- October 25, 2021
- Posted by: Adminct
- Category: leadership-Report
No Comments

Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi imesema Ijumaa Februari 18, 2022 itatoa uamuzi iwapo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu wana kesi ya kujibu au la katika kesi ya ugaidi inayowakabili.
Jaji Joachim Tiganga anayesikiliza kesi hiyo amesema hayo leo Jumanne Februari 15, 2022 baada ya upande wa mashtaka kuieleza mahaka kuwa wamefunga kesi hiyo kwa shahidi wa 13 kuhitimisha ushahidi wake.
Shahidi huyo wa 13 wa upande wa mashtaka ambaye ni Mkaguzi wa Polisi, kutoka Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi, Mkoa wa Kipolisi Temeke, Tumaini Swila amemaliza kutoa ushahidi baada ya kuhojiwa maswali ya dodoso na upande wa utetezi.