa watendaji walikiuka sheria na wanaharakati walikuwa mstari wa mbele kupingana na matendo yao. Kwa nini sasa wachukiwe na RAIS? Kwa nini Rais anaonekana kushindwa kuungana na wapigania haki?  Kitendo cha kuita wapigania haki kama MAADUI wa Taifa ni hatari na kinatakiwa kukimewa na kila mtu. #ChangeTanzania

Read More Download Document

Nasisi tunashiriki siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia

Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake. Kampeni hii hufanyika kuanzia tarehe 25 Novemba na kumalizika 10 Desemba ya kila mwaka kwa ajili ya kupinga ukatili na kutetea haki za wanawake. Tarehe hii ilichaguliwa kuwaenzi akina dada wa Mirabal sisters, wanaharakati watatu wa kisiasa kutoka Jamhuri ya Dominika ambao waliuawa kikatili mwaka 1960 kwa amri ya mtawala wa nchi hiyo, Rafael Trujillo (1930 – 1961). Tarehe 20 Desemba 1993, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha Azimio la Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake kupitia azimio namba 48/104, kuweka njia kuelekea kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na wasichana duniani kote.  Hatimaye, mnamo tarehe 7 Februari 2000, Baraza Kuu lilipitisha azimio 54/134, likiitaja rasmi tarehe 25 Novemba kuwa siku ya kimataifa ya Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na kwa kufanya hivyo, kukaribisha serikali, mashirika ya kimataifa pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali, NGOs kuungana pamoja na kuandaa shughuli zilizoundwa ili kuongeza uelewa wa umma juu ya suala hilo kila mwaka katika tarehe hii ya 25 Novemba.  Lengo la kampeni hii ni kuongeza ushawishi, kubadilishana taarifa na uzoefu, kujenga uwezo wa pamoja, matumizi mazuri ya rasilimali zinazopatikana na kuunganisha nguvu za asasi za kijamii katika kuhamasisha, kuelimisha, kukemea na kuchukua hatua kwa pamoja ili kupinga ukatili wa kijinsia katika jamii. MAMBO TUNAYOHITAJI WATANZANIA KATIKA KUADHIMISHA SIKU HIZI NI KAMA YAFUATAYO; Uwepo wa usawa katika upatikanaji wa elimu kwa wote watoto wa kike na wa kiume bila kuwanyanyapaa au kuwatenga kutokana na hali au jinsia zao na mambo yahusianayo na jinsia kama ujauzito. Kuwe na #ElimuBilaUbaguzi  Kuongeza ufadhili wa muda mrefu na usaidizi kwa mashirika ya haki za wanawake yanayofanyia kazi masuluhisho madhubuti ya kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji dhidi ya wanawake.  Kupinga kurudi nyuma kwa haki za wanawake, paza sauti za watetezi wa haki za binadamu wanawake, na vuguvugu la wanawake wanaotetea haki za wanawake katika utofauti wao na kuhamasisha watendaji zaidi kujiunga na harakati za kukomesha unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana kote ulimwenguni iwe chachu ya kushiriki na kuunga mkono baadhi ya wanawake wanao pambania haki za wanawake kama shangazi Maria Sarungi Tsehai na shangazi Fatuma Karume.  Kukuza uongozi na ushiriki wa wanawake na wasichana katika nafasi za kisiasa, utungaji sera, na maamuzi kutoka ngazi za kimataifa hadi za mitaa, ikiwa ni pamoja na katika michakato ya maendeleo, binadamu na amani.  Imarisha taratibu za ulinzi ili kuzuia na kuondoa ukatili, unyanyasaji, vitisho na ubaguzi dhidi ya watetezi wa haki za binadamu wanawake na watetezi/wanaharakati wa haki za wanawake. #ChangeTanzania

Read More Download Document

Makala Juu ya adha ya maji inayoendelea nchini.

MAKALA JUU YA ADHA YA MAJI INAYOENDELEA NCHINI Changamoto ya upatikanaji wa maji nchini hasa katika jiji la Dar es salaam na maeneo mengine kama Mwanza ambayo ni majiji makubwa  kibiashara imeibua maswali mengi magumu juu ya huduma muhimu nchini, je kuna vipaumbele vya kutosha? Tuna mikakati ya kuboresha huduma hizi na kuzifanya kuwa stahimilivu katika vipindi vyote vya majira ya mwaka ?. Kukosekana kwa maji Serikali haiwezi kuwepa lawama au kuwajibika sababu maji na umeme ni  huduma za msingi lazima ziwe za uhakika, kukosekana kwa huduma hisi uchuchea mazingira ya magonjwa ya kuambukiza lakini pia uathiri kipato cha wananchi hasa  kipato cha chini , kwa kupoteza muda mwingi kutafuta maji na kupoteza biashara maana wengi hutegemea pia huduma hizo katika biashara zao,  Kukosekana kwa ubunifu au matumizi ya sayansi na teknolojia inachangia sana uhaba wa maji au kukosekana umeme, sera ya maji hasa kwa watu wenye majengo makubwa na viwanja kujihudumia sio rafiki , Serikali ingehamasisha uchimbwaji wa visima virefu kwenye viwanda na makazi binafsi yenye watu wengi mafano magorofa imekuwa dhaifu , lakini pia kwa utaratibu wa hifadhi ya maji kwenye mabwawa makubwa ni moja ya sababu iliyotufikisha hapa, lazima kuwe na a utekelezaji mkubwa kwenye hifadhi ya maji Wakati jiji la Dar es Salaam lina uhaba mkubwa wa maji, Mkuranga kuna tafiti zinaonyesha kuna maji mengi karibu nusu ya ukubwa wa ziwa victoria, Kwa nini tumeshindwa kutumia maji haya ya ardhini kuhudumia jiji la Dar.  Sheria ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009 imeweka mkazo katika ushirikishaji jamii kwenye utoaji wa huduma za maji na usafi wa mazingira; na wananchi kupewa fursa ya kuunda vyombo vya watumiaji maji na kuvisajili kwa Msajili ambaye ni Mkurugenzi wa halmashauri husika. https://www.maji.go.tz/uploads/publications/en1547641391-THE%20WATER%20SUPPLY%20%20AND%20SANITATION%20ACT%20NO%2012%20OF%202009.pdf  Sheria Na.5 ya mwaka 2019 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira, pamoja na mambo mengine, ilianzisha Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ambayo ilichukua majukumu yaliyokuwa hapo awali yamekabidhiwa kwa OR-TAMISEMI, Sekretarieti za Mikoa (RSs) na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Majukumu yaliyohamishwa ni pamoja na kuhakikisha huduma za maji zinapatikana kwenye jamii za watu waishio maeneo ya vijijini, miji midogo na Makao Makuu ya Wilaya. Pamoja na hilo, Sheria Na.5 ya mwaka 2019 imehamisha uwajibikaji wa maafisa wanaohusika na utoaji wa huduma ya maji kutoka OR-TAMISEMI, Sekretarieti za Mikoa (RSs) na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenda Wizara ya Maji. Wakala mpya iliyoanzishwa (RUWASA) ina ofisi ngazi za Makao Makuu Dodoma, Mikoa na Wilaya. Hii ni tofauti na muundo wa hapo awali ambao ulikuwa unajumuisha ofisi katika ngazi ya Serikali za Mitaa (LGAs) na Sekretarieti za mikoa (RSs). Lakini pamoja na uwepo wa sheria na mabadilko hayo hakuna matokeo chnya katika upatikanaji wa huduma ya maji, Je shida ni nini kwa nini hakuna uwajibikaji na uwajibishwaji katika eneo hili?  Katika jiji la Dar Es Salaam hivi karibuni kumekuwa na uhaba wa maji katika maeneo mbalimbali kusababisha kero kwa wananchi na usumbufu mkubwa kwa wakazi wa Dar Es Salaam na kukosa huduma hiyo muhimu kwa afya ya binadamu, kwa kuwa sote tunajua kuwa maji ni uhai. https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/makalla-atangaza-mgawo-wa-maji-dar-3997512  Kwa mujibu wa taarifa za mamlaka ni kwamba kiwango cha uzalishaji maji katika mitambo ya Ruvu juu na chini inayotumika kusambaza maji katika jiji hilo na maeneo ya Pwani kimepungua kutoka lita milioni 466 kwa siku mpaka 300. Hali hii inakuja ikiwa ni miezi mitatu tu imepita tangu Mamkala ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (Dawasa) itoe tathimini yake ikisema jiji hilo linajitosheleza kwa maji kwa karibu asilimia 96. Kulikoni sasa? Kwa taarifa kama hizo bado kunaonekana kuna opotoshaji  mkubwa kwenye taarifa zinazotolewa na viongozi wa serikali juu ya miradi mikubwa  ya maji , Majanga yanapo ibuka kama hivi tunavyoona upungufu mkubwa wa maji ndipo wanajitokeza tena kupoza wananchi na kuandaa uongo mwingine wa kuendelea kutuliza  wananchi, lakini uhalisia ni kwamba wanaoteseka ni wananchi .  Ni wazi kuwa tatizo la maji nchini linachangiwa na ukosefu wa miundombinu ya kuwapatia Watanzania maji safi na salama HAKUNA hifadhi ya maji ambayo ingeweza tumika kwa miezi kadhaa inapotokea dharura au maafa, utamaduni wa kuhifadhi maji sio kipaumbele kwa mamlaka husika, hawatoi elimu wale kukaribisha technologia ya uhifadhi maji majumbani. Tumekuwa na miradi chefuchefu  iliyo chini ya kiwango ambayo inahitaji marekebisho mara kwa mara na inapelekea adha kubwa kwa wananchi, Bomba linalopita TEGETA toka Ruvu mpaka chuo kikuu eneo la Makongo tulitegemea lingekuwa na ukombozi, lakini je kuna hifadhi ya maji ya kutosha kwenye eneo husika? . Tanzania imebarikiwa vyanzo vya maji vya kutosha ni aibu kubwa kulia na mgao wa maji au maji kukosekana kwa kuwa tu serikali imeshindwa jambo dogo tu la kusimamia zoezi zima la kuwafikishia maji watanzania. Kwa mujibu wa DAWASA, hatua za sasa za muda mfupi, mradi wa kigamboni utakua msaada ukitarajia kupunguza uhaba wa maji hasa katika wilaya za Ilala na Kigamboni.Kwa mujibu wa wizara ya maji walisema kuwa mradi huu ungekamilika April 2021 na kuanza kuwanufaisha wakazi wa kigamboni na mji mzima wa DSM, Je changamoto ni nini mpaka sasa mradi huo haujakamilika na wananchi wanapata adha kubwa ya maji?. Wakati tukiendelea kusubiri kina cha maji kiongezeke kwenye mitambo yake kwa "kudra za mvua" mambo mengine ambayo yanatajwa kufanywa na Dawasa sasa ni kutumia visima virefu zaidi ya 170 vilivyopo ambavyo mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam amepanga kuvitembelea. #ChangeTanzania

Read More Download Document

Ripoti Ya Kikosi Kazi – 21 October, 2022

Utangulizi - Ripoti Ya Kikosi Kazi 1.1 Usuli Tanzania ilitimiza miaka sitini (60) ya Uhuru wa Tanzania Bara, miaka hamsini na saba (57) ya Mapinduzi ya Zanzibar na miaka hamsini na saba (57) ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Mwaka 2021. Katika kipindi hiki, nchi yetu imepitia katika awamu za uongozi na mifumo mbalimbali iliyokusudia kuimarisha uhuru, umoja, amani, utulivu, demokrasia na utawala bora. Ripoti hii inahusu juhudi zinazoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Awamu ya Sita za kuimarisha na kuboresha mfumo wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa na Utawala Bora. Kabla ya uhuru, chama cha siasa Tanganyika African National Union (TANU) kilichoanzishwa mwaka 1954 kikiongozwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kiliongoza jitihada za kutafuta uhuru wa Tanganyika. Pamoja na TANU kulikuwepo na vyama vya siasa vingine vikiwemo, United Tanganyika Party (UTP) kilichoanzishwa mwaka 1956, African National Congress (ANC) kilichoanzishwa mwaka 1958 na All Muslim National Union of Tanganyika (AMNUT) kilichoanzishwa mwaka 1959 kwa upande wa Tanganyika. Kwa upande wa Zanzibar, kulikuwa na vyama vya siasa vifuatavyo, Afro-Shiraz Party (ASP) kilianzishwa tarehe 5 Februari 1957, Zanzibar and Pemba People’s Party (ZPPP) kilianzishwa mwaka 1959, Zanzibar Nationalist Party (ZNP) kilianzishwa mwaka 1955 na Chama cha Umma kilianzishwa mwaka 1962. Vyama hivi vinadhihirisha kuwepo kwa mfumo wa demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa hata kabla ya uhuru. Tarehe 9 Desemba 1961 Tanganyika ilifanikiwa kupata uhuru wake kutoka kwa utawala wa kikoloni wa Uingereza na hivyo kuendelea na mfumo wa demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa baada ya uhuru, ambapo mfumo huo ulitamkwa katika Katiba ya Uhuru (Independent Constitution of 1961). Tarehe 9 Desemba 1962 Tanganyika ilipata Katiba Mpya, ambayo iliitangaza Tanganyika kuwa Jamhuri. Tarehe 12 Januari 1964, chama cha siasa Afro-Shiraz Party (ASP), kikiongozwa na Sheikh Abeid Amani Karume, kiliongoza wananchi wa Zanzibar kufanya Mapinduzi na kuunda Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Baada ya Mapinduzi Vyama vya Siasa vingine pamoja na asasi za kiraia vilipigwa marufuku. Tarehe 26 Aprili 1964 Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kuwa nchi moja inayoitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Muungano huo wa nchi mbili, umedumu kwa miaka zaidi ya hamsini, hivyo ni muungano pekee hai katika bara la Afrika. Hata hivyo, kuna changamoto kadhaa katika Muungano huo ambazo zimekuwa zikifanyiwa kazi na kupungua siku hadi siku. Baada ya Muungano kulikuwa na Katiba ya Muda ya Muungano inayoitwa “The Interim Constitution of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar of 1964”, na mwaka 1965 ikatungwa Katiba Mpya ya Mpito inayoitwa “The Interim Constitution of Tanzania of 1965)”, iliyodumu hadi mwaka 1977. Katiba ya mwaka 1965 ilifuta mfumo wa vyama vingi vya siasa na kuanzisha mfumo wa chama kimoja cha siasa mwaka huo huo. Aidha, mwaka1967 lilitangazwa Azimio la Arusha ambalo liliweka misingi ya maendeleo ya uchumi na ustawi wa jamii katika mrengo wa ujamaa na kujitegemea na kuimarisha mfumo wa chama kimoja. Mwaka 1977 vyama viwili vya siasa ASP na TANU viliungana na kuunda Chama cha Mapinduzi (CCM). Sambamba na hilo, ilitungwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 iliyoanza kutumika tarehe 26 Aprili 1977. Mwaka 1992, Serikali ya Awamu ya Pili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliunda Tume ya Rais ya Kukusanya Maoni Kuhusu Chama Kimoja au Vyama Vingi vya Siasa na kufanyika kwa Mabadiliko ya Nane ya Katiba yaliyorejesha mfumo wa vyama vingi vya siasa Tanzania. Sababu za mfumo huo kurejea ni hizi zifuatazo: a) vuguvugu la mabadiliko ya kisiasa duniani, ambapo kulikuwa na msukumo wa nchi mbalimbali kutoka katika mfumo wa uchumi hodhi na siasa za kijamaa na kuelekea katika mfumo wa uchumi huria na demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa; na b) msukumo wa ndani ya nchi wa kudai mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa, kutokana na hali ngumu ya kiuchumi iliyokuwepo katika miaka ya themanini. Baada ya mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa kurejea mwaka 1992, Vyama vya Siasa vimekuwa vikifanya jitihada za kutafuta wanachama, kunadi sera zao kupitia mikutano ya hadhara, kujiimarisha kitaasisi kupitia mikutano ya ndani na kuweka mifumo mbalimbali ya kiutawala. Hatimaye, vyama hivi vilianza kushiriki Uchaguzi Mkuu na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kutafuta uongozi wa kisiasa. Tangu mwaka 1992 mpaka mwaka 2015 kulifanyika uchaguzi mkuu mara tano. Matokeo ya uchaguzi katika kipindi hicho yalionesha kukua kwa hali ya ushindani.....!

Read More Download Document

Fahamu Kuhusu Msingi Wa Madaraka Makubwa Ya Rais Katika Nchi Ya Tanzania.

Tulipoingia kwenye mfumo wa urais mwaka 1962 baada ya kupata uhuru mwaka 1961 , hatukuanza maisha tukiwa na Rais, hata wakati wa mkoloni cheo hiki hakikuwepo kabisa kwenye mfumo wa uongozi nchini, huyu kiumbe ni wa mwaka 1962 sio kiumbe wa uhuru Urais ulikuwa baadaye. Tumeingia katika uhuru madaraka ya serikali yalikua chini ya waziri mkuu anayewajibika kwa Bunge, huyu ndiye alikuwa mkuu wa serikali na mtendaji mkuu katika nchi yetu,. Lakini  Bunge kilikua chombo chenye mamlaka makuu ya nchi na Waziri mkuu alikuwa anafanya kazi kwa imani ya Bunge. Waziri mkuu alikuwa anahojiwa na bunge na mambo yote alitakiwa kupitisha bungeni ili atekeleze, japo lilikuwa ni bunge la chama kimoja lakini kulikuwa na upinzani mkali sana ndani ya bunge hilo. Bunge lilikua na mamlaka ya kumuondoa waziri mkuu  likikosa imani naye kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani kama ilivyo Uingereza, India, Ujerumani, Israel, Japan, Uholanzi kama zilivyo nchi nyingine zote zilizoendelea isipokuwa Marekani na Ufaransa. Kwenye masuala yanayohitaji mkuu wa nchi kulikua na Gavana General, tulikuwa bado kwenye himaya ya kiingereza. Huu mfumo wa kibunge ni mfumo wa kiingereza. Kwahiyo tuliingia katika uhuru tukiwa na mfumo huu yaani baada ya Malkia kulikuwa na Gavana Jenerali. Gavana Jenerali alikua mkuu wa nchi asiyekuwa na mamalaka ya kiutendaji, kama alivyo mfalme wa uingereza, Rais wa India, Ujerumani, Israel, Malkia wa nchi yoyote wa Ulaya. Gavana Jenerali alikuwa  head of state na commander in chief kwa jina tu, Mwenye mamlaka ya kiutendaji alikuwa ni waziri mkuu aliyekuwa chini ya Bunge, na kuwajibika kwa bunge. Mambo  yalibadilika baada ya kupata uhuru, kwani Miezi miwili baada ya uhuru mwalimu Nyerere akajiuzuru  ambaye ndio aliyekuwa waziri mkuu. #MwlNyerere alipojiuliza historia tunayofundishwwa mashuleni tunaambiwa kwamba ajiuzulu kwenda kuimarisha Tanu. Tanu mwaka 1962 ilikua na miaka 7 tu, na ilikua imeongoza uchaguzi mkuu wa mwaka 1960 sasa TANU ilikua na udhaifu gani wa kumfanya Nyerere ajiuzulu ni propaganda na uongo. Maana TANU ilikuwa imemaliza kushinda uchaguzi haikuwa dhaifu. Kilichomfanya Nyerere kujiuzulu mapema mwaka 1962 miezi michache kabla ya Uhuru kulikuwa na mgogoro mkubwa bungeni juu ya sheria ya Uraia, sheria hii tuliyonayo msingi wake ni mwaka 1962 na kwenye huo mjadala bungeni kulikua na upinzani mkubwa wa wabunge.  Bunge lilikua na Wanachama 81 wa TANU, isipokuwa mmoja tu Mbunge wa Mbulu ambaye Mwl Nyerere na wenzake hawakumpenda wakakataa kumuingiza kama mgombea akaingia kama mgombea binafsi akashinda. Kwenye mjadala wa sheria ya Uraia, Kulikuwa na Upinzani mkubwa Nyerere alisemwa sana na ilimtisha hiyo sheria kupitishwa. Hivyo  akajiuzulu ili kwenda kuandaa mapinduzi ya kikatiba, ili kwenda kuupindua mfumo wa kikatiba unaoipa Bunge mamlaka makubwa. Serikali ya Tanganyika ikawasilisha white paper baada ya Nyerere kujiuzulu  ili Tanganyika iwe Jamhuri  na Nyerere alikwenda kuifanyia kazi.  Hiyo White Paper (waraka mweupe)  ndiyo ilipendekeza Tanganyika iondokane na mfumo wa Waziri mkuu wa kuwajibika Bungeni na ifate mfumo wa Rais kuwa mkuu kiutendaji.   Waraka mweupe ulisema yafuatayo juu ya Rais; waraka ulitengenezwa na Nyerere na alisema hivi,  Kwetu sisi Rais atapewa heshima na hadhi anayopewa chifu  au mfalme au chini ya Jamhuri, Rais kwetu sisi hawezi kutofautishwa na mamlaka aliyokuwa nayo mfalme. Habari ya kutenganisha hadi ya mfalme na madaraka kama ilivyo India au Ujerumani au hizi nchi nyingine hii haifai yani tunataka heshima iwe ya kifalme, madaraka yawe ya kifalme na hadhi iwe ya kifalme hauwezi kuitenganisha yaani kwetu sisi hatuwezi kuyatengenisha. Waingereza wameyatengenisha hadhi na heshima ya mfalme na madaraka aliyonayo kwahiyo sisi tunataka kuunganisha. Maana yake tunataka Rais atakayekuwa na madaraka na heshima kama mfalme. Waraka wa serikali ya Tanganyika mwaka 1962 na ndio unaelezea huyó Rais atakuaje; atakuwa mkuu wa nchi, amiri jeshi mkuu na kiongozi mkuu wa serikali, wateule wote wa vyombo  vya dola watakuwa wateule wa Rais. Waraka wa serikali ya Tanganyika mwaka 1962 unaeleza watu wote walio katika utumishi wa umma wasiokuwa wateule wa Raiss watafanya kazi kwa niaba ya Rais, Tume zote, Majaji na kila mtu aliye katika utumishi wa umma atateuliwa na Rais au atafanya kazi kwa niaba. Waraka wa serikali ya Tanganyika mwaka 1962 unaelezA, Rais atapewa mamlaka ya kinidhamu ya kuamua nani afanye kazi nani aondolewe kazini, atapewa mamlaka ya kuteua wabunge, mamlaka ya kuvunja Bunge ambayo hayakuwepo na kuhutubia bunge wakati wowote. Waraka wa serikali ya Tanganyika mwaka 1962 unaeleza Rais atapitisha miswada ya sheria na kuteua watendaji wakuu wa vyombo vyake ikiwemo bunge na mahakama, mamlaka ya kuamua mpaka mishahara ya wabunge yote hi ni kazi ya Nyerere mwaka 1962. Kulikua na upinzani mikubwa ndani ya Bunge kupitisha waraka mweupe lakini Baadae wakamkubalia sasa tukaingia kwenye Jamhuri. Tumetengeneza katiba toka mwaka 1962, Katiba haikutokea kwa bahati mbaya ni Nyerere alitaka iwe hivyo na alipendekeza na kuetetea uwa haoni tofauti kati ya mfalme na Rais. Badaae alitambua madaraka makubwa aliyokuwa nayo mwaka 1967 akasema hivi “Nina mamlaka ya kuwa dictator akizungumza na gazeti la uingereza la Observer 1967 na mwaka 1978 anazunguzma na BBC akasema vile vile, ukweli ni kwamba aliyataka, aliyatetea na kutengeneza mwenyewe. #MwlNyerere hakuwa mtu wa demokrasia mpaka anaondoka madarakani amekuja kufunguka macho akiwa nje ya ikulu, Nyerere aliweka watu kuzuizini maelfu na maelfu, siku tukiingia madarakani mtajua idadi ya watu wahanga wa utawala wa Nyerere. Lakini pia Nyerere alituunganisha na Zanzibar yeye peke yake, muungano haukutokana na azimio baraza la mawaziri, haukutokana na  Bunge ilikua ni siri, siri yake yeye na wasaidizi wake wachache akiwemo waziri wa usalama wa Taifa Bwana Munaka na mwanasheria wa serikali Bwana Rolland Brown na upande wa Karume alikuwa na yule aliyeambiwa akanyoe ndevu huku nyuma wakasaini mkataba.  Tumetengenezewa mfumo ambao unamtaka Rais atumie utawala wake anavyotaka na kwa kutumia madaraka hayo akapiga marufuku vyama huru vya wafanyakazi mwaka 1964, Akapiga marufuku vyama huru vya ushirika mwaka 1966, Akapiga marufuku serikali mitaa zilizokuwa huru 1972. Nyerere alitumia madaraka yake ya urais akahamisha watu kwa nguvu (opresheni vijiji) 1973 -77 watu zaidi ya milion 8 asilimia 75 walitolewa kwenye maeneo yao kupelekwa katika maeneo yanayoitwa vijiji vya ujamaa. Nyerere alitumia madaraka yake ya urais akatuingiza katika uchumi dola 1967 Azimio la Arusha liliamuliwa kwa bunge gani? Kanyang’anya watu mali zao kwasababu ya Azimio la Arusha, akapiga marufuku vyombo huru vya habari mwaka 1968-69. Tukaanzishiwa Uhuru na Daily news za serikali na Radio ni moja tu Radio Tanzania, akapiga marufuku vyama vya siasa mwaka 1964-65, Tukatengenezewa mfumo wa kidikteta ambao tunahangaika nao sasa hivi. Ni mfumo wa kidikteta uliotengenezwa na mwalimu Nyerere mwaka 1962 tusije tukasahau hilo kwa sababu kumekuwa na jitihada nyingi sana za kumfanya kuwa mtakatifu sio tu wa kisiasa hata wa kidini na watakatifu huwa hawasemi vibaya. Ili tuondokane na huu mfumo wa Nyerere inabidi tukabiliane naye kwenye mijadala kama hii. Haya mambo yamejulikana muda mrefu sana mwaka 1990-91 wakati tunajiandaa kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa ilikua ni njia ya kukataa ile legacy ya Nyerere, Tume ya Nyalali ilipendekeza mambo mengi ikiwemo kuwa na katiba mpya ya kidemokrasia ukisoma ripoti ya Nyalali ilikua na juzuu 2 zile zilikuwa ni ukosoaji wa mfumo wetu wa kisiasa kama ulivyojengeka toka 1962, angalau kwamba toka 1961 ulikua unajulikana rasmi huu mfumo wa urais wa kifalme umetuumiza inabidi tuondokje nao na toka wakati huo tumejifunza mambo mengi sana, sasa haya mambo yote tulkiyojifunza yameelezwa vyema sana na tume ya warioba, ila kuna jitihada nyingi za kutusahaulisha kazi kubwa iliyo fanywa na Warioba. Katika juzuu zake Tume ya Warioba kuna volume kubwa kuhusu utafiti kuhusu mambo masuala mbalimbali ya kikatiba, katika tafiti hizo utafiti wa kwanza unaitwa utafiti kuhusu madaraka ya Rais wa Jamhuri ya muungano Tanzania, hili ndilo la kwanza walianza nalo kwasababu wanajua hili ndilo shina la matatizo ya watanzania, kuhusu maadili ya viongozi na uwajibikaji, Kuna utafiti unauhusu muungano wa Tanganyika na Zanzibar,  na kuna ushauri elekezi juu ya mifumo ya uchaguzi na tume ya uchaguzi haya ndiyo mambo manne makubwa ambayo tumeilifanyia uchunguzi mahususi. #KatibaMpya #WenyeNchiWananchi

Read More Download Document

Report on the audit of utilization of funds issued of funds under the catastrophe.

The IMF Executive Board through a Press Release of 10 June 2020, approved debt relief to Tanzania under the Catastrophe Containment and Relief Trust (CCRT), amounting to USD 25.7 million (equivalent to SDR 18,566,777 or TZS 58,800,009,860) from 10 June 2020 to 30 April 2022. The funds were earmarked to fight adverse impacts of the COVID-19 pandemic by improving the public health sector and mitigating the shocks on the balance of payments brought by the pandemic. The IMF Country report to Tanzania No. 20/203, the Fund Press Release and Letter of Intent from Government of URT to the Fund with Ref. No. CMB.445/624/01 dated 27 May 2020 require the Controller and Auditor General to perform post-audit on the CCRT Fund and publish the audit report. In that regard, I structured my audit to include a review of financial transactions, internal controls and operations to the extent considered necessary for the effective performance of the audit to provide assurance on the appropriate utilisation of funds. The following are key audit matters of my report. I confirmed BOT transferred a total of SDR 18,566,777 (USD 25,700,000) equivalent to TZS 60,465,678,582 being the sum of the total facility provided to the government. The noted increment of TZS 1,801,997,721 (from TZS 58,800,009,860 to TZS 60,465,678,582) is a result of depreciation in exchange rate between TZS and strong currencies (SDR and USD). The Government received the funds through Development Revenue Account 9921139901. The Government of the United Republic of Tanzania allocated the facility funds to Health and Tourism Sectors as required in the facility’s conditions. In the Health sector, funds were directed to National Public Health Laboratory (NPHL) to acquire the necessary facilities to enhance the testing of COVID 19 and to establish a center for oxygen production at Benjamin Mkapa Hospital. In the tourism sector funds were directed to provide budget support in terms of salaries, other charges and financing of infrastructure projects to government entities involved directly in the sector which were experiencing a significant loss in revenues due to the pandemic. I confirmed completeness in transferring and receiving CCRT funds between Treasury, Parent Ministries and Implementing Agencies. I audited the utilization of funds in all Implementing Agencies, for which I reviewed financial transactions, procurement processes and contracts and performed physical verification of assets. The following is the summary of key audit findings and recommendations. Details are reflected in the body of this report. A. Health Sector Lack of contract between MoH and MSD for procured non-catalogue items I noted that items ordered by MoH from MSD for NPHL were non catalogue items. As such, the Ministry was required to have a special contract with MSD to ensure effective execution and supervision of the tender. However, MoH could not provide a specific contract with MSD on the procured items but explained the reliance on the existing general MOU. Recommendation I recommend that the Management of MoH enhance contract management by ensuring the signing of special contracts with MSD whenever specific procurement of non-catalogue items is involved. Weaknesses noted in procurement process of the Contractor for installation, commissioning and training of oxygen medical plant Review of contract No. PA/148/2020-2021/P/26 for the supply, installation, commissioning, and training of oxygen medical plant entered into by Benjamin Mkapa Hospital and Ozcan Kardesler Tip cihazlari Ltd Sti (The Manufacturer), noted that, the management provided two extensions to the contractor without documenting justifiable reason to which extension was requested and granted. This is contrary to Regulation 110(2) of Public Procurement Regulations, 2013. Further, I also noted that respective performance bond and advance payment guarantee were not extended to match the granted time extensions, contrary to the Special Conditions of underlying Contracts. I recommend that Management ensure in future; (a) Extensions are properly requested by contractors with justification, and Project Managers analyse the mentioned reasons with evidence and correctly determine the time extension to be granted; and (b) Contractors and Suppliers submit extended or new securities to cover the contract extension granted. B. Tourism Sector Inadequate utilisation of development funds As of 17 March 2022, TANAPA and NCAA had unutilised fund balance from development projects of TZS 2,367,536,799 (17%) and TZS 6,124,242,713 (63%) respectively. The challenges were mainly attributed to delays in obtaining approval for reallocation of funds and retendering of tenders. I recommend that Implementing Agencies ensure disbursed funds are utilised for the intended projects and at the right time. Delayed delivery of products and completion of projects I noted the delays in completing construction works in TANAPA, NCAA, and TAWA. Seven projects worth TZS 6,124,242,713.29 in NCAA were not implemented as of 15 March 2022. Construction of NAABI entrance and exit gates was delayed for twenty-seven (27) months in TANAPA. Also, the construction of the Tourism lounge and rest banda by TAWA has been delayed for three and seven months respectively. Further, I noted that TAWA requested GPSA to procure nine (9) vehicles, Toyota Land Cruiser Hard Top-LX at TZS 1,393,819,344.54. Full payment was made on 4 May 2021; however, as of the time of audit on 16 March 2022, four vehicles worth TZS 619,475,264 were yet to be delivered to TAWA. Likewise, I noted that TANAPA deposited TZS 894,539,725 to Tanzania Wildlife Protection Fund (TWPF) account on 30 June 2020 to acquire arms and ammunitions intended to enhance the defence and security of the National Parks. As of 18 March 2022, when the audit was conducted, being twenty-one (21) months since the funds were deposited in the TWPF account, no delivery of arms had been made. Delayed construction and delivery of products in all cases are attributed to the impact of COVID 19 pandemic on suppliers/contractors’ operations. I recommend that Implementing Agencies liaise with responsible Government institutions to ensure timely delivery of the required products to attain the intended objectives. Challenges noted in the implementation of infrastructural development projects My audit on funds that were disbursed for development projects in the tourism sector mainly to improve tourism infrastructures noted the following weaknesses; inadequate design and specification of projects, implementation of projects without feasibility studies, lack of as-built drawings, inappropriate change management controls and insufficient supervision of projects. The weaknesses were attributed to shortfalls in the management of projects. I recommend that the Management of Implementing Agencies enhance controls to improve the supervision of development projects. Download document to read more…..

Read More Download Document

#KatibaMpya Jana na Leo – Jenerali Ulimwengu  

Jeshi la polisi ni chombo muhimu sana katika nchi hasa katika kulinda amani, demokrasia na utawala bora, Jeshi la polisi lina wajibu wa kulinda wananchi pale wanapokuwa na hoja ya kuwasilisha kwa wananchi kupitia maandamano, hii ni haki ya msingi sana na imewekwa katika misingi ya sheria zetu yaani Katiba.Wananchi wana haki ya kufikisha malalamiko au hoja za kwa viongozi, namna ya kuwasilisha hoja hizo inaweza kuwa maandamano ya amani, sheria zetu zinaruhusu namna hii ya hisia au mfumo katika kuwasilisha maoni, lakini tumekuwa na uzoefu tofauti sana sana hasa kutokana na matendo ya jeshi la polisi, wao kazi yao nimekuwa ni kuzuia tu, wamekuwa na akili ya aina moja tu ya kuzuia bila kuangalia umuhimu wa wananchi kuwa na nafasi kuwasilisha malalamiko yao. Kama wananchi watakuwa na fursa ya kuwasilisha malalamiko au maoni yao kwa viongozi, ndivyo pia wataweza kuwa na hali ya kusifia au kupongeza viongozi wao. Haya mambo yanaendena sana na ni muhimu yote kwa pamoja yakaheshimika   “Polisi hawana uzoefu wa kuratibu maandamano ya namna yoyote kwa muda wa miaka mitano iwe anapongeza au anakosoa huwezi kupata hiyo nafasi. Hii sio sawa kwa Taifa kuwa na polisi na namna hii. 2016 Magufuli alisema Demokrasia kwake yeye ni kuwajengea watu miundombinu kama  barabara, ili waweze kusafirisha mazao na tukampigia makofi na kweli akaanza kujenga mpaka vitu vingine ambavyo hatujui vinatusaiudia walipa kodi. Magufuli alipiga marufuku vyama vya siasa na alisema wazi kuwa kufikia 2020 hakutokuwa na upinzani Tanzania na kweli 2020 tuliona jinsi ambavyo upinzani uliondolewa Magufuli alipiga marufuku sio upinzani tu hata shughuli za kisiasa ndani ya chama chake mwenyewe hakuna shughuli za kiasa pale katika ccm zinazoendelea isipokuwa ni shughuli zinzohusika na mambo ya kiserikali na kiutawala tu. Imefika 2015 alipoingia Magufuli anachokita yeye ndio inakuwa sera ya nchi, sera ya chama na sera ya serikali kwa hiyo Magufuli ndio alikuwa anaamua. N aipata hii nguvu kutokana na mapungufu makubwa yaliyoko katika katiba yetu ambayo imempa Rais madaraka makubwa zaidi, Hivyo akitokea mtu mwenye sifa kama za Rais magufuli haya ndio matokea yake. Rais Magufuli kweli alikuwa ni Rais mbaya na hilo wala sitaki kuomba radhi kwa yeyote yule. Rais Magufuli hakufaa kuwa Rais wa nchi yetu na alitufanyia mambo mabaya sana mpaka leo tunaumia kwa sababu mambo aliyoyaacha, na mpaka leo hakuna aliyeyagusa kuna watu wamekaa nayo tu kama vile wamemeza bangi, wanaogopa kuyasema wazi, ili iwe fundisho kwa wengine. Kuna watu wanamsifia hasa kwa kusema alikuwa anapambana na rushwa, sas msiniambie kuwa alikuwa anapambana na rushwa kwa sababu mtu anayepambana na rushwa hawezi akazuia magazeti yote lakini pia akazuia bunge ili wannachi wasifahamu yanayoendelea. Mtu anayepambana na rushwa anahitaji sana msaada wa vyombo vya habari vimsaidie kufichua maovu yote, anahitaji sanaa masaada wa bunge huru la kumpa taarifa nini kinatokea nchini kote, sasa kama yeye alikuwa anapambana na Rushwa kwa nini azuie vyombo ambavyo ni msaada kwake katika mapambano na rushwa? Wale aliowatuma Magufuli kuzima vyombo vya habari bado wako serikalini na sisi tunawafahamu siwezi kumsahau Dr Abbasi, huyu alichangia kuhakikisha vyombo vya habari havifanyi kazi kabisa. Watu kama hawa hawafai kupewa nafasi za kutuongoza kwa sababu hawana nia njema na nchi yetu isipokuwa wapo kwa ajili ya watawala tu. Tunasikia za chini chini kuwa CCM wataanzisha machakato wa katiba mpya kwa ukubwa lakini matarajio yao yakiwa sio 2025 sasa watu wa aina hii ukiwaamini wewe unakuwa mjinga. Unakuwa ni mjinga kama ukipingana na kila kitu anachosema mpinzani wako, lakini vilevile unakuwa ni bwege kama kila kitu anachokisema mpinzani wako unakichukulia kama ni ukweli. Tusiwaamini na tuendelee kupambana kuhakikisha tunapata katiba mpya nzuri inayotokana na maoni halali ya Wananchi. https://www.youtube.com/watch?v=97p-sSqHykQ #MariaSpaces #WenyeNchiWananchi #KatibaMpya 

Read More Download Document

Requests for disbursement under the rapid credit facility and purchase under the rapid financing instrument.

In the context of the Requests for Disbursement Under the Rapid Credit Facility and Purchase Under the Rapid Financing Instrument, the following documents have been released and are included in this package: • A Press Release including a statement by the Chair of the Executive Board. • The Staff Report prepared by a staff team of the IMF for the Executive Board’s consideration on September 7, 2021, following discussions that ended on July 16, 2021, with the officials of the United Republic of Tanzania on economic developments and policies underpinning the IMF arrangement under the Rapid Credit Facility. Based on information available at the time of these discussions, the staff report was completed on August 20, 2021. • A Debt Sustainability Analysis prepared by the staffs of the IMF and the International Development Association (IDA). • A Statement by the Executive Director for the United Republic of Tanzania. The IMF’s transparency policy allows for the deletion of market-sensitive information and premature disclosure of the authorities’ policy intentions in published staff reports and other documents. IMF Executive Board Approves US$567.25 Million in Emergency Support to Tanzania to Address the COVID-19 Pandemic FOR IMMEDIATE RELEASE • The COVID-19 outbreak has led to the collapse of the tourism sector and amplified the need for significant financing to tackle the health and economic effects of the pandemic. • The IMF approved US$567.25 million in emergency financial assistance under the Rapid Credit Facility and Rapid Financing Instrument to support the authorities’ efforts in responding to the pandemic by addressing the urgent health, humanitarian, and economic costs. The resources are also expected to play a catalytic role in their efforts to mobilize additional support from development partners. • The authorities also commit to strengthening governance and transparency to ensure that the financial resources are efficiently spent on addressing the crisis. Washington, DC – September 7, 2021: The Executive Board of the International Monetary Fund (IMF) today approved a disbursement of SDR132.6 million (US$189.08 million) under the Rapid Credit Facility (RCF) and a purchase equivalent to SDR265.2 million (US$378.17 million) under the Rapid Financing Instrument (RFI), a total of SDR397.8 million (US$567.25 million or 100 percent of quota). This emergency financing will help finance Tanzania’s urgent balance of payment needs stemming from the outbreak of the COVID-19 pandemic. Tanzania’s economic outlook has deteriorated due to the impact of the COVID-19 pandemic. With the collapse in tourism in the wake of travel restrictions, the economy reportedly decelerated to 4.8 percent growth in 2020, and growth is expected to remain subdued in 2021.Tanzania faces an urgent balance of payment need of about 1.5 percent of GDP as the authorities implement a comprehensive plan to mitigate the effects of the pandemic and preserve macroeconomic stability in the face of a reported third wave of the virus. The disbursement under the RCF and purchase under the RFI will help finance the interventions needed to mitigate the severe socio-economic impacts of the pandemic and help catalyze support from development partners. The authorities have indicated that they are committed to pursuing economic policies appropriate for addressing the impact of the pandemic and are committed to strengthening coordination and transparency to ensure that RCF and RFI resources are spent on fighting the pandemic. These measures include publishing reports of RCF and RFI resources spent and undertaking a post-crisis audit of all pandemic-related spending. Following the Executive Board’s discussion, Mr. Bo Li, Deputy Managing Director and Chair, issued the following statement: “The COVID-19 pandemic has negatively impacted Tanzania’s macroeconomic outlook, and the health and wellbeing of its population. Growth decelerated in 2020 and is expected to remain subdued in 2021, increasing poverty and negatively affecting employment. Tanzania’s risk of external and public debt distress increased to moderate, mainly due to the pandemic’s effect on tourism exports. Tanzania’s macroeconomic outlook hinges on satisfactorily addressing the pandemic, but significant downside risks remain due to uncertainties surrounding the course of the pandemic. “The authorities are implementing a comprehensive pandemic response plan—Tanzania COVID-19 Socioeconomic Response Plan (TCRP) —to address the fallout of the COVID-19 shock. Tanzania requires urgent financial assistance to implement the plan and avert the severe health, social and economic consequences of a reported third wave of the virus. Emergency support under the Rapid Credit Facility and Rapid Financing Instrument will substantially contribute to filling immediate external financing needs and help catalyze donor support. Temporarily loosening macroeconomic and financial policies will mitigate the pandemic’s adverse impact, by deploying a vaccination campaign, increasing health and social spending, and supporting the private sector. Prioritizing the health response, strengthening coordination and transparency to ensure that funds received are spent on fighting the pandemic, and regularly and transparently reporting epidemiological data will be critical for the plan’s success. “Maintaining fiscal and debt sustainability, and preserving financial stability, while supporting the economy, will also be important. Closely monitoring the banking system’s health in light of increased banking sector vulnerabilities will be key. “Once the crisis abates, the authorities appropriately intend to resume implementing reforms to achieve sustainable and inclusive growth. Their broader policy and reform agenda includes fiscal reforms to avoid domestic arrears and pay tax refunds on time, increasing support for education and health spending, and improvements to the business climate.”

Read More Download Document

Utawala wa sheria Loliondo na Ngorongoro

Leo nitazungumza kuhusu sheria uhifadhi ya wanyama pori ya mwaka 2009 ambayo kwayo hii amri ya kutenga maeneo mawili ya wilaya ya Ngorongoro yaliyopo katika eneo la Loliondo kuwa ni maeneo ya udhibiti wa wanyama pori, sio mapori tengefu ya wanyapori, nitaelezea tofauti kati ya haya maneno mawili.  Kwasababu yana umuhimu mkubwa sana na baadae swali ambalo najiuliza nitataka kulijibu ni kwamba ‘Hili tangazo la haya maeneo mawili ya Loliondo kuwa maeneo ya udhibiti ya wanyamapori ni halali au ni hamaramu kama kawaida ya mambo ya Tanzania ya CCM. Nikiuliza swali hilo nahisi wengi mnajua jibu langu ya kwamba, kilichotangazwa ni haramu tupu kwa mujibu wa sheria ya wanyama pori, mkihisi hivyo mtakua hamjanikosea. Kwanza nianze kwa kusema yale ambayo ni fact zisizokuwa na mgogoro wowote yaani yale ambayo hayana ubishani, hakuna ubishani sasa kwasababu tuna ushahidi sasa kwamba wiki iliyopita tarehe 17 ya mwezi huu waziri wa maliasili na utalii na maliasili, Mh Pindi Chana ametoa amri inayoitwa amri ya kutangaza eneo la udhibiti wa wanyamapori linaloitwa POLORETI Haya maeneo mwili yaliotengwa kwa ujumla yake yanaitwa POLORETI GAME CONTROL AREA Haya maeneo mawili kwa ujumla wake limetangazwa tarehe 17 June ya mwaka huu yani wiki iliyopita na limetangaza kisheria kwa kuchapishwa kwa gazeti la serikali linaloitwa namba 221 la 17 June 2022 hili halina ubishi. Kuna kitu kingine hakina ubishi kwamba kwa mujibu wa tangazo hili eneo ambalo limetengwa lina ukubwa wa km za mraba 1952. Tumekuwa tukiambiwa na waziri mkuu na hili ni muhimu kwa sababu waziri mkuu wetu ni muongo, sasa waziri mkuu wetu na serikali nzima wametuambia eneo linalotengwa ni km za mraba 1500 ukweli usiokuwa na shaka na ushahidi wake ni tangazo lenyewe ni kwamba eneo linalochukuliwa ni km 1952.   Kuna KM 1502 za mraba za eneo la kwanza ambalo linapakana na hifadhi ya serengeti, kun aeneo la pili ambalo hawalisemi kabisa lipo chini mwa Lake Natron, eneo unalolipita ukienda Loliondo hili eneo lina ukubwa wa km 450 kwa hiyo jumla ya eneo lote ambalo zilizotangazwa ni km 1952 na sio km 1500 ambazo tumeaminishwa, na serikali ya uongo ambayo inasema Rais Magufuli anafanya kazi ofisini kumbe amekufa huo ni uongo. Na mpaka sasa sijui ni kwanini Rais Samia anasubri nini kumfukuza kazi Kasimu Majaliwa, mtu ambaye anaidharaulisha serikali nzima na chama kwa uongo. La tatu ni kwamba hili eneo ni eneo la udhibiti wa wanyama pori sio eneo tengefu la wanyapori, kisheria hili eneo sio game reserve bali ni  game control area, maana ya kuwa game control na game reserve ni nini? eneo tengefu la wanyapori ni eneo ambalo linatangazwa na Rais kwa kushauriana na halmashauri za serikali za mitaa wa maeneo husika na kutangazwa kwenye gazeti la serikali, eneo la udhibiti linatangazwa na waziri baada ya kushauriana na halmashauri za serikali za mitaa wa maeneo husika.  Hili lililotangazawa ni Eneo la  udhibiti wa wanyamapori, tofauti muhimu zaidi ni kwamba ukitangaza eneo kuwa eneo tengefu la wanyama pori kwa mujibu wa sheria eneo hilo linaondolewa mikononi mwa wananchi na ndio maana katika sheria ya wanyamapori imelekeza kwamba eneo likitangazwa kuwa game reserve ni lazima wananchi walipwe fidia ya haki na kutekelezwa na sheria imesema iwalipe fidia kwa mujibu wa sheria za ardhi, mpaka kufanya tathmini na kulipwa fidia ya haki timilifu na ya wakati muafaka. Kwenye Maeneo ya udhibiti kwenye haya maeneo ambayo yametangazwa sasa, hakuna masharti yoyote ya kulipa mtu fidia, swali ni kwanini. Jibu lake ni kwamba sheria hii imepiga marufuku kutangaza eneo la ardhi ya vijiji, unaweza kutangaza katika eneo ambalo sio ardhi ya vijiji tu. Kwa waliomsikiliza mbunge wa Ngorongoro jana amenikosha sana amezungumza hoja nzuri sana na mwenye mawasiliano yao anifikishie pongezi zangu. Hoja ya mbunge wa Ngorongoro jana ni kwamba hilo eneo mnaloliita eneo tengefu ni eneo la vijiji kwa hiyo huwezi ukatangaza Maeneo ya udhibiti   kwenye eneo la vijiji. Kuna vijiji zaidi ya 14 na watu tumewaona kwenye picha sasa kilichofanywa na Dkt Pindi Chana na ninaambiwa ana PHD ya Sheria, Miaka kumi iliyopita kuna siku nilisema “Waliozoea vya kunyonga vya kuchinja hawaviwezi, walio zoea kufanya haramu halali hawaiwezi”.  Wamekuwa wanasema waziri mkuu muongo, tulikua na waziri anaitwa Sospeter Muhongo sasa tuna waziri mkuu anaitwa Majaliwa Muongo. Waziri mkuu na wapambe wake wote waliounga mkono haya ya Serikali ya huyu anayeitwa mama, wengi wanasema hili eneo linatengwa kwa ajili ya uhifadhi sasa hoja yangu ya nne ni kwamba hakuna uhifadhi wowote ule eneo hili linatengwa kwa ajili ya uwindaji, Kwenye maeneo yaliyotengwa kama game reserve au kama Maeneo ya udhibiti  moja ufugaji umepigwa marufuku iwe ni kwenye Maeneo tengefu ya wanyama pori  au Maeneo ya udhibiti. Kumbuka kwenye Maeneo tengefu ya wanyama pori watu wanalipwa fidia na wanaondoka na hawawezi kutangaza katika eneo la vijiji peke yake kwa maana hiyo watu hawawezi kwenda kuchunga kwasababu sio eneo lao. Kwahiyo katika maeneo yote mawili kuchunga wanyama kumepigwa marufuku, kwenye maeneo tengefu ya wanyamapori imepigwa marufuku kabisa na kwenye Maeneo ya udhibiti  ni marufuku mpaka upate kibali cha maandishi kwa mkurugenzi wa wanyama pori kwahiyo mmasai akitaka kuchunga ni lazima aende Dar es salaam au Dodoma kwenye ofisi ya mkurugenzi wa  wanyamapori kuomba kibali.  Hata hivyo uwindaji kwa mujibu wa kifungo cha 20 (2) uchomaji, kukamata wanyama, kuua, kujeruhi, kuvua samaki imeruhusiwa kama umepata leseni ya mkurugenzi wa wanyama pori, haya maeneo mawili wamesema yametengwa kwa ajili ya uhifadhi ni uongo yametengwa kwa ajili ya uwindaji. Kwa Sababu sheria inasema uwindaji uchomaji, kukamata wanyama, kuua wanyama, kujeruhi, au kusumbua wanyama au samaki inaruhusiwa kama umepata kibali cha mkurugenzi wa wanyama pori na serikali yao ndio wanafanya biashara kubwa na makampuni yanayokuja kuwinda ya kitalii kwa kutumia vifungu hivi, kwahiyo haya  maeneo mawili yamepokonywa kwa wananchi ili yagaiwe kwa wawindaji wa kitalii sio kwa ajili ya kutengwa kwa uhifadhi. Kulikuwa na maneno mengine kwamba haya ni mazalia ya wanyama hii habari nayo ni ya uongo kwa sababu maeneo yanayotengwa kwa ajili ya mazalia ya wanyama yanaitwa “Breeding and disposal area” kwenye sheria na utaratibu wa kuyatenga upo tofauti na huu ambao amezungumza huyu waziri wa sheria Dkt Pindi Chana. Kwahiyo hayajatengwa kwa ajili ya mazalia ya wanyama bali uwindaji kwasababu ni maeneo yanayoruhusu uwindaji, kuua wanyama kujereuhi wanyama na kusumbua wanyama au samaki. Vile vile haya ni maeneo ambayo endapo kukagundulika madini yanaweza kutengwa kwa ajili ya uchimbaji wa madini kwasababu sheria imesema maeneo haya uchimbaji wa mafuta, gesi asilia, au urani unaruhusiwa baada ya kufanyika kwa masharti ya kimazingira na taratibu nyingine kama kulipa ushuru.  Kumbukeni kwa wale wafatiliaji wa madini moja ya maeneo yaliyogundulika kuna madini ya oil exploration ni bonde la Natron na hizi km 450 za maeneo haya kuna eneo la magharibi linalopakana na Serengeti national park na eneo la mashariki linalokaribia Lake Natron, nafikiri litakuwa sehemu ya lake Natron ambalo ni eneo mojawapo lililotengwa kwa ajili ya oil exploration block kwa taarifa zangu za miaka ya nyuma Lake Natron ni eneo ambalo lilitengwa na TPDC.  Waziri wa maliasili na utalii alipewa mamlaka ya kutangaza maeneo ambayo zamani yalikuwa ni game Control Area kwa sheria ya 1951 kama ilivyobadilishwa na sheria 1974, anataka yaendelee kuwa Game Control Area. Kabla ya sheria hii ya sasa kutungwa sheria iliyokuwa inatumika ni ya mwaka 1974 (Wildlife conservation Areas act ) Na kabla ya mwaka 1974 sheria iliyokuwa inaitwa FAUNA PROTECTION ORDINANCE, Kwahiyo haya maeneo yamekuwa Game Control Area yakayuhishwa  na wakoloni mpaka mwaka 1974 na yakaendelea kuwa Game Control Area mpaka 2009.  Ilipotungwa sheria ya sasa kwenye kifungu cha 16 inasema waziri anatakiwa atangaze ni maeneo gani yaliyokuwa Game Control Areas anataka yaendelea kuwa hivyo. Kwa hiyo hakukuwa na muendelezo wa haya maneno, kuna mbunge mmoja alizungumza alisema kwamba haya maeneo yalikuwa Game Control Area toka 1951 chini ya sheria ya fauna, na yakaacha kuwa Game Control Area mwaka 2009 kwasababu sheria hii mpya ilimtaka waziri ndani ya  mwaka mmoja tu ya kutangaza kuwa ni maeneo yapi anataka yaendeleee kuwa Game Control Area, alipewa mwaka mmoja tu. Sasa waziri ametangaza hili eneo wiki iliyopita yaani miaka 12 baada ya muda wa kutangaza kupita, sasa kwenye sheria zetu za ardhi ukinyanganywa ardhi miaka 12 usiipoidai sio ya kwako tena.  Waziri alipewa mwaka mmoja tu akalalia haki yake kwa miaka 12 imekula kwake, alichokifanya wiki iliyopita ni haramu tupu na hana mamlaka ya kutangaza eneo kuwa Game Control Area.  Kwa mamlaka aliyopewa mwaka 2009 na hana mamlaka ya kutangaza maneno ya ardhi ya vijiji kuwa Game Control Area, walizoea vya kunyonga vya kuchinja hawaviwezi, waliozoea vya haramu vya halali hawaviwezi, hii ni serikali ya kunyonganyonga tu, ushahidi ni huu hapo sijauliza kwamba kulifanyika mashauriano kati ya waziri na halmashauri ya vijiji kuhusu hayo makubaliano kwa vile wamewakamata viongozi wa vijiji nahisi hakukuwa na mashaurinao nao.  Naomba nipendekeze jambo la haraka sana, nawaombeni sana tafuteni watu (wananchi) waliopo katika hilo eneo kupendekeza maombi ya Judicial Review yapelekwe mahakama kuu kanda ya Arusha, mkaombe amri ya mahakama ya Certiorari kufuta hili tangazo la waziri kwa  hoja ya kwamba Waziri hana mamlaka ya kutangaza haya maeneo kuwa Game Control Area, Kwa Sababu ni ardhi ya vijiji na pili mamlaka yake yaliisha mwaka 2009 kwa sababu mamlaka yake yalikua ya mwaka mmoja tu na yaliiisha mwaka 2010. Hili tangazo kwa jinsi nilivyo fundishwa na Profesa shivji na marehemu prof, Mwaikusa ni kwamba hili Tangazo la Dr Pindi Chana mwenyekiti wangu wa amani wa kamati ya sheria na katiba bungeni ni tangazo ambalo ni ULTRA VIRES Wildlife Conservation Area act, Ni tangazo lililotungwa nje ya mamlaka ya sheria ya wanyamapori.  Pelekeni hiyo application ya judicial review na tuta piga kelele kweli kweli ili Majaji wajue kwamba tunaangalia kwa macho yote kwa chochote watakachofanya, kisheria tu hili tangazo haliwezi kudumu nusu saa kwa hoja za Kibatala na Mtobesya na timu yao. Kwahiyo nawaombeni sana wanasheria wa Ngorongoro na vijana mnaonisikiliza kwa sababu ni ardhi yenu jitokezni muwe wadai katika hiyo hiyo application itakayopelekwa Arusha kusikilizwa.   #StopMaasaiEviction #ChangeTanzania

Read More Download Document

The Search For Volcanic Heat Sources In Tanzania: A Helium Isotope Perspective

Tanzania is characterized by unique volcanoes. Most of those volcanoes are located within the eastern and western branches of the Cenozoic East African Rift. Latest helium and neon isotope investigations of lavas and xenoliths are indicating a super-plume beneath East Africa (Halldórsson et al. 2014). Additionally, to the distinction between plume and non-plume related volcanism, helium isotope analyses are a versatile tool for relating geothermal resources to any type of volcanic heat source. In Tanzania there are several distinct areas with significant geothermal surface manifestations: (i) Mwanza region in the N, (ii) Arusha region in the NE, (iii) Dodoma region in central Tanzania, (iv) Dar es Salaam region in the E, (v) Kigoma region in the W and (vi) Mbeya region in the SW. Helium isotope data of Ruhoi hot spring in E Tanzania does not show any indications of a volcanic heat source in contrast to Ngozi-Songwe geothermal system in SW Tanzania (Kraml et al. 2014a, b). In N Tanzania (data this study) the normalized 3He/4He ratio (R/Ra) of the Kogaja mineralized spring indicates crustal helium. Also the Maji Moto hot spring is characterized by non-volcanic gas as indicated by the carbon isotopic composition of CO2. In NE Tanzania the R/Ra values of Ol Doinyo Lengai fumaroles indicates a mantle composition (Fisher et al. 2009, Barry et al. 2013). The Isotopic composition of Lake Natron hot springs (Barry et al. 2013) is dominated by crustal helium but show a small but significant mantle component due to the proximity to Ol Doinyo Lengai, whereas R/Ra of Lake Manyara hot spring (Pik et al. 2006) indicates crustal helium. In W Tanzania noble gas isotope data is only available for Lake Rukwa area (Pik et al. 2006; Danabalan et al. 2016) indicating crustal compositions. Hydrothermal emanations at the floor of Lake Tanganyika (D.R.C.) are characterized by a magmatic carbon isotopic composition of CO2 (Botz & Stoffers 1993). The implications of a crustal or magmatic helium and/or carbon isotopic composition (and supporting evidence) are discussed concerning the existence of viable geothermal heat sources at individual sites of major Tanzanian geothermal areas. 1. INTRODUCTION Tanzania is characterized by unique volcanoes like (i) Ol Doinyo Lengai, the only active carbonatite volcano, (ii) Kilimanjaro, the highest African volcano (5895 m) with a glacier on top, (iii) Ngorongoro Crater, the world's largest, intact, and unfilled volcanic caldera and (iv) Igwizi Hills, the youngest Kimberlite on earth. Most of those volcanoes are located within the eastern and western branch of the Cenozoic East African Rift. However, Igwizi Hills volcano is situated in the middle of the Tanzanian craton. Latest helium and neon isotope investigations of lavas and xenoliths (in conjunction with seismic tomography and Sr-Nd-Pb isotope studies) indicate a super-plume beneath East Africa (Halldórsson et al. 2014). Additionally, to the distinction between plume and non-plume related volcanism, helium isotope analysis is a versatile tool for relating geothermal resources to any type of volcanic heat source. Isotopic ratios of noble gases (3He/4He, 40Ar/36Ar) are very useful to determine the source of the gases, because they are unaffected by fractionation during degassing of the magma (Fischer et al. 2009). Also, noble gas isotope analyses are especially useful in case of blind geothermal systems (e.g. Dobson et al. 2015; Kraml et al. 2016). In case of samples from hot springs, the residence time of the fluid within the (Precambrian) earth crust will cause an addition of radiogenic helium (4He) altering the ratio towards more crustal compositions. Therefore, the interpretation of fluid helium isotope data is not as straightforward as 3He/4He ratios of primary lavas lacking crustal contamination. However, this apparent disadvantage can be turned into an advantage: Within the TRACE research project in the Upper Rhine (non-magmatic) Rift, Germany we have found indications for a relation of residence time and permeability at depth, i.e. the shorter the residence time ( high 3He/4He ratios) the higher the permeability (Kraml et al. 2016). In Tanzania are several distinct areas with significant geothermal surface manifestations: (i) N Tanzania (Mwanza region) e.g. Maji Moto hot spring within the Precambrian Tanzania Craton, (ii) NE Tanzania (Arusha region) e.g. Lake Natron hot springs near Ol Doinyo Lengai within the eastern branch of the East African Rift System (EARS), (iii) central Tanzania e.g. Lake Balangida hot springs within the Manyara-Dodoma segment of the EARS (eastern branch), (iv) E Tanzania (Dar es Salaam region) e.g. Ruhoi hot spring within a sedimentary coastal basin, (v) W Tanzania (Kigoma region) e.g. Uvinza saline springs within the Precambrian basement and (vi) SW Tanzania (Mbeya region) e.g. Songwe hot springs downstream of Ngozi volcano within the western branch of the EARS. The interpretation of helium isotope data from E and SW Tanzania was already published by Kraml et al. (2014a, b). In this paper, only the implications of the helium isotopic composition for the existence of viable geothermal heat sources are discussed for the individual sites of the remaining Tanzanian geothermal areas considering further e.g., petrologic supporting evidence…...

Read More Download Document